Mimba iliyotunga nje
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya
MIMBA ILIYOTUNGIA NJE:
Mimba ya namna hii kitaalamu hufahamika kama ectopic pregnancy. Je hii ni mimba gani? Hii ni mimba ambayo yai lililorutubishwa linaendelea kukuwa nje ya mji wa mimba (uterus). mimba inaweza kukuwa sehemu yeyote kwenye tumbo ila nje ya mji wa mimba. Kwa asilimia kama 90% mimba hukuwa kwenye mirija ya falopia. Hii ni mimba hatari sana na inahitaji uangalizi wa haraka sana, kwani inaweza kuhatarisha maisha ya mama. Inakadiriwa kuwa mimba za namna hii huchukuwa kati ya asilimia 1 mpaka 2 ya miba zote.
Kwa nini mimba hii ni hatari?1.Mimba inatkuwa nje ya mji wa mimba hivyo haiwezekani mtoto kupona2.Inaweza kusababisha kupasuka kwa mirija ama sehemu ilipokuwa.3.Inaweza kusababisha ulemavu kwa mama endapo itachelewa kuonekana4.Kwa asilimia 30 mimba hii haina dalili hii ni hatari zaidi.5.Inaweza kusababisha uvujaji wa damu kwa kiasi ikubwa6.Inaweza kusababisha mwanamke kuhitajiwa kufanyiwa upasuaji kamma tiba.
Sababu za kutokea mimba hiiKama nilivyotangulia kukueleza kuwa asilimia 30 ya mimba hizi hazina dalili. Lakini kwa kiasi kikubwa mimba hizi huwa na dalili. Tafiti zinaonyesha kuwa dalili zake hutokea kabla ya wiki ya 10. Sasa hapa nitakutajia baadhi tu ya dalili za mimba hii:-1.Maumivu ya tumbo upande mmoja wa nyonga.2.Maumivu ya mabega3.Kutokwa na damu kwenye uke.4.Maumivu ya nyonga.5.Mvurugiko wa tumbo na kutapika6.Maumivu ya upande mmoja wa mwili.7.Kizunguzungu na uchovu8.Maumivu ya mabega, shingo na mkundu.
Sababu za kutokea kwa mimba hii.1.Kuwa na maambukizi kwenye via vya uzazi yaani PID2.Uvutaji wa sigara3.Kama una umri wa miaka 35 na kuendelea4.Kama unatumia madawa ya kuivisha mayai5.Kama ulishapata ujauzito huu hapo mwanzo upo uwezekano kuja kupata tena6.Kama ulifanyiwa upasuaji kwenye mirija ya falopia7.Kama una tatizo la endometriosis8.Baadhi ya njia za kuthibiti uzazi mfano, IUD
Nini tena yapasa kujuwa?1.Ujauzito uliotungia njea haurithiwi yaani kama mama aliwahikupata ujauzito huu hali hii hairithiwi.2.Kutoka kwa ujauzito sio sababu ya kupata mimba hii3.Kutoa ujauzito pia hakuna mahusianao na ujauzito huu4.Mazoezi na michezo pia hihusiani na kutokea kwa ujauzito huu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 web hosting 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Kupima ujauzito kwa kutumia chumvi, sukari na sabuni
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupima mimba kwa kutumia chumvi sukari na sabuni
Soma Zaidi...Dalili za uvimbe kwenye kizazi
Posti hii inahusu zaidi Dalili za uvimbe kwenye kizazi,hizi ni Dalili ambazo ujitokeza kwa akina mama ambao wana uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo endapo mama ameona Dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali mara moja kwa uangalizi zaidi.
Soma Zaidi...Sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto mchanga kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, ni tatizo ambalo utokea kwa baadhi ya wajawazito kupata mtoto mwenye Uzito mkubwa, wengine uona kama ni sifa ila Kuna madhara yanaweza kujitokeza kwa Mama hasa wakati wa kujif
Soma Zaidi...Madhara ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya matumizi ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana ambao hawajafikilia mpango wa kuanza kujifungua watoto.
Soma Zaidi...Kwanini nikimaliza kufanya mapenzi na mume wangu anawashwa sana!!!!!
Habari DoktaNikuulize kituu?
Soma Zaidi...Dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku ya 7 Hadi ya 14
Soma Zaidi...