Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike

Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume.

Kila mwanamke mwenye mina ana hamu ya mujuwa jinsia ya mtoto wake. Huwenda ili aweze kujiandaa kununua mavazi mapema, ama kupata pongezi kutoka kwa mwenzi wake ambaye amemuahidi kuzipata endapo atakuwa na mtoto wa jinsia fulani. Dalili za mimba iwe ya mtoto wa kike ama wa kiume ni zilezile isipokuwa kuna mambo flani yanaongezeka.  Katika post hii nitakueleza dalili ambazo watu wengi wanaamini kuwa zinaonyesha jinsia ya mtoto. Hata hivyo pia nitakueleza usahihi wa maoni yao kitaalamu.

 

Dalili za kawaida za ujauzito wa mtoto bila kujali jinsia:

  1. Kutoka na matone ya damu iliyo nyepesi
  2. Kukosa hedhi
  3. Maumivu ya kichwa bila ya sababu
  4. Mwili kuongezeka joto
  5. Mapigo ya moyo kuongezeka
  6. Kupata kizungzungu
  7. Kupatwa na kichefuchefu
  8. Kuchoka bila ya kufanya kazi
  9. Maumivu ya tumbo

 

Sasa wacha tuje kwenye swali letu la awali kuhusu dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama wa kike. katika kuelezea kkila dalili nitakwenda kukuambia uhakika wa dalili hizo. Jambo la kuzingatia ni kuwa dalili pekee hazithibitishi bila ya kupata vipimo kwa kitaalamu. kwani misingi ya dalili hizo imewekwa kutokana na imani za watu vile wanavyodhani ama mazoea yao ama historia ya yale yaliowakuta.

 

Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama wa kike:

  1. Uzito wa tumbo; Inaaminika kuwa endapo mjamzito atahisi tumbo ni zito sana basi mtoto ni wa kiume. lakini endapo tumbo siuo zito sana basi mtoto ni wa kike. Wanaamini kuwa mtoto wa kiume ni mzito kuliko wa kike. Hata hivyo nadharia hii haina uithibitisho wa kitaalamu ijapokuwa watu wanaamini hivyo.

 

  1. Kichefuchefu: Wanadai wamama kuwa endapo mjamzito atakuwa na kichefuchefu sana basi mtot ni wa kiume. na endapo hatapata kabisa ama itakuwa ni cha kawaida basi mtoto ni wa kike.

 

  1. Mabadiliko kwenye ngozi: Dhana hii ni kuwa endapo mwanamke atapata mabadiliko kwenye ngozi yake, mabadiliko ambayo yatakwenda kuharibu muonekano wa ngozi na uzuri wake basi mimba hiyo ni ya mtoto wa kike. Pia wnaamini kuwa mtoto wa kike anachukuwa urembo wa mama yake. Miongoni mwa mabbadiliko hayo ni chunusi, ngozi kupauka na kukosa mvuto. Kwa uoande mwiungine mtoto wa kiume hawezi kumfanya majamzito abadilikwe na ngazi yake. pia nadharia hii haina ushahidi wa kitaalamu kutoka kwa madaktari.

 

  1. Mabadiliko ya nywele waumini wa dhana hii wanasema kuwa mtoto wa kiume hana shida na uzuri wa mama yake. Kwa kuwa nywele ni moja ya uzuri wa mama basi zitabaki kama zilivyo. kwanamke hatakuwa na mabadiliko ya nywele akiwa na mimba ya mtoto wa kiume. Kwa upande mwingine mimba ya mtoto wa kike itamfanya nywele kunyonyoka ama kukatika. Imani hii pia haina ushahidi wa kisayansi.

 

  1. Kuchaguwa sukari na chumvi: Inaaminika kuwa mwanamke mwenye mimba ya mtoto wa kike anapenda sana vitu vitamu. lakini ikiwa mimba ni ya mtoto wa kiume anapendelea sana vitu vyenye chumvi chumvi. hata hivyo hakuna ushahidi wa kitaalamu kuthibitisha nadharia hii.

