Zijuwe sababu kuu za kuwepo kwa maumivu ya tumbo baada ya kula chakula
MAUMIVU YA TUMBO BAADA YA KULA
Baada ya kula ni wakatiwa wa kupumzika, lakini sivyo kwa baadhi ya watu. Wao anapomaliza tu, anangojewa na maumivu ya tumbo. Je unajuwa sababu?, je na wewe unapatwa na maumivu ya tumbo baada ya kumaliza kula? Makala hii ni kwa ajilli yako.
Kwa ufupi maumivu haya yanaweza kusababishwa na mchafuko wa tumbo. Tunapozungumzia mchafuko wa tumbo tunazungumzia mmeng’enypo wa chakula unakuwa na hali ambayo si ya kawaida.
Dalili za mchafuko wa tumbo ni kama:-
A.Kichefuchefu
B.Kuhara
C.Kiungulia ama kucheua
D.Kujaa tumbo na kutoa hewa kwa mdomoni. Kwa kucheua
E.Maumivu ya tumbo
F.Kushiba kusikkokuwa kwa kawaida
G.Lushiba kwa haraka
H.Maumivu ya sehemu ya juu ya tumbo
I.Kuhisi kuunguwa chini ya tumbo
J.Kuhisi kuunguwa kifuani na maumivu ya kifua
K.Kutapika
Nini husababisha maumivu ya tumbo baada ya kula?
Kwa hakika kuna sababi nyingi ambazo zinaweza kupelekea maumivu ya tumbo baada ya kula. Sio hivyo tu pia tumbo linapatwa na machafuko makubwa kwa mfano kutapika, kichefuchefu, kuharisha na mengineyo. Sasa ni zipi sababi hizo zinazoletwa maumivu ya tumbo baada ya kula?
1.Aleji ya chakula.
2.kuna baadhi ya vyakula huwa vina aleji, hii hutokea pale mwili mwili unapokidhania chakula kuwa hakipo salama, na kuanza kukishambulia ili kukitoa. Hali hii hupelekea maumivu ya tumbo kama matokeo ya mpambano. Baadhi ya vyakula vyenye aleji ni kama:-
1.Maziwa
2.Maharagwe ya soya
3.Baadhi ya samaki
4.Vyakula jamii ya karanga na korosho
5.Mayai
6.Ngano
3.kama mfumo wa kumeng’enya chakula umeshindwa kukivumilia aina ya chakula ulichokula. Yaani mfumo wa chakula unashindwa kukimeng’enya kabisa ama kinameng’enywa lakini si kwa ufasaha. Kwa mfano baadhi ya vyakula vilivyotengenezwa na maziwa kwa baadhi ya watu inakuwa ni tatizo na hupelekea mvurugiko wa tumbo.
4.kama ukuta wa utumbo mdogo umeathiriwa na protini ya gluten, protini inayopatikamna kwenye nafaka kama ngano na shayiri. Hali hii hutambulika kama celiac disease.
5.Kama una tatizo la kupanda kwa tinikali za tumboni kuja juumkwenye koo sehemu inayojulikana kama esophagus. Tindikali hii inaweza kuathiri kuta za kiungo hiki na kusababisha machafuko ya tumbo. Hali hii kitaalamu hutambulika kama Gastroesophageal disease (GERD)
6.kama una matatizo kwenye utumbo mkubwa kwa kitaalamu huitwa irritable bowel syndrome. Hali hiii inaweza kuonyesha dalili kama:-
A. Maumivu ya tumbo
B.Kujaa kwa tumbo
C.Kuharisha
D.Kukosa choo
E.Kujaa gesi
7.Kuvimba kwa baadhi ya sehemu kwenye mfumo wa kumeng’enya chakula. Mgonjwa anaweza kuona dalili kama maumivu ya tumbo, kuhara, damu kwenye kinyesi n.k
8.Kama una vidonda vya tumbo. Vidond vya tumbo vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo baada ya kumaliza kula.
9.Kukosa choo. Hali hii hutokea pale chakula kinapotembea kidogokidogo katika njia ya mmeng’enyo wa chakula.
Namna ya kujikinga na maumivu ya tumbo baada ya kula.
1.Kama kuna chakula unakumbuka kilikuletea matatizo kama haya hebu kiepuke
2.Kula chakula chenye kambakmba kwa wingi na matunda
3.Kunywa maji mengi
4.Punguza unywaji wa pombe
5.Punguza matumizi ya caffein (majani ya chai kwa wingi)
6.Punguza misongo ya mawazo
Umeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kitunguu thaumu
Soma Zaidi...Makala hii inakwenda kukuletea kazi kuu za protini na vyakula vya protini katika miili yetu. Mkala hii itakusaiidia kujuwa namna ya kupangilia lishe yako kiusalama zaidi baada ya kujuwa kazi za protini katika miili yetu.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza aina 20 za vitamini. Utajifunza kazu zake mwilini, vyanzo vyake na madhara yanayoweza kutokea kutokana na upungufu wake.
Soma Zaidi...Matunda ya zamani, matunda ya asili, Zaituni tunda lipendezalo, zijuwe faida zake leo
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za mchaichai/lemongrass
Soma Zaidi...Tezi za lymph huanza kuonyesha dalili za kuwa mwili upo katika mapambano dhidi ya vijidudu vya maradhi. Ishara ni pale utakapoona tezi za lymph zina maumivu. Tezi hizi hupatikana kwenye mapaja, kwapa nashingo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za matumizi ya vyakula vya asili, kama tunavyojua kwamba mababu na mabibi zetu walitumia vyakula vya asili wakaishi miaka mingi kweli.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida ya juice ya tende,ni juice inayotumiwa na watu wengi sana na wengine wanajua kabisa faida zake na kuna wengine hawajui wanaitumia kama mazoea tu, ila kuna ambao hawajui kabisa basi zifuatazo ni faida za juice ya tende kwa wal
Soma Zaidi...