Mimba iliyotunga nje
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya
MIMBA ILIYOTUNGIA NJE:
Mimba ya namna hii kitaalamu hufahamika kama ectopic pregnancy. Je hii ni mimba gani? Hii ni mimba ambayo yai lililorutubishwa linaendelea kukuwa nje ya mji wa mimba (uterus). mimba inaweza kukuwa sehemu yeyote kwenye tumbo ila nje ya mji wa mimba. Kwa asilimia kama 90% mimba hukuwa kwenye mirija ya falopia. Hii ni mimba hatari sana na inahitaji uangalizi wa haraka sana, kwani inaweza kuhatarisha maisha ya mama. Inakadiriwa kuwa mimba za namna hii huchukuwa kati ya asilimia 1 mpaka 2 ya miba zote.
Kwa nini mimba hii ni hatari?1.Mimba inatkuwa nje ya mji wa mimba hivyo haiwezekani mtoto kupona2.Inaweza kusababisha kupasuka kwa mirija ama sehemu ilipokuwa.3.Inaweza kusababisha ulemavu kwa mama endapo itachelewa kuonekana4.Kwa asilimia 30 mimba hii haina dalili hii ni hatari zaidi.5.Inaweza kusababisha uvujaji wa damu kwa kiasi ikubwa6.Inaweza kusababisha mwanamke kuhitajiwa kufanyiwa upasuaji kamma tiba.
Sababu za kutokea mimba hiiKama nilivyotangulia kukueleza kuwa asilimia 30 ya mimba hizi hazina dalili. Lakini kwa kiasi kikubwa mimba hizi huwa na dalili. Tafiti zinaonyesha kuwa dalili zake hutokea kabla ya wiki ya 10. Sasa hapa nitakutajia baadhi tu ya dalili za mimba hii:-1.Maumivu ya tumbo upande mmoja wa nyonga.2.Maumivu ya mabega3.Kutokwa na damu kwenye uke.4.Maumivu ya nyonga.5.Mvurugiko wa tumbo na kutapika6.Maumivu ya upande mmoja wa mwili.7.Kizunguzungu na uchovu8.Maumivu ya mabega, shingo na mkundu.
Sababu za kutokea kwa mimba hii.1.Kuwa na maambukizi kwenye via vya uzazi yaani PID2.Uvutaji wa sigara3.Kama una umri wa miaka 35 na kuendelea4.Kama unatumia madawa ya kuivisha mayai5.Kama ulishapata ujauzito huu hapo mwanzo upo uwezekano kuja kupata tena6.Kama ulifanyiwa upasuaji kwenye mirija ya falopia7.Kama una tatizo la endometriosis8.Baadhi ya njia za kuthibiti uzazi mfano, IUD
Nini tena yapasa kujuwa?1.Ujauzito uliotungia njea haurithiwi yaani kama mama aliwahikupata ujauzito huu hali hii hairithiwi.2.Kutoka kwa ujauzito sio sababu ya kupata mimba hii3.Kutoa ujauzito pia hakuna mahusianao na ujauzito huu4.Mazoezi na michezo pia hihusiani na kutokea kwa ujauzito huu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 ai web app 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Vipimo muhimu wakati wa ujauzito
Post hii inahusu zaidi vipimo muhimu wakati wa ujauzito ni vipimo ambavyo vinapaswa kupimwa na Mama ili kuangalia mambo mbalimbali katika damu au sehemu yoyote, pia vipimo hivi umsaidia sana Mama kujua afya yake.
Soma Zaidi...Maumivu ya Uke na Uume baada ya tendo la ndoa na wakati wa tendo la ndoa
Utajifunza sababu za maumivu ya uume na uke wakati wa tendo la ndoa na baada ya tendo la ndoa na matibabu yake.
Soma Zaidi...Mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula.
Soma Zaidi...Uzazi wa mpango
Uzazi wa Mpango hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa. Uzazi wa mpango una faida kadhaa kwa mama wa mtoto, wanandoa na jamii Ujuzi wa mzunguko wa hedhi humwezesha mtoa huduma kumshaur
Soma Zaidi...Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.
Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h
Soma Zaidi...Maandalizi ya mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia.
Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.
Soma Zaidi...