Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike

Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume.

Kila mwanamke mwenye mina ana hamu ya mujuwa jinsia ya mtoto wake. Huwenda ili aweze kujiandaa kununua mavazi mapema, ama kupata pongezi kutoka kwa mwenzi wake ambaye amemuahidi kuzipata endapo atakuwa na mtoto wa jinsia fulani. Dalili za mimba iwe ya mtoto wa kike ama wa kiume ni zilezile isipokuwa kuna mambo flani yanaongezeka.  Katika post hii nitakueleza dalili ambazo watu wengi wanaamini kuwa zinaonyesha jinsia ya mtoto. Hata hivyo pia nitakueleza usahihi wa maoni yao kitaalamu.

 

Dalili za kawaida za ujauzito wa mtoto bila kujali jinsia:

  1. Kutoka na matone ya damu iliyo nyepesi
  2. Kukosa hedhi
  3. Maumivu ya kichwa bila ya sababu
  4. Mwili kuongezeka joto
  5. Mapigo ya moyo kuongezeka
  6. Kupata kizungzungu
  7. Kupatwa na kichefuchefu
  8. Kuchoka bila ya kufanya kazi
  9. Maumivu ya tumbo

 

Sasa wacha tuje kwenye swali letu la awali kuhusu dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama wa kike. katika kuelezea kkila dalili nitakwenda kukuambia uhakika wa dalili hizo. Jambo la kuzingatia ni kuwa dalili pekee hazithibitishi bila ya kupata vipimo kwa kitaalamu. kwani misingi ya dalili hizo imewekwa kutokana na imani za watu vile wanavyodhani ama mazoea yao ama historia ya yale yaliowakuta.

 

Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama wa kike:

  1. Uzito wa tumbo; Inaaminika kuwa endapo mjamzito atahisi tumbo ni zito sana basi mtoto ni wa kiume. lakini endapo tumbo siuo zito sana basi mtoto ni wa kike. Wanaamini kuwa mtoto wa kiume ni mzito kuliko wa kike. Hata hivyo nadharia hii haina uithibitisho wa kitaalamu ijapokuwa watu wanaamini hivyo.

 

  1. Kichefuchefu: Wanadai wamama kuwa endapo mjamzito atakuwa na kichefuchefu sana basi mtot ni wa kiume. na endapo hatapata kabisa ama itakuwa ni cha kawaida basi mtoto ni wa kike.

 

  1. Mabadiliko kwenye ngozi: Dhana hii ni kuwa endapo mwanamke atapata mabadiliko kwenye ngozi yake, mabadiliko ambayo yatakwenda kuharibu muonekano wa ngozi na uzuri wake basi mimba hiyo ni ya mtoto wa kike. Pia wnaamini kuwa mtoto wa kike anachukuwa urembo wa mama yake. Miongoni mwa mabbadiliko hayo ni chunusi, ngozi kupauka na kukosa mvuto. Kwa uoande mwiungine mtoto wa kiume hawezi kumfanya majamzito abadilikwe na ngazi yake. pia nadharia hii haina ushahidi wa kitaalamu kutoka kwa madaktari.

 

  1. Mabadiliko ya nywele waumini wa dhana hii wanasema kuwa mtoto wa kiume hana shida na uzuri wa mama yake. Kwa kuwa nywele ni moja ya uzuri wa mama basi zitabaki kama zilivyo. kwanamke hatakuwa na mabadiliko ya nywele akiwa na mimba ya mtoto wa kiume. Kwa upande mwingine mimba ya mtoto wa kike itamfanya nywele kunyonyoka ama kukatika. Imani hii pia haina ushahidi wa kisayansi.

 

  1. Kuchaguwa sukari na chumvi: Inaaminika kuwa mwanamke mwenye mimba ya mtoto wa kike anapenda sana vitu vitamu. lakini ikiwa mimba ni ya mtoto wa kiume anapendelea sana vitu vyenye chumvi chumvi. hata hivyo hakuna ushahidi wa kitaalamu kuthibitisha nadharia hii.

 

  1. Utofauti wa kwenye mapigo ya moyo: Wanaamini kuwa endapo mimba ni ya mtoto wa kike mapigo ya moyo huwa mengi zaidi. kwa mfano yakiwa ni zaidi ya 140 ndani ya dakika basi mimba ni ya mtoto wa kike. na yakiwa chini ya 140 mtoto ni wa kiume. nadharia hii inaonekana ni ya kitaalamu zaidi, hata hivyo haina ushahidi wa kuthibitisha.

