picha

Dalili za mimba ya watoto mapacha

Makala hii itakwenda kukupa dalili ambazo zinaonyesha kuwa mimba ni ya mapacha. Dalili hizi zitahitajika kuthibitishwa na kipimo cha daktari ili kujuwa kuwa ni kweli.

Mapacha hutokea endapo mbegu Mwanamke atatoa mayai mawili na yote yakarutubishwa mapacha wa aina hii ni mapacha ambao hawafanani. Na pia mapacha hutokea endapo yai lililorutubishwa nikajigawa sehemu mbili na kila moja katika sehemu hizo ikakuwa kama mtoto. mapacha wa aina hii hufanana.

 

Dalili za mapacha ni kawaida na zile za mimba za kawaida. hata hivyo kunakuwa na ongezeko la ukali wa dalili hizo. Pia kuna dalili baadhi ambazo hawezi kuzipata mwenye mimba ya mtoto mmoja. Dalili za kawaida za mimba ni kama:

  1. kukosa hedhi
  2. maumivu ya tumbo
  3. kupata kichefuchefu
  4. uchovu
  5. maumivu ya tumbo na kichwa

 

Dalili ambazo ni za kawaida za mimba lakini mwenue mappacha zinaweza kuwa kali zaidi:

  1. Kujaa sana kwa maziwa
  2. maumivu makali ya maziwa
  3. uchovu mkali sana
  4. kuhisi njaa kali na kupata hamu ya kula

 

Tofauti na dalili hizo sasa nitakwenda kukuelekeza daili za mimba mapacha. Hata hivyo dalili hizi zinahitaji kuthibitishwa na kipimo ili kuwa na uhakika kama ni mimba mapacha. Dalili hizo ni kama:-

  1. Mtoto kuanza kucheza mapema sana tofauti na mimba nyingine
  2. Mtoto anapocheza unahizi anacheza kwenye maeneo tofautitofauti ya tumbo na sio sehemu moja.
  3. tumbo huwa kubwa zaidi na hukuwa kwa haraka sana.
  4. kuongezeka kwa uzito haraka haraka
  5. mapigo ya moyo ya mtoto huwa ni zaidi ya mapigo ya mtoto mmoja.

 

Changamoto za mimba mapacha

Mwanamke mwenye mimba ya mapacha anaweza kupatwa na changamoto ambazo zinaweza kuwa kali zaidi ya asiye na mpacha. Changamoto hizo ni kama:-

  1. ongezeko la shinikizo la juu la damu (presha ya kupanda) wakati wa ujauzito
  2. Yupo hatarini kupata kisukari cha mimba
  3. uchache wa majimaji ya amniotic fluid
  4. kujifunguwa watoto njiti
  5. kupasuka kwa placenter

 

Changamoto za mimba mapacha sio tu sitaishia kwa mama bali pia zinaweza kumpata mtoto ama watoto. Matatizo yanayoweza kuwapata watoto ni pamoja na:-

  1. Ubongo kuvuja damu
  2. Kuzaliwa njiti
  3. kuzaliwa na uzito kidogo
  4. kuwa na tatizo la kupata baridi
  5. mtoto kushundwa kula
  6. mtoto kupata matatizo ya kuona

 

Nini kifanyike kumlinda mama na watoto

Kutokana na changamoto ambazo mama mwenye mimba mapacha anaweza kuyapata ama matatizo ambayo yanaweza kuwapata watoto, hapa nitakupa mambo ya kufanya kukabiliana na shida hizo:-

  1. kuhudhuria clinic kila inapofika tarehe ya kwenda bila kukosa
  2. onana na daktari kila unapopata tatizo la kiafya.
  3. kula vizuri
  4. pata muda wa kuoumzika
  5. fanya mazoezi hata ya kutembea
  6. kunywa maji mengi
  7. kuwa na furaha. epuka mambo ya kukuletea misongo ya mawazo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023/03/28/Tuesday - 02:38:36 pm Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 31558

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 web hosting    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Njia za kupunguza tatizo la kutanuka kwa tezi dume.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo tunaweza kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili la kutanuka kwa tezi dume, kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili kwenye jamii kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Sababu za mwanamke kukosa hamu ya tendo la ndoa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mwanamke kukosa tendo la ndoa, ni sababu ambazo uwakuta wanawake wengi unakuta mama yuko kwenye ndoa ila hana hata hamu ya lile tendo la ndoa hali ambayo umfanya mwanamke kuona kitendo cha tendo la ndoa ni unyanyasaji au

Soma Zaidi...
Hatua Saba za kutibu au kuepuka uvimbe kwenye kizazi

Posti hii inahusu zaidi hatua ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kutibu uvimbe au kwa kitaalamu huitwa fibroids. Hizi hatua zikitumika uweza kusaidia kupunguza kiwango cha kupata au kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...
Namna ya kumtunza mtoto aliyezaliwa

Post hii inahusu zaidi namna ya kumtunza mtoto mchanga aliyezaliwa, ni njia zitoleeazo na wakunga Ili kumtunza mtoto mchanga aliyezaliwa.

Soma Zaidi...
Magonjwa madogo madogo kwa Mama wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi magonjwa madogo madogo kwa akina Mama wajawazito, ni magonjwa ambayo hayawezi kupelekea kupoteza maisha kwa Mama mjamzito, magonjwa haya upotea ikiwa Mama atajifungua.

Soma Zaidi...
Sifa za siku za kupata mimba

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya sifa za siku za kupata mimba

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa hedhi.

Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Damu, majimaji na uteute unaotoka kwenye uke wa Mjamzito, sababu zake na dalili zake

Unataka kujuwa sababu za mjamzito kutokwa na damu, utelezi ama majimaji kwenye uke wake. Na dalili gani zinaashiriwa na majimaji haya

Soma Zaidi...
Umuhimu wa maji yaliyomo kwenye mfuko wa mtoto akiwa tumboni mwa mama

Post hii inahusu zaidi umuhimu wa maji yaliyomo kwenye mfuko wa mtoto akiwa tumboni. Ni maji ambayo kwa kitaalamu huitwa (Amniotic fluid)

Soma Zaidi...