Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun
Mbinu za kupunguza tatizo la saratani kwa watoto.
1.Kwanza kabisa akina Mama wakati wa ujauzito wanapaswa kuhudhuria maudhurio yote ya kliniki ili kuweza kupata mafundisho mbalimbali yanayohusu namna ya kuishi wakati wa ujauzito ili kuweza kupata mtoto ambaye hana matatizo yoyote.
2 . Lakini cha kushangaza Mama anaanza mahudhurio ya kliniki mimba ikiwa na miezi sita au saba kusema ukweli hata kama mama anapata mafundisho aameshaharibu kama ni maisha yasiyo ya kawaida kwa mimba ameshafanya na mimba sasa ni kubwa, kwa hiyo akina Mama mnapaswa kujali hali zenu na kutunza watoto wenu vizuri kwa hiyo tuwatunze watoto wetu ili waweze kuwa na afya njema na tushirikiane kuitokomeza janga la saratani kwa watoto wetu.
3. Akina Mama wanapaswa kuepuka kabisa matumizi ya sigara wakati wa ujauzito kwasababu moshi wa sigara unaweza kuingia kwenye plasenta na kusababisha maambukizi kwenye sehemu ya plasenta hali ambayo Usababisha kiwango cha kupelekea chakula kutoka kwenye plasenta kwenda kwa mtoto kubwa na hitilafu kubwa hatimaye mtoto uzaliwa akiwa na Dalili za saratani.
4. pia moshi wa sigara usababisha kupunguza kwa vichiocheo vya progesterone na oestrogen na pia katika kufanyika kwa mtoto moshi wa sigara unaweza kusababisha sehemu nyingine kutokamilika vizuri na kusababisha mapungufu kwa mtoto ambayo Usababisha saratani kwa watoto.kwa hiyo akina Mama ni vizuri kuachana na matumizi ya sigara wakati wa ujauzito ili kuweza kumpatia mtoto nafasi ya kukua vizuri akiwa tumboni na akizaliwa awe na afya njema kama watoto wengine.
5. Akina mama wanapaswa kukamilisha kwa chanjo za watoto wao, tunajua kubwa chanjo kwa watoto na kwa mama akiwa na mimba ni lazima kuchomwa sindano ya Tetunus kwa ajili ya Mama na mtoto na pia mtoto akizaliwa anapaswa kutumia chanjo zote na kuzimaliza kwa wakati chanjo hizi ni kama vile, chanjo ya kifua kikuu ambayo utolewa kwenye bega la kulia , hii chanjo utolewa tu mtoto anapozaliwa, chanjo ya pili ni chanjo ya polio ambayo uzuia kupooza na utolewa baada ya kuzaliwa, wiki ya sita, wiki ya Kumi mpaka mwisho wiki ya Kumi na nne.
6.Chanjo nyingine ni chanjo ya kuzuia kuharisha ambayo kwa kitaalamu huitwa Rotarix ambayo utolewa kwa matone, chanjo hiyo utolewa wiki ya sita na wiki ya Kumi, pia chanjo nyingine ni chanjo inayoitwa pentavalent ambayo inatibu Magonjwa matano Nayo utolewa kwenye wiki ya sita, kumi na kumi na nne, pia chanjo nyingine ni chanjo inayotibu upumuaji na magonjwa ya Nimonia nayo utolewa kwenye wiki ya sita, wiki ya Kumi na wiki ya Kumi na nne na nyingine ni chanjo ya Surua ambayo utolewa kwenye wiki ya nane na kumi na tano, kwa hiyo mtoto akipokea chanjo zote ni mara chache kupata magonjwa ya saratani.
7. Kupunguza uharibifu wa hewa kwenye nyumba.
Kwa wakati mwingine mtoto anaweza kupata ugonjwa huu wa saratani kwa sababu ya kuwepo kwa uharibifu wa hewa kwenye nyumba kwa sababu nyumba nyingine unakuta kuna mionzi mikali na mambo kama hayo ambayo yanaweza kusababisha kuwepo kwa uharibifu kwenye afya wa mtoto , kwa kawaida weka nyumba katika hali ya usafi pamoja na hewa safi.
8. Watoto wadogo wasikae Juani kwa mda mrefu.
Tunajua wazi kuwa mionzi ya jua huwa ni hatari kwa kusababisha saratani kwa hiyo ngozi ya watoto wadogo ,inakuwa bado ni raini na zinaweza kupitisha mwanga kwa urahisi kwa hiyo ni vizuri kutowaweka watoto wadogo kwenye mwanga wa jua kwa sababu ni hatari unaweza kusababisha saratani kwa watoto wadogo.kwa hiyo wazazi wanapaswa kuwaambia wanafamilia wote ili wasiweze kuwapeleka watoto wadogo kwenye mwanga wa jua.
9. Mpeleke mtoto mwenye Dalili za saratani hospitali kwa matibabu zaidi.
Kuzama ukweli watu wameshajiwekea imani kubwa saratani hauponi hiyo si kweli kwa sababu saratani ukiwahi pake inapokuwa kwenye hatua za mwanzoni kupona ni rahisi, lakini ukisubiri kwenda hospitalini kwenye dakika za mwisho na za Maambukizi yameshakuwa mengi sana kupona ni vigumu kwa hiyo tunapaswa kuwahi hospitali ili tuweze kupata matibabu mapema.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Kupungua kwa idadi ya mbegu za kiume kunamaanisha kuwa Majimaji (shahawa) unayotoa wakati wa kufika kileleni huwa na mbegu chache kuliko kawaida. Hesabu yako ya manii inachukuliwa kuwa chini kuliko kawaida ikiwa una chini ya mbegu milioni 15. Kuwa na idad
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...KubaleheΓΒ ni wakati mwili wa mtoto unapoanza kubadilika na kuwa wa mtu mzima (balehe) hivi karibuni. Kubalehe ambao huanza kabla ya umri wa miaka 8 kwa wasichana na kabla ya umri wa miaka 9 kwa wavulana.
Soma Zaidi...Nimesoma makala yenu, sasa nina swaliJe kitunguu saumu kina madhara kwa Mgonjwa wa figo?
Soma Zaidi...Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil
Soma Zaidi...Je unaweza kunielezaKwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kutibu tatizo la ugumba kwa Mwanaume, ni njia ambazo utumiwa na wataalam mbalimbali Ili kuweza kutibu tatizo la ugumba kwa wanaume.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke.
Soma Zaidi...