 

Je nitajuwaje kwa uhakika kuwa mtoto ni wa kiume ama wa kike?

Sasa wacha tuangaie kitaalamu zaidi kwa namna gani utaweza kujuwa jinsia ya mtoto. Ukweli ni kwamba utaweza kuwa na uhakika wa jinsia ya mtoto kwa kutumia vipimo. Hivyo hapa nitakueleza baadhi ya vipimo ambavyo vinatumika kujuwa jinsia ya mtoto.

  1. Kwa kutumia kipimo cha damu cha DNA kwa mfano kipimo cha panorama kinachojulikana kama Noninvasive prenatal testing (NIPT). Kipimo hiki kinaweza kuonyesha jinsia ya mtoto kuanzia wiki ya 7 hadi ya 10 toka ujauzito kutungwa.

 

  1. Kwa kutumia kipimo cha utrasound: Kipimo cha utrasound hutumika kumulika ndani ya tumbo la mjaozito na kumuona mtoto na jinsia yake. kipimo hilki kinaweza kuona jinsia ya mtoto kuanzia ujauzito wa wiki ya 18 hadi 20.

 

Mwisho nimalizie kusema kuwa bila ya kutumia vipimo vya kitaalamu hatuwezi kuwa na uhakika juu y jinsia ya mtoto. Hivyo kwa mwenye kutaka kujuwa jinsia ya mtoto afanye vipimo vya kitaalamu. kwa mfano kipimo cha utrasound sio cha ghali kukifanya ukilinganisha vipimo vinginevyo.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 50487

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Je mwanamke anaweza pata mimba ikiwa wakati watendo la ndoa hakukojoa Wala kusikia raha yoyote ya sex wakati watendo landoa

Je wewe ni mwanmake unayepata shida kufika kileleni? (Kukojoa wakati wa tendo lwa ndoa). Post hii itakujibu baadhi ya maswali yako.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuz

Soma Zaidi...
Sababu za kupasuka kwa mfuko wa kizazi

Posti hii inahusu zaidi sababu za kupasuka kwa mfuko wa uzazi hasa mama anapokalibia kujifungua.

Soma Zaidi...
Mm tumbo linaniuma mara kwa mara na linakua kama linages alaf kichwa kinauma mara kwa mara na nakosa choo wakati mwingine na kiuno kinauma je?inawezakua n ujauzito? Maana nilshirki tendo la ndoa siku ya tano baada ya kutoka hedhi

Dalili za mwanzo za ujauzito zinaweza kuwa ni changamoto kwamwanamke hasa ikiwa ndio mimba yake ya kwanza. Maumivu ya tumbo, kujaa kwa tumbo gesi, kukosa choo ama hamu ya kula na kadhalika huweza pia kuambatana na ujauzito.

Soma Zaidi...
Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?

Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?

Soma Zaidi...
Ijue kazi ya homoni ya HCG wakati wa kupima mimba.

Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya HCG katika kupima mimba, HCG maana yake ni human chorionic gonadotropin ni homoni ambayo uonekanekana kwenye mkojo na damu kama mtu ana mimba.

Soma Zaidi...
Vyakula hatari kwa mjamzito mwenye mimba na mimba changa

Vyakula hivi hapasi kuvila mwanamke mwenye ujauzito kwa kiasi kikubwa, hasa yule mwenye mimba chaga

Soma Zaidi...
Namna ya kutibu kuharisha kwa mtoto ukiwa nyumbani.

Post hii inahusu zaidi njia za kutibu kuharisha kwa watoto wakiwa nyumbani, kwa sababu mara nyingine mtoto anaweza kuharisha si kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ila ni uchafu tu kwa hiyo njia muhimu zinazofaa kutibu mtoto ni pamoja na yafuatayo.

Soma Zaidi...
Habari nilitaka kujua kuhusu ugonjwa wa fungusi kwenye uume

Je na wewe unasumbuliwa na fangasi wenye uume. Post hii ni kwa ajili yako.

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia kama mtoto aliyezaliwa anapumua

Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.

Soma Zaidi...