Vyanzo vya minyoo

Vyanzo vya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyanzo vya minyoo

Download Post hii hapa

VYNZO VYA MINYOO

Kama tulivyoona hapo mwanzo kuusu aina za minyoo, pia tumeona vyanzo vya minyoo hao kulingana na aina zao. Hapa ninakwenda kukuorodheshea kwa ufupi vyanzo hivi vya minyoo kwa ujumla wao na makundi yao:

 

kula kitu kisichooshwa kwema kwa maji yaliyo safi na salama. Wakati mwingine kuosha tu haitoshelezi, maana unaweza kuosha kwa maji ambayo yana vimelea vya minyoo, hivyo unajikuta hukufanya kitu. Kwani minyoo wanaishi ardhini, kwenye majani na kwenye maji.

Kunywa maji ambayo si masafi na si salama. Maji machafu yanaweza kuwa na mayai ama lava wa minyoo hii. Maji ambayo yamechanganyika na choo kikubwa yanakuwa na mazalia ya minyoo hii. Ni vyema kuchemsha maji hata yachemke, yapozwe na yahifadhiwe vyema kwa matumizi ya nyumbani na hata biashara.

Kula nyama ambayo haikuiva vyema, ama nyama mbichi. Upikaji wa nyama yeyote unatakiwa uwe wa makini sana. Kuhakikisha kuwa nyama imewiva vyema. Kuna baadhi ya nyama zinashauriwa kuwa makini sana katika kuzipika kama nyama ya ngurue na ya punda. Pia kuna aiana za samaki nao wanahitajika kuwapika vyema kama samaki aina ya kaa.

Kutembea pekupeku kwenye ardhi yeye minyoo. Minyoo huweza kuishi kwenye udongo, na ikitokea my akatembea bila ya viatu katika eneo hili, minyoo hawa wanaweza kupenya kwenye ngozi yake na kuingia mwilini.

Kula udongo, tunaona sana mara nyingi watu wanakula udongo, ukweli ni kuwa sio kila udongo unakuwa na minyoo. Kama utakuwa umeandaliwa vyema unaweza kuwa hauna minyoo. Lakini kula udongo kunaweza kusababisha minyoo. Pia kuna madhara makubwa sana ya kiafya katika kula udongo.

Kinyesi cha wanyama na binadamu. Hivi ni vyanzo vizuri sana vya minyoo. Kwani minyoo wanaweza kuishi kwenye kinyesi vyema na kwa muda mrefu zaidi kuliko maeneo mengine.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1317

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende
Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n

Soma Zaidi...
Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika
Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika

DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.

Soma Zaidi...
Presha ya kushuka (hypotension) dalili zake na njia ya kukabiliana nayo
Presha ya kushuka (hypotension) dalili zake na njia ya kukabiliana nayo

Presha ya kushuka ama kitaalamu huitwa hypotension, presha ya kushuka ni hatari kwa afya kama ilivyo presha ya kupanda, maana mwili unakosa nguvu kabisa.

Soma Zaidi...
Dalilili za kidole  tumbo (appendicitis)
Dalilili za kidole tumbo (appendicitis)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na ugonjwa wa Kidole ambao kitaalamu hujulikana Kama Appendicitis. Kidole tumbo husababisha maumivu kwenye tumbo la chini la kulia. Hata hivyo, kwa watu wengi, maumivu huanza karibu na kitovu na kisha kusonga. Kadiri uvi

Soma Zaidi...
Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa
Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa

Soma Zaidi...
Ishara na dalilili za Kichaa Cha mbwa
Ishara na dalilili za Kichaa Cha mbwa

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kichaa cha mbwa ni virusi hatari vinavyoenezwa kwa watu kutoka kwa mate ya wanyama walioambukizwa. Virusi vya kichaa cha mbwa kawaida hupitishwa kwa kuuma.

Soma Zaidi...
Vidonda vya tumbo husababishwa na nini
Vidonda vya tumbo husababishwa na nini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu visababishi vya vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
 Matatozo katika choo kidogo, maradhi ya figo na dalili zake pia namna ya kujikinga na madhradhi ya figo
Matatozo katika choo kidogo, maradhi ya figo na dalili zake pia namna ya kujikinga na madhradhi ya figo

MATATIZO YA CHOO KIDOGO NA FIGOFigo ni kiungo muhimu sana katika uchujaji wa mkojo, na afya ya mfumo wa utoaji taka mwili.

Soma Zaidi...
Sababu zinazopelekea maumivu ya Matiti.
Sababu zinazopelekea maumivu ya Matiti.

 Maumivu ya matiti hutokea zaidi kwa watu ambao hawajamaliza hedhi, ingawa yanaweza kutokea baada ya kukoma hedhi. 

Soma Zaidi...