picha

Sababu za kutoona hedhi kwa wakati

Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.

Sababu za kukosa hedhi kwa mda ambao msichana anapaswa kuingia kwenye siku zake tayari.

1.Hili ni tatizo ambalo uwakumba wasichana wachache sana kwenye jamii, kwa wasichana huanza kuona hedhi kuanzia kwenye miaka kumi na miwili na kuendelea na kuna wengine ambao hawaoni na hali hii uwafanya kujisikia vibaya na kwa hiyo tunapaswa kujua sababu hizo kama ifuatavyo.

 

2. Kuwepo kwa Kiriba tumbo au kwa kitaalamu huitwa obesity hali hiyo ni kwa sababu ya kuwepo kwa mafuta mengi kila mahali ambayo yanasababisha vitu vingine kwenye mwili kwenda vibaya na kusababisha yai kushindwa kutoka kwenye kasha lake na hatimaye msichana hawezi kupata hedhi, kwa hiyo wazazi mnapaswa kuchagua aina nzuri ya vyakula vya kuwapa watoto wenu ili kuepuka matatizo kama haya.

 

3.Kuwepo kwa Mazoezi makali.

Mazoezi makali yakiwepo yanaweza kusababisha sehemu za via vya uzazi kutofanya kazi zake za kawaida au mazoezi hayo yanasababisha baadhi ya sehemu kuaribika na hatimaye Msichana anashindwa kupata hedhi kwa hiyo wale wanaofanya mazoezi makali jaribuni kutapunguza ili kuepuka matatizo haya,

 

4.Kuwepo kwa kiwango kidogo cha mafuta mwilini,

Kitendo cha kuwepo kwa mafuta kidogo mwilini nacho usababisha msichana kukosa hedhi kwa sababu mafuta ni mojawapo ya kitu kinachohitajika wakati wa ukuaji wa mtoto.kwa hiyo mafuta yakiwa chini ya asilimia kumi na tano mpaka kumi na saba msichana hawezi kupata hedhi maana ni kidogo mno.

 

5. Kutozalishwa au kuwepo kwa matatizo ya homoni ambazo usaidia kwenye makuzi ya mtoto, kwa hiyo kama homoni hazipo kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi au pengine kwa sababu amezaliwa hivyo ni vigumu sana kupata hedhi, kwa hiyo wazazi wanapaswa kuwalea watoto wao kwenye misingi kizuri ili waweze kuepukakana na Magonjwa na wanapaswa kula vyakula muhimu sio vyakula ambavyo usababisha kuwepo kwa matatizo kwenye maisha yake

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2556

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Dr nahis kuchanganyikiwa nimetoka niliingia hedhi tar 18 mwezi wa9 lakini saivi Jana tena nmeingia dr hii imekaaje mimi?

Kamaumeshawahi kujiuliza kuhusu kutokwaba damu tofautivna siku za hedhi, base mwaka hii ni kwaajiki yako.

Soma Zaidi...
Faida na hasara za kutumia kondomu kama njia ya uzazi wa mpango

Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia mimba zisiharibike.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuzuia mimba zisiharibike, kwa sababu kila mama anayebeba mimba anategemea kupata mtoto kwa hiyo na sisi hamu yetu ni kuhakikisha kwamba mtoto anazaliwa kwa kuzuia mimba kuharibik

Soma Zaidi...
Sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kwa mtoto mara tu anapozaliwa

Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.

Soma Zaidi...
Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Soma Zaidi...