Mimba iliyotunga nje


image


Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya


MIMBA ILIYOTUNGIA NJE:

Mimba ya namna hii kitaalamu hufahamika kama ectopic pregnancy. Je hii ni mimba gani? Hii ni mimba ambayo yai lililorutubishwa linaendelea kukuwa nje ya mji wa mimba (uterus). mimba inaweza kukuwa sehemu yeyote kwenye tumbo ila nje ya mji wa mimba. Kwa asilimia kama 90% mimba hukuwa kwenye mirija ya falopia. Hii ni mimba hatari sana na inahitaji uangalizi wa haraka sana, kwani inaweza kuhatarisha maisha ya mama. Inakadiriwa kuwa mimba za namna hii huchukuwa kati ya asilimia 1 mpaka 2 ya miba zote.

 

Kwa nini mimba hii ni hatari?1.Mimba inatkuwa nje ya mji wa mimba hivyo haiwezekani mtoto kupona2.Inaweza kusababisha kupasuka kwa mirija ama sehemu ilipokuwa.3.Inaweza kusababisha ulemavu kwa mama endapo itachelewa kuonekana4.Kwa asilimia 30 mimba hii haina dalili hii ni hatari zaidi.5.Inaweza kusababisha uvujaji wa damu kwa kiasi ikubwa6.Inaweza kusababisha mwanamke kuhitajiwa kufanyiwa upasuaji kamma tiba.

 

Sababu za kutokea mimba hiiKama nilivyotangulia kukueleza kuwa asilimia 30 ya mimba hizi hazina dalili. Lakini kwa kiasi kikubwa mimba hizi huwa na dalili. Tafiti zinaonyesha kuwa dalili zake hutokea kabla ya wiki ya 10. Sasa hapa nitakutajia baadhi tu ya dalili za mimba hii:-1.Maumivu ya tumbo upande mmoja wa nyonga.2.Maumivu ya mabega3.Kutokwa na damu kwenye uke.4.Maumivu ya nyonga.5.Mvurugiko wa tumbo na kutapika6.Maumivu ya upande mmoja wa mwili.7.Kizunguzungu na uchovu8.Maumivu ya mabega, shingo na mkundu.

 

Sababu za kutokea kwa mimba hii.1.Kuwa na maambukizi kwenye via vya uzazi yaani PID2.Uvutaji wa sigara3.Kama una umri wa miaka 35 na kuendelea4.Kama unatumia madawa ya kuivisha mayai5.Kama ulishapata ujauzito huu hapo mwanzo upo uwezekano kuja kupata tena6.Kama ulifanyiwa upasuaji kwenye mirija ya falopia7.Kama una tatizo la endometriosis8.Baadhi ya njia za kuthibiti uzazi mfano, IUD

 

Nini tena yapasa kujuwa?1.Ujauzito uliotungia njea haurithiwi yaani kama mama aliwahikupata ujauzito huu hali hii hairithiwi.2.Kutoka kwa ujauzito sio sababu ya kupata mimba hii3.Kutoa ujauzito pia hakuna mahusianao na ujauzito huu4.Mazoezi na michezo pia hihusiani na kutokea kwa ujauzito huu.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Namna ya kuangalia kama mtoto aliyezaliwa anapumua
Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu. Soma Zaidi...

image Siku za kupata mimba
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata mimba Soma Zaidi...

image Mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito, tunajua wazi kuwa wajawazito pindi ujauzito ukiingia tu, kila kitu kwenye mwili ubadilika vile vile na mzunguko wa damu ubadilika. Soma Zaidi...

image Kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren. Soma Zaidi...

image Fahamu Mambo ya hatari yanayosababisha kuzaliwa kabla ya wakati (premature)
Kuzaliwa kabla ya wakati humpa mtoto muda mdogo wa kukua tumboni. Watoto waliozaliwa kabla ya wakati, hasa wale waliozaliwa mapema, mara nyingi huwa na matatizo magumu ya matibabu. Soma Zaidi...

image Dalili za Ujauzito mchanga Siku Saba Baada ya Ovulation
Unaweza kujiuliza ikiwa inawezekana kupata dalili za ujauzito mchanga kama siku 7 baada ya kudondoshwa kwa yai (DPO yaani Days Past Ovulation). Soma Zaidi...

image Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone. Soma Zaidi...

image Mimba iliyotunga nje
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya Soma Zaidi...

image Njia za kuzuia mimba zisiharibike.
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuzuia mimba zisiharibike, kwa sababu kila mama anayebeba mimba anategemea kupata mtoto kwa hiyo na sisi hamu yetu ni kuhakikisha kwamba mtoto anazaliwa kwa kuzuia mimba kuharibika kwa kufuata njia zifuatazo. Soma Zaidi...

image Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?
Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi? Soma Zaidi...