Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.
Uchafu kutoka ukeni na rangi zake.
1. Kuna uchafu wenye rangi ya kahawia na uambatana na damu.
Uchafu huu unaweza kutoka kwa wale ambao wanaingia kwenye siku zao za mwezi na wale ambao wameshamaliza, kwa wale wanaoingia kwenye siku zao za mwezi inawezekana ni kubadilika kwa mzunguko ila kwa wale ambao washamaliza inawezekana ika ni kansa ya kizazi.
2.Angalizo kwa akina Mama ambao wameshamaliza taratibu za mzunguko wa damu na wakaona tena damu inatoka ni vizuri kuwahi mapema hospitali kwa uchunguzi zaidi ili kuangalia shida ni nini kwa sababu kuna akina Mama wengine wakiona mambo kama hayo wanaficha, sio vizuri kuficha ni lazima kuweka wazi ili kupata msaada zaidi.
3. Pia kuna uchafu wenye rangi ya njano ikiambatana na harufu mbaya.
Aina hii ya rangi ya njano na harufu mbaya utokana na kuwepo kwa Magonjwa ya zinaa kwa hiyo mtu akipata anapaswa kutibiwa Magonjwa haya.
4. Pengine kuna uchafu mweupe mzito kama jibini hii ni aina ya uchafu ambao hutokea kwa wanawake ambao una maana ya kuwepo kwa mashambulizi ya tangazo kwenye via vya uzazi.
5. Kuna na uchafu mwingine unakuwa mweupe au wa kijivu wenye harufu ya samaki .
Pia uchafu wa aina hiyo unaonyesha juwa kuna Maambukizi ya kandaida kwenye via vya uzazi kwa hiyo ni lazima kupima na kutumia dawa.
6 . Kwa hiyo kama tulivyoona aina mbalimbali za uchafu na harufu zake tunapaswa kuziangalia kwa makini na kujua shida ni nini kama hujaelewa vizuri unaweza nkumwona mtaalamu yeyote wa afya ili kuweza kupata msaada zaidi kwa sababu Magonjwa yanayoshambulia sehemu za siri Usababisha madhara mengi ambayo ni kansa na ugumba.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Saratani ya matiti ji moja kati ya saratani zinazosumbuwa wqnawake wengi. Katika somo hili utajifunza chanzo cha kutokea saratani ya matiti
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa sababu zinazoweza kupelekea uke kuwa mkavu yaani kukosa majimaji wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.
Soma Zaidi...