Maumivu ya tumbo kitomvuni, sababu zake na dalili zake

Hapa utajifunza sababu za kuwepo na maumovu ya tumbe kitomvuni.

Maumivu ya tumbo kitomvuni, sababu zake na dalili zake

Maumivu ya tumbo kitomvuni




Maumivu ya tumbo kwenye kitomvu, yanaweza kuwa ni ishara ya maradhi mengi. Mara nyingi maumivu haya yanaweza kuondoka yenyewe baada ya muda. Ila wakati mwingine yanaweza kuwa ni ishara ya shida za kiafya ambazo huhitaji uangalizi wa daktari kwa haraka. Kwa wanaume huwa henia ikisumbuwa sana eneo hili.



Je na wewe ni mwene kusumbuliwa na maumivu ya tumbo kwenye kitomvu? Makala hii ji kwa ajili yako. Hapa tunakwenda kuona sababu za maumivu ya tumbo kwenye kitomvu, dalili na maradhi yanayohusiana na maumivu ya tumbo kitomvuni. Unaweza kutuachia maoni yako hapo chini.



Eneo hili la kitomvuni kitaalamu hufahamika kama umblical region. Eneo hili la tumbo linahusisha viungo kama tumbo la chakula, utumbo mdogo, utumbo mkubwa na kongosho. Hivi ni katika viungo muhimu sana katika mmengenyo wa chakula, na afya ya mtu kwa ujumla.



SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI NA DALILI ZAKE




1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.



Dalili zake
Tofauti na kuwa mgonjwa atakuwa anaumwa na tumbo kwenye kitomvu, lakini tumbo hili litafungamana na dalili zifuatazo:-
1.Kuharisha
2.Kichefuchefu
3.Kutapika
4.Homa
5.Kutokwa na jasho sana



2.Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili. Tofauti na kuwepo kwa maumivu haya pia mgonjwa ataona dalili flani.



Dalili za ugonjwa wa appendix
1.Kujaa kwa tumbo na kukaza kama mtu aliye vimbiwa
2.Kichefuchefu
3.Kutapika
4.Kuhisi maumivu ambayo huwa yakiongezeka kila unapokohoa ama unapojongea.
5.Mvurugiko wa tumbo kama kukosa choo au kuharisha
6.Homa
7.Kukosa hamu ya kula.



Ugonjwa huu ni katika magonjwa ambayo yanahitajika kutibiwa mapema na haraka sana. Endapo mgo jwa atachelewa kutibiwa appendix inaweza kupasuka, na endapo itapasuka inaweza kuhatarisha maisha.



3.Vidonda vya tumbo
Yes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum. Tofauti na maumivu ya tumbo kwenye kitomvu pia mgonjwa ataona dalili zifuatazo



Dalili za vidonda vya tumbo:
1.mvurugiko wa tumbo
2.Kuhisi tumbo kujaa na kucheua
3.Kichefuchefu
4.Kutapika
5.Kukosa hamu ya kula
6.Kutoa hewa kwa mdomoni kwa sauti



4.Matatizo kwenye kongosho
Huu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali. Pia zinapoonyesha dalili zake huwa ni kama:-



Dalili za maradhi ya kongosho
1.Kichefuchefu
2.Kutapika
3.Homa
4.Mapigo ya moyo kuongezeka



5.Kuwa na ngriri ya henia
Ugonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.



6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-
1.Mashambulizi ya bakteria
2.Henia
3.Uvimbe
4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.



Dalili
1.Kichefuchefu
2.Kutapika
3.Tumbo kujaa
4.Kupunguwa maji
5.Kukosa hamu ya kula
6.Kukoa choo
7.Homa
8.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo



7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.



Dalili nyingine:-
1.Kupata pumzi kwa tabu
2.Kushuka kwa presha ya damu
3.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
4.Kuzimia
5.Udhoifu wa ghafla upande mmoja wa mwili



8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-
1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
2.Kuona damu kwenye choo





                   



Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1347

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Dalili za ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster. Kwa hiyo ili kugundua kubwa mtu ana Ugonjwa huu Dalili kama hizi zifuatazo zinaweza kutokea kwa mgonjwa.

Soma Zaidi...
Je mtu akapima ukimwi na kile kipimo kidogo .je kina usahihi au la ..na pia kama inaonyesha mistari miwili.

Hivi umeshawahi kuwazakuwa jekipimo cha HIV ni sahihi kwa kiasi gani. Unadhani huwa kinakoseaga kutoa majibu?

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake

Soma Zaidi...
dalili za Uvimbe kwwnye jicho (sty)

Sty ni uvimbe mwekundu, chungu karibu na ukingo wa kope ambalo linaweza kuonekana kama jipu au chunusi. Sties mara nyingi hujazwa na usaha. Mtindo kawaida huunda nje ya kope lako. Lakini wakati mwingine inaweza kuunda kwenye sehemu ya ndani ya kope lak

Soma Zaidi...
Dalili ya pressure ya kupanda

Post ya leo inaenda kufundisha dalili na hatari za presha ya kupanda. Presha ni ugonjwa unaosababishwa na baadhi ya vitu mbalimbali.pressure hujulikana kwa jina lingine ambolo ni hypertension (pressure ya kupanda). presha hugundulika pale ambapo presha ya

Soma Zaidi...
Dalili za kifua kikuu (tuberculosis)

Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kiafya yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex. Kwa binadamu sababu ya kawaida ni Mycobacterium tuberculosis.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Malengelenge sehemu za siri

Malengelenge sehemu za siri ni maambukizi ya kawaida ya zinaa ambayo huathiri wanaume na wanawake. Makala ya malengelenge sehemu za siri ni pamoja na maumivu, kuwasha na vidonda katika sehemu yako ya uzazi. Lakini huenda usiwe na dalili au ishara za mal

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa ,kwa kawaida Ugonjwa huu utokea kuanzia kwenye wiki ya pili mpaka mwaka mmoja na hapo Ugonjwa unakuwa bado haujaonesha Dalili na Dalili zikishaonekana ni vigumu kutibika.

Soma Zaidi...
TIBA YA MINYOO AU DAWA YA MINYOO: praziquantel (biltricide) mebendazole (vermox, emverm) na albendazole (albenza).

TIBA YA MINYOO Moja katika sifa za minyoo ni kuwa wanatibika kwa urahisi pindi mgonjwa akipewa dawa husika.

Soma Zaidi...