picha

Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa

Utajifunza sababua zinazopelekea kuhisi maumivu makali ya tumbo baada ya kumaliza tendo la ndoa

Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa

MAUMIVU YA TUMBO BAADA YA TENDO LA NDOA




Mara nyingi maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa sio tatizo sana kiasi cha kuogopa. Kwani hali hii husababishwa na gesi iliyoppntumboni mama kama uume ulikuwa ukiingia ndani sana, na hii hutokea endapo uume ni mrefu sana ama mtindo uliotumika katika tendo la ndoa. Tatizo la kupatwa na maumivu wakati wa tendo la ndoa ama baada hutambulika kama dyspareunia.



Inakadiriwa kuwa asilimia 10 mapka 20 ya wanawake huweza kusumbuliwa na tatizo hili. Ila pia tatizo hili si kwa wanawake tu hutokea pia kwa wanaume, ila kwa kiasi kidogo yapata lamda asilimia 5. lakini tatizo hili linatibika bila ya wasi hivyo si vyema kuendelea kuteseka.



Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa.
Tofauti na sababu ya ya gesi ama uume kuingia ndani sana, tatizo hili linaweza kusababishwa na mambo yafuatayo:-



1.Fikra, hisia na mawazo ya mtu. Hii hutokea kama mtu ana misongo ya mawazo kibao, ama ana woga juu ya tendo la ndoa ama mahusianao yake na ya mwenzie sio mazuri lamada amembaka ama kumlazimisha, haya yote yanaweza kutengeneza mazingira ya kuumwa na tumbo baada ya tendo.



2.Endapo tendo la ndoa litafanyika kwa kiasi kuwa uume uliingia ndani sana. Hii inaweza kusababisha maumivu ya tumbo, ila ni ya muda mfupi na yataweza kuondoka baada ya kupumzika. Ni vyema kubadili mikao ama kupunguza kukandamiza sana uume.



3.Wakati mwingine hali huweza kutokea endapo mwanamke ameingia kileleni. Wakati wa kufika kileleni misuli inayozungukia mfumo wa uzazi, maeneo ya kiunoni na nyonga misuli hii kusinjaa na kujikaza na kusababisha maumivu ya chini ya tumbo. Hali jii kitaalamu hufahamika kama dysorgasmia.



Watu wanaosumbuliwa sana tatizo hili ni:-
A.Wajawazito
B.Wenye matatizo kwenye ovari
C.wenye mashambulizi ya kwenye mfumo wa uzazi (PID)
D.Wenye matatizo kwenye korodani.



4.Gesi; wakati wa kupushi uume ndani unaweza kupushi hewa kuingia ndani ya tumbo. Sasa kama hewa hii itanaswa sehmemu humo ndani inaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa juu ama kifuani. Mtu anaweza kuhisia kama gesi inatembea tumboni na maumivu haya yanaweza kuelekea maeneo mengine ya mwili.



5.Kama mtu anasumbuliwa na UTI
UTI inaweza kuwa ni katika sababu za maumivu haya. Mtu pia anaweza kuhisi dalili kama
A.Maumivu wakati wa kukojoa kama anaungua
B.Kukojoa mara kwa mara
C.Mkojo kuwa mchafu
D.Kuwa na damu kwenye mkojo
E.Maumivu ya mkundu.



6.Kuwa na maradhi ya ngono kama gonoria na chlamydia. Pia mtu anaweza kuona dalili kama:
A.Kutoa harufu mbaya sehemu za siri
B.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
C.Maumivu wakati wa kukojoa



7.Kama mfuko wa uzazi umeinama, hii inaweza kupelekea kuguswa kwa mfukowa uzazi wakati wa tendo la ndoa hivyo kupelekea maumivu



8.Kama kunashida kwenye ovari




9.Kama kuna uvimbe kwenye kizazi. Dalili zake ni kama
A.Kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi
B.Hedhi kutokata ndani ya siki 7
C.Kukosa choo
D.Maumivu ya miguu ama mgongo



10.Kama mirija ya falopia imeziba.



11.Kama mwanaume ana maradhi kwenye mfumo wa uzazi.





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 14015

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 web hosting    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike

Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume.

Soma Zaidi...
Mimba iliyotunga nje

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya

Soma Zaidi...
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Njia za uzazi wa mpango kwa akina Mama kuanzia miezi sita baada ya kujifungua mpaka mwaka mmoja

Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango kwa mama aliyejifungua kuanzia miezi sita mpaka mwaka mmoja.

Soma Zaidi...
Sababu za kutoona hedhi kwa wakati

Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.

Soma Zaidi...
Madhara ya mwili kushindwa kutengeneza projestron ya kutosha

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo mtu anaweza kupata ikiwa mwili utaeweza kutengeneza progesterone ya kutosha.

Soma Zaidi...
Je? Naomba kuuliza mkewangu ali ingiya kwenye hezi siku tatu damu ikakata nikakutana nae siku ya nane je? Anaweza pata ujauzito

Idadi ya siku hatari za kupata mimba hutofautiana kutoka kwa mwanamke mmoja namwinhine. Kinda ambao idadivyavsikuvzao za hatari ni nyingi kuliko wengine.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba ya watoto mapacha

Makala hii itakwenda kukupa dalili ambazo zinaonyesha kuwa mimba ni ya mapacha. Dalili hizi zitahitajika kuthibitishwa na kipimo cha daktari ili kujuwa kuwa ni kweli.

Soma Zaidi...