 

  1. Utofauti wa kwenye mapigo ya moyo: Wanaamini kuwa endapo mimba ni ya mtoto wa kike mapigo ya moyo huwa mengi zaidi. kwa mfano yakiwa ni zaidi ya 140 ndani ya dakika basi mimba ni ya mtoto wa kike. na yakiwa chini ya 140 mtoto ni wa kiume. nadharia hii inaonekana ni ya kitaalamu zaidi, hata hivyo haina ushahidi wa kuthibitisha.

 

Je nitajuwaje kwa uhakika kuwa mtoto ni wa kiume ama wa kike?

Sasa wacha tuangaie kitaalamu zaidi kwa namna gani utaweza kujuwa jinsia ya mtoto. Ukweli ni kwamba utaweza kuwa na uhakika wa jinsia ya mtoto kwa kutumia vipimo. Hivyo hapa nitakueleza baadhi ya vipimo ambavyo vinatumika kujuwa jinsia ya mtoto.

  1. Kwa kutumia kipimo cha damu cha DNA kwa mfano kipimo cha panorama kinachojulikana kama Noninvasive prenatal testing (NIPT). Kipimo hiki kinaweza kuonyesha jinsia ya mtoto kuanzia wiki ya 7 hadi ya 10 toka ujauzito kutungwa.

 

  1. Kwa kutumia kipimo cha utrasound: Kipimo cha utrasound hutumika kumulika ndani ya tumbo la mjaozito na kumuona mtoto na jinsia yake. kipimo hilki kinaweza kuona jinsia ya mtoto kuanzia ujauzito wa wiki ya 18 hadi 20.

 

Mwisho nimalizie kusema kuwa bila ya kutumia vipimo vya kitaalamu hatuwezi kuwa na uhakika juu y jinsia ya mtoto. Hivyo kwa mwenye kutaka kujuwa jinsia ya mtoto afanye vipimo vya kitaalamu. kwa mfano kipimo cha utrasound sio cha ghali kukifanya ukilinganisha vipimo vinginevyo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 62879

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Je, wajua sababu zinazopelekea maumivu ya Matiti kwa wanawake?

Maumivu ya matiti ni malalamiko ya kawaida miongoni mwa wanawake yanaweza kujumuisha uchungu wa matiti, maumivu makali ya kuungua au kubana kwenye tishu zako za matiti. Maumivu yanaweza kuwa ya mara kwa mara au yanaweza kutokea mara kwa mara tu. Maumiv

Soma Zaidi...
Huduma kwa mama mwenye kifafa cha mimba.

Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wajawazito wanaweza kuzipata wakiwa na Dalli au tayari wana kifafa cha mimba.

Soma Zaidi...
Sorry kunamchumba wangu katokwa na majimaji meupe na tumbo linamuuma BAADA mda likaacha nidalili za Nini au.nikawaida tu

Majimaji msule sehemu za siriyanaweza kuashiria mambo mengi ka mwanamke. Ikiwemo ujauzitina maradhi. Pia yanaweza kuashiria kuwa mwanamke unaweza kuoatavujauzito amalaa.

Soma Zaidi...
Ni ipi hasa siku ambayo nitafute ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kutafuta ujauzito

Soma Zaidi...
Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua

Posti hii inahusu zaidi mda ambao mama anapaswa kukaa bila kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kujifungua.

Soma Zaidi...
Mambo yanayodhihirisha afya ya nguvu za kiume

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali yanayodhoofisha afya za wanaume, kwa wakati mwingine wanaume ukosa kujiamini kwa sababu ya mambo ambayo yanaadhiri afya za wanaume.

Soma Zaidi...
siku za hatari

Hizi ni siku za hatari kupata ujauzito.Siku hizi ndio siku za kupata mimba kwa urahisi

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku ya 7 Hadi ya 14

Soma Zaidi...
Dawa ya chango na dawa maumivu ya tumbo la hedhi

Nitakujiza dawa ya chango na maumivu ya tumbo lahedhi, dalili zake na njia za kukabiliana na maumivu ya tumbo la chango.

Soma Zaidi...