Dalili za mimba ya watoto mapacha

Makala hii itakwenda kukupa dalili ambazo zinaonyesha kuwa mimba ni ya mapacha. Dalili hizi zitahitajika kuthibitishwa na kipimo cha daktari ili kujuwa kuwa ni kweli.

Mapacha hutokea endapo mbegu Mwanamke atatoa mayai mawili na yote yakarutubishwa mapacha wa aina hii ni mapacha ambao hawafanani. Na pia mapacha hutokea endapo yai lililorutubishwa nikajigawa sehemu mbili na kila moja katika sehemu hizo ikakuwa kama mtoto. mapacha wa aina hii hufanana.

 

Dalili za mapacha ni kawaida na zile za mimba za kawaida. hata hivyo kunakuwa na ongezeko la ukali wa dalili hizo. Pia kuna dalili baadhi ambazo hawezi kuzipata mwenye mimba ya mtoto mmoja. Dalili za kawaida za mimba ni kama:

  1. kukosa hedhi
  2. maumivu ya tumbo
  3. kupata kichefuchefu
  4. uchovu
  5. maumivu ya tumbo na kichwa

 

Dalili ambazo ni za kawaida za mimba lakini mwenue mappacha zinaweza kuwa kali zaidi:

  1. Kujaa sana kwa maziwa
  2. maumivu makali ya maziwa
  3. uchovu mkali sana
  4. kuhisi njaa kali na kupata hamu ya kula

 

Tofauti na dalili hizo sasa nitakwenda kukuelekeza daili za mimba mapacha. Hata hivyo dalili hizi zinahitaji kuthibitishwa na kipimo ili kuwa na uhakika kama ni mimba mapacha. Dalili hizo ni kama:-

  1. Mtoto kuanza kucheza mapema sana tofauti na mimba nyingine
  2. Mtoto anapocheza unahizi anacheza kwenye maeneo tofautitofauti ya tumbo na sio sehemu moja.
  3. tumbo huwa kubwa zaidi na hukuwa kwa haraka sana.
  4. kuongezeka kwa uzito haraka haraka
  5. mapigo ya moyo ya mtoto huwa ni zaidi ya mapigo ya mtoto mmoja.

 

Changamoto za mimba mapacha

Mwanamke mwenye mimba ya mapacha anaweza kupatwa na changamoto ambazo zinaweza kuwa kali zaidi ya asiye na mpacha. Changamoto hizo ni kama:-

  1. ongezeko la shinikizo la juu la damu (presha ya kupanda) wakati wa ujauzito
  2. Yupo hatarini kupata kisukari cha mimba
  3. uchache wa majimaji ya amniotic fluid
  4. kujifunguwa watoto njiti
  5. kupasuka kwa placenter

 

Changamoto za mimba mapacha sio tu sitaishia kwa mama bali pia zinaweza kumpata mtoto ama watoto. Matatizo yanayoweza kuwapata watoto ni pamoja na:-

  1. Ubongo kuvuja damu
  2. Kuzaliwa njiti
  3. kuzaliwa na uzito kidogo
  4. kuwa na tatizo la kupata baridi
  5. mtoto kushundwa kula
  6. mtoto kupata matatizo ya kuona

 

Nini kifanyike kumlinda mama na watoto

Kutokana na changamoto ambazo mama mwenye mimba mapacha anaweza kuyapata ama matatizo ambayo yanaweza kuwapata watoto, hapa nitakupa mambo ya kufanya kukabiliana na shida hizo:-

  1. kuhudhuria clinic kila inapofika tarehe ya kwenda bila kukosa
  2. onana na daktari kila unapopata tatizo la kiafya.
  3. kula vizuri
  4. pata muda wa kuoumzika
  5. fanya mazoezi hata ya kutembea
  6. kunywa maji mengi
  7. kuwa na furaha. epuka mambo ya kukuletea misongo ya mawazo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 25223

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba

Posti hii inahusu zaidi vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba,ni vipimo vya moja kwa moja kutoka maabara na vingine sio vya maabara.

Soma Zaidi...
je mwana mke ana weza kubeba mimba kama hayupo kwenye siku zake za hatali ama

Mimba haipatikani kila siku, na pia mimba huingia kwa siku moja na katika muda mmoja. Baada ya mimba kutungwa hakuna tena nafasi ya kutungwa mimba nyingine.

Soma Zaidi...
dalili za uchungu kwa mama mjamzito

Makala hii itakwenda kukufundisha baadhi ya dalili za uchungu kwa mama mjamzito.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Nikila tumbo linauma, mdomo mchungu, matiti yanauma na hedhi sijapata, je ni dalili za mimba?

Mdomo kuwa mchungu ni halia mabayo haiashirii ishara mbaya za kiafya. Mdomo unaweza kuwa mchungu kutokana na vyakula. Pia hutokea ikawa ni ishara ya baadhi ya maradhi, ama ni matokeo ya baadhi ya shda za kiafya. Je vipi kuhusu maumivu ya matiti na tumb?

Soma Zaidi...
Kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi, tunajua kabisa wakati wa hedhi damu inapaswa kuwa nyepesi na ya kawaida ila kuna wakati mwingine inakuwa na mabonge zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi.

Soma Zaidi...
Kaka nasumbuliwa saan na tatizo la kuwasha kwenye kichwa Cha uume Sijui nifanyaje

Je kichwa cha uume wako kinawasha, na je kinatoa majimaji kwenye njia ya mkojo, una muda ganinavtatizo hili. Na je ulishiriki ngono zembe siku za hivi karibuni?

Soma Zaidi...
Dalili za ujauzito: Nini kinatokea kwanza

Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia.

Soma Zaidi...
Mimba kutoka kabla ya umri wake

Posti hii inahusu zaidi kuhusu kwa mimba kutoka kabla ya mda wake,ni kitendo ambacho mimba utoka kabla ya wiki ishilini na na nane.

Soma Zaidi...