picha

Mbinu za kuwakinga watoto na saratani.

Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun

Mbinu za kupunguza tatizo la saratani kwa watoto.

1.Kwanza kabisa akina Mama wakati wa ujauzito wanapaswa kuhudhuria maudhurio yote ya kliniki ili kuweza kupata mafundisho mbalimbali yanayohusu namna ya kuishi wakati wa ujauzito ili kuweza kupata mtoto ambaye hana matatizo yoyote.

 

2 . Lakini cha kushangaza Mama anaanza mahudhurio ya kliniki mimba ikiwa na miezi sita au saba kusema ukweli hata kama mama anapata mafundisho aameshaharibu kama ni maisha yasiyo ya kawaida kwa mimba ameshafanya na mimba sasa ni kubwa, kwa hiyo akina Mama  mnapaswa kujali  hali  zenu na kutunza watoto wenu vizuri kwa hiyo tuwatunze watoto wetu ili waweze kuwa na afya njema na tushirikiane kuitokomeza janga la saratani kwa watoto wetu.

 

3. Akina Mama wanapaswa kuepuka kabisa matumizi ya sigara wakati wa ujauzito kwasababu moshi wa sigara unaweza kuingia kwenye plasenta na kusababisha maambukizi kwenye sehemu ya plasenta hali ambayo Usababisha kiwango cha kupelekea chakula kutoka kwenye plasenta kwenda kwa mtoto kubwa na hitilafu kubwa hatimaye mtoto uzaliwa akiwa na Dalili za saratani.

 

 4. pia moshi wa sigara usababisha kupunguza kwa vichiocheo vya progesterone na oestrogen na pia katika kufanyika kwa mtoto moshi wa sigara unaweza kusababisha sehemu nyingine kutokamilika vizuri na kusababisha mapungufu kwa mtoto ambayo Usababisha saratani kwa watoto.kwa hiyo akina Mama ni vizuri kuachana na matumizi ya sigara wakati wa ujauzito ili kuweza kumpatia mtoto nafasi ya kukua vizuri akiwa tumboni na akizaliwa awe na afya njema kama watoto wengine.

 

5. Akina mama wanapaswa kukamilisha kwa chanjo za watoto wao, tunajua kubwa chanjo kwa watoto na kwa mama akiwa na mimba ni lazima kuchomwa sindano ya Tetunus kwa ajili ya Mama na mtoto na pia mtoto akizaliwa anapaswa kutumia chanjo zote na kuzimaliza kwa wakati chanjo hizi ni kama vile, chanjo ya kifua kikuu ambayo utolewa kwenye bega la kulia , hii chanjo utolewa tu mtoto anapozaliwa, chanjo ya pili ni chanjo ya polio ambayo uzuia kupooza na utolewa baada ya kuzaliwa, wiki ya sita, wiki ya Kumi mpaka mwisho wiki ya Kumi na nne.

 

6.Chanjo nyingine ni chanjo ya kuzuia kuharisha ambayo kwa kitaalamu huitwa Rotarix ambayo utolewa kwa matone, chanjo hiyo utolewa wiki ya sita na wiki ya Kumi, pia chanjo nyingine ni chanjo inayoitwa pentavalent ambayo inatibu Magonjwa matano Nayo utolewa kwenye wiki ya sita, kumi na kumi na nne, pia chanjo nyingine ni chanjo inayotibu upumuaji na magonjwa ya Nimonia nayo utolewa kwenye wiki ya sita, wiki ya Kumi na wiki ya Kumi na nne na nyingine ni chanjo ya Surua ambayo utolewa kwenye wiki ya nane na kumi na tano, kwa hiyo mtoto akipokea chanjo zote ni mara chache kupata magonjwa ya saratani.

 

7. Kupunguza uharibifu wa hewa kwenye nyumba.

Kwa wakati mwingine mtoto anaweza kupata ugonjwa huu wa saratani kwa sababu ya kuwepo kwa uharibifu wa hewa kwenye nyumba kwa sababu nyumba nyingine unakuta kuna mionzi mikali  na mambo kama hayo ambayo yanaweza kusababisha kuwepo kwa uharibifu kwenye afya wa mtoto , kwa kawaida weka nyumba katika hali ya usafi pamoja na hewa safi.

 

8. Watoto wadogo wasikae Juani kwa mda mrefu.

Tunajua wazi kuwa mionzi ya jua huwa ni hatari kwa kusababisha saratani kwa hiyo ngozi ya watoto wadogo ,inakuwa bado ni raini na zinaweza kupitisha mwanga kwa urahisi kwa hiyo ni vizuri kutowaweka watoto wadogo kwenye  mwanga wa jua kwa sababu ni hatari unaweza kusababisha saratani kwa watoto wadogo.kwa hiyo wazazi wanapaswa kuwaambia wanafamilia wote ili wasiweze kuwapeleka watoto wadogo kwenye mwanga wa jua.

 

9. Mpeleke mtoto mwenye Dalili za saratani hospitali kwa matibabu zaidi.

Kuzama ukweli watu wameshajiwekea imani kubwa saratani hauponi hiyo si kweli kwa sababu saratani ukiwahi pake inapokuwa kwenye hatua za mwanzoni kupona ni rahisi, lakini ukisubiri kwenda hospitalini kwenye dakika za mwisho na za Maambukizi yameshakuwa mengi sana kupona ni vigumu kwa hiyo tunapaswa kuwahi hospitali ili tuweze kupata matibabu mapema.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 1680

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Nini husababisha upungufu wa nguvu za kiume

Post hii itakujulidha mambo ambayo hupunguza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Nna mimba ya miez miezi mitano 5 naruhusiwa kula papai kwa wing

Miongoni mwa matunda yenye virutubisho vingi ni pamoja na papai, nanasi, tikiti, palachichi, pera, karoti, hindi na boga. Lakini katika matunda haya yapo ambayo kwa mimba changa anatakiwa awe makini, kama papai na nanasi. Sasa vipi kuhusu mimba ya

Soma Zaidi...
Hatua za ukuwaji was mimba na dalili zake

Somo hili linakwenda kukuletea hatua za ukuaji mimba na dalili zake

Soma Zaidi...
Je matiti kujaa na chuchu kuuma inakua ni dalili za hedhi?

Kuunda na kujaa kwa matiti ni miongoni mwa dalili za ujauzito lakini pia ni dalili za kukaribia hedhi kwa baadhi ya wanawake. Posti hii itakwenda kufafanuabutofauti wa dalili hizi na kipi ni sahihibkatibya hedhi ama ujauzito.

Soma Zaidi...
Damu, majimaji na uteute unaotoka kwenye uke wa Mjamzito, sababu zake na dalili zake

Unataka kujuwa sababu za mjamzito kutokwa na damu, utelezi ama majimaji kwenye uke wake. Na dalili gani zinaashiriwa na majimaji haya

Soma Zaidi...
DALILI ZA UJAUZITO KICHEFU CHEFU, KUTAPIKA, HEDHI, DAMU UKENI, KUJOJOAKOJOA N.K (mimba changa, mimba ya wiki moja, mimba ya mwezi mmoja )

DALILI KUU ZA MIMBA (UJAUZITO) Watu wengi sana wamekuwa wakilalamika kuwa mimba zao zinatoka, ama kupotea bila ya kujulikana tatizo wala bila ya kuugua.

Soma Zaidi...