Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.
Sababu za kukosa hedhi kwa mda ambao msichana anapaswa kuingia kwenye siku zake tayari.
1.Hili ni tatizo ambalo uwakumba wasichana wachache sana kwenye jamii, kwa wasichana huanza kuona hedhi kuanzia kwenye miaka kumi na miwili na kuendelea na kuna wengine ambao hawaoni na hali hii uwafanya kujisikia vibaya na kwa hiyo tunapaswa kujua sababu hizo kama ifuatavyo.
2. Kuwepo kwa Kiriba tumbo au kwa kitaalamu huitwa obesity hali hiyo ni kwa sababu ya kuwepo kwa mafuta mengi kila mahali ambayo yanasababisha vitu vingine kwenye mwili kwenda vibaya na kusababisha yai kushindwa kutoka kwenye kasha lake na hatimaye msichana hawezi kupata hedhi, kwa hiyo wazazi mnapaswa kuchagua aina nzuri ya vyakula vya kuwapa watoto wenu ili kuepuka matatizo kama haya.
3.Kuwepo kwa Mazoezi makali.
Mazoezi makali yakiwepo yanaweza kusababisha sehemu za via vya uzazi kutofanya kazi zake za kawaida au mazoezi hayo yanasababisha baadhi ya sehemu kuaribika na hatimaye Msichana anashindwa kupata hedhi kwa hiyo wale wanaofanya mazoezi makali jaribuni kutapunguza ili kuepuka matatizo haya,
4.Kuwepo kwa kiwango kidogo cha mafuta mwilini,
Kitendo cha kuwepo kwa mafuta kidogo mwilini nacho usababisha msichana kukosa hedhi kwa sababu mafuta ni mojawapo ya kitu kinachohitajika wakati wa ukuaji wa mtoto.kwa hiyo mafuta yakiwa chini ya asilimia kumi na tano mpaka kumi na saba msichana hawezi kupata hedhi maana ni kidogo mno.
5. Kutozalishwa au kuwepo kwa matatizo ya homoni ambazo usaidia kwenye makuzi ya mtoto, kwa hiyo kama homoni hazipo kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi au pengine kwa sababu amezaliwa hivyo ni vigumu sana kupata hedhi, kwa hiyo wazazi wanapaswa kuwalea watoto wao kwenye misingi kizuri ili waweze kuepukakana na Magonjwa na wanapaswa kula vyakula muhimu sio vyakula ambavyo usababisha kuwepo kwa matatizo kwenye maisha yake
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu zaidi dalili za PID maana yake ni maambukizi kwenye pelvic kwa kitaalamu huitwa pelvic infection disease, ni ugonjwa unaoshambulia sana wanawake na wasichana
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni hii ya cortisol,hii ni homoni ambayo utokana na tezi glang(adrenal gland) kufanya kazi kupitiliza hali ambayo mara nyingi husababishwa na msongo wa mawazo wa mda mrefu, yaani wale watu ambao mda mwingi huwa wenye
Soma Zaidi...Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?
Soma Zaidi...Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoabkunaweza kuashiria kuwa kuna majeraha yametokea huwenda ni michubuko ilitokea ndio ikavujisha damu. Lakini kwa nini hali kama hii itokee. Posti hii itakwwnda mujibu swali hili.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa sababu zinazoweza kupelekea uke kuwa mkavu yaani kukosa majimaji wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Watu wengi wanadhania kuwa kufanya tendo la ndoa katika siku hatari ni lazima kuwa utapata ujauzito. Hili sio sahihi kabisa. Post hii itakwenda kuangalia jambo hili zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii zaidi kazi ya Dawa ya metronidazole katika kutibu Minyoo, ni aina ya Dawa ambayo imetumiwa na watu wengi wakaweza kupona na kuepukana na minyoo. Zifuatazo ni baadhi ya kazi za metronidazole.
Soma Zaidi...Swali langu ni hili doktaJe siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?
Soma Zaidi...