Utajifunza sababua zinazopelekea kuhisi maumivu makali ya tumbo baada ya kumaliza tendo la ndoa
MAUMIVU YA TUMBO BAADA YA TENDO LA NDOA
Mara nyingi maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa sio tatizo sana kiasi cha kuogopa. Kwani hali hii husababishwa na gesi iliyoppntumboni mama kama uume ulikuwa ukiingia ndani sana, na hii hutokea endapo uume ni mrefu sana ama mtindo uliotumika katika tendo la ndoa. Tatizo la kupatwa na maumivu wakati wa tendo la ndoa ama baada hutambulika kama dyspareunia.
Inakadiriwa kuwa asilimia 10 mapka 20 ya wanawake huweza kusumbuliwa na tatizo hili. Ila pia tatizo hili si kwa wanawake tu hutokea pia kwa wanaume, ila kwa kiasi kidogo yapata lamda asilimia 5. lakini tatizo hili linatibika bila ya wasi hivyo si vyema kuendelea kuteseka.
Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa.
Tofauti na sababu ya ya gesi ama uume kuingia ndani sana, tatizo hili linaweza kusababishwa na mambo yafuatayo:-
1.Fikra, hisia na mawazo ya mtu. Hii hutokea kama mtu ana misongo ya mawazo kibao, ama ana woga juu ya tendo la ndoa ama mahusianao yake na ya mwenzie sio mazuri lamada amembaka ama kumlazimisha, haya yote yanaweza kutengeneza mazingira ya kuumwa na tumbo baada ya tendo.
2.Endapo tendo la ndoa litafanyika kwa kiasi kuwa uume uliingia ndani sana. Hii inaweza kusababisha maumivu ya tumbo, ila ni ya muda mfupi na yataweza kuondoka baada ya kupumzika. Ni vyema kubadili mikao ama kupunguza kukandamiza sana uume.
3.Wakati mwingine hali huweza kutokea endapo mwanamke ameingia kileleni. Wakati wa kufika kileleni misuli inayozungukia mfumo wa uzazi, maeneo ya kiunoni na nyonga misuli hii kusinjaa na kujikaza na kusababisha maumivu ya chini ya tumbo. Hali jii kitaalamu hufahamika kama dysorgasmia.
Watu wanaosumbuliwa sana tatizo hili ni:-
A.Wajawazito
B.Wenye matatizo kwenye ovari
C.wenye mashambulizi ya kwenye mfumo wa uzazi (PID)
D.Wenye matatizo kwenye korodani.
4.Gesi; wakati wa kupushi uume ndani unaweza kupushi hewa kuingia ndani ya tumbo. Sasa kama hewa hii itanaswa sehmemu humo ndani inaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa juu ama kifuani. Mtu anaweza kuhisia kama gesi inatembea tumboni na maumivu haya yanaweza kuelekea maeneo mengine ya mwili.
5.Kama mtu anasumbuliwa na UTI
UTI inaweza kuwa ni katika sababu za maumivu haya. Mtu pia anaweza kuhisi dalili kama
A.Maumivu wakati wa kukojoa kama anaungua
B.Kukojoa mara kwa mara
C.Mkojo kuwa mchafu
D.Kuwa na damu kwenye mkojo
E.Maumivu ya mkundu.
6.Kuwa na maradhi ya ngono kama gonoria na chlamydia. Pia mtu anaweza kuona dalili kama:
A.Kutoa harufu mbaya sehemu za siri
B.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
C.Maumivu wakati wa kukojoa
7.Kama mfuko wa uzazi umeinama, hii inaweza kupelekea kuguswa kwa mfukowa uzazi wakati wa tendo la ndoa hivyo kupelekea maumivu
8.Kama kunashida kwenye ovari
9.Kama kuna uvimbe kwenye kizazi. Dalili zake ni kama
A.Kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi
B.Hedhi kutokata ndani ya siki 7
C.Kukosa choo
D.Maumivu ya miguu ama mgongo
10.Kama mirija ya falopia imeziba.
11.Kama mwanaume ana maradhi kwenye mfumo wa uzazi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal
Soma Zaidi...Hizi ni siku za hatari kupata ujauzito.Siku hizi ndio siku za kupata mimba kwa urahisi
Soma Zaidi...Tendo la ndoa wakati wa siku za hedhi ni halia mbayo jamii nying zinakataza. Katika vitabu vya dini pia haviruhusu, hata ki saikolojia utaona kuwa sio jambo jema. Hata hivyo hapa ninakuletea madhara yake kiafya
Soma Zaidi...Ni Swali kila mjamzito anataka kujiuliza hasa akiwa katika mimba ya kwanza. Wengine wanataka kujuwa ni muda gani anujuwe mavazi makubwa. Kama na wewe unataka kujuwa muda ambao tumbo huwa kubwa, endelea kusoma.
Soma Zaidi...Kutoka na majimaji ka uchache kwa mwanamke sio jambo lakishangaa sana. Damu hii inawezapiabkikbatana damu na maumivu makali.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuz
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, hali hii utokea kwa watoto wadogo wakati wa kuzaliwa kwa sababu maalum kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Nitakujulisha siku ya kupata mimba na sifa zake, na namna ya kuweza kuitafuta
Soma Zaidi...KUVIMBA VYA MIGUU KWA WAJAWAZITO Kuvimba kwa miguu ni hali inayowapara wengi katika wajawazito.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi na uvimbe katika mirija ya uzazi. Mara nyingi hutumiwa sawa na ugonjwa wa uvimbe kwenye fupa nyonga (PID), ingawa PID haina ufafanuzi sahihi na inaweza kurejelea magonjwa kadhaa ya njia ya juu ya uzazi
Soma Zaidi...