Sababu za maumivu ya tumbo baada ya kula

Zijuwe sababu kuu za kuwepo kwa maumivu ya tumbo baada ya kula chakula

Sababu za maumivu ya tumbo baada ya kula

MAUMIVU YA TUMBO BAADA YA KULA




Baada ya kula ni wakatiwa wa kupumzika, lakini sivyo kwa baadhi ya watu. Wao anapomaliza tu, anangojewa na maumivu ya tumbo. Je unajuwa sababu?, je na wewe unapatwa na maumivu ya tumbo baada ya kumaliza kula? Makala hii ni kwa ajilli yako.



Kwa ufupi maumivu haya yanaweza kusababishwa na mchafuko wa tumbo. Tunapozungumzia mchafuko wa tumbo tunazungumzia mmeng’enypo wa chakula unakuwa na hali ambayo si ya kawaida.



Dalili za mchafuko wa tumbo ni kama:-
A.Kichefuchefu
B.Kuhara
C.Kiungulia ama kucheua
D.Kujaa tumbo na kutoa hewa kwa mdomoni. Kwa kucheua
E.Maumivu ya tumbo
F.Kushiba kusikkokuwa kwa kawaida
G.Lushiba kwa haraka
H.Maumivu ya sehemu ya juu ya tumbo
I.Kuhisi kuunguwa chini ya tumbo
J.Kuhisi kuunguwa kifuani na maumivu ya kifua
K.Kutapika




Nini husababisha maumivu ya tumbo baada ya kula?
Kwa hakika kuna sababi nyingi ambazo zinaweza kupelekea maumivu ya tumbo baada ya kula. Sio hivyo tu pia tumbo linapatwa na machafuko makubwa kwa mfano kutapika, kichefuchefu, kuharisha na mengineyo. Sasa ni zipi sababi hizo zinazoletwa maumivu ya tumbo baada ya kula?



1.Aleji ya chakula.
2.kuna baadhi ya vyakula huwa vina aleji, hii hutokea pale mwili mwili unapokidhania chakula kuwa hakipo salama, na kuanza kukishambulia ili kukitoa. Hali hii hupelekea maumivu ya tumbo kama matokeo ya mpambano. Baadhi ya vyakula vyenye aleji ni kama:-
1.Maziwa
2.Maharagwe ya soya
3.Baadhi ya samaki
4.Vyakula jamii ya karanga na korosho
5.Mayai
6.Ngano



3.kama mfumo wa kumeng’enya chakula umeshindwa kukivumilia aina ya chakula ulichokula. Yaani mfumo wa chakula unashindwa kukimeng’enya kabisa ama kinameng’enywa lakini si kwa ufasaha. Kwa mfano baadhi ya vyakula vilivyotengenezwa na maziwa kwa baadhi ya watu inakuwa ni tatizo na hupelekea mvurugiko wa tumbo.



4.kama ukuta wa utumbo mdogo umeathiriwa na protini ya gluten, protini inayopatikamna kwenye nafaka kama ngano na shayiri. Hali hii hutambulika kama celiac disease.



5.Kama una tatizo la kupanda kwa tinikali za tumboni kuja juumkwenye koo sehemu inayojulikana kama esophagus. Tindikali hii inaweza kuathiri kuta za kiungo hiki na kusababisha machafuko ya tumbo. Hali hii kitaalamu hutambulika kama Gastroesophageal disease (GERD)



6.kama una matatizo kwenye utumbo mkubwa kwa kitaalamu huitwa irritable bowel syndrome. Hali hiii inaweza kuonyesha dalili kama:-
A. Maumivu ya tumbo
B.Kujaa kwa tumbo
C.Kuharisha
D.Kukosa choo
E.Kujaa gesi



7.Kuvimba kwa baadhi ya sehemu kwenye mfumo wa kumeng’enya chakula. Mgonjwa anaweza kuona dalili kama maumivu ya tumbo, kuhara, damu kwenye kinyesi n.k



8.Kama una vidonda vya tumbo. Vidond vya tumbo vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo baada ya kumaliza kula.



9.Kukosa choo. Hali hii hutokea pale chakula kinapotembea kidogokidogo katika njia ya mmeng’enyo wa chakula.



Namna ya kujikinga na maumivu ya tumbo baada ya kula.
1.Kama kuna chakula unakumbuka kilikuletea matatizo kama haya hebu kiepuke
2.Kula chakula chenye kambakmba kwa wingi na matunda
3.Kunywa maji mengi
4.Punguza unywaji wa pombe
5.Punguza matumizi ya caffein (majani ya chai kwa wingi)
6.Punguza misongo ya mawazo





                   



Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 2691

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Faida za kula Pilipili

Usiogope kuwashwa, kula pilipili ni nzuri kwa afya yako ia virutubisho vingi sana

Soma Zaidi...
UPUNGUFU WA VITAMIN NA MAJI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Faida za kula apple (tufaha)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula apple/tufaha

Soma Zaidi...
Madhara ya vyakula vya kisasa

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kuwepo kwa vyakula vya kisasa, vyakula vya kisasa ni vyakula vya madukani ambavyo vimetengenezwa na kuwekwa kwenye maduka

Soma Zaidi...
Faida za kula mayai

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kula mayai

Soma Zaidi...
Vyakula muhimu kwa kulinda afya ya macho - Epuka upofu kwa kula vyakula hivi

Matatizo ya macho yanaweza kuruthiwa kutoka kwa wazazi kwenda kwa mtoto. hata hivyo shughuli zetu na vyakula tunavyokula vinaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa matatizo haya. Hapa nitakuletea vyakula muhimu kwa afya ya macho yako.

Soma Zaidi...
RANGI ZA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula panzi, senene na kumbikumbi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula panzi senene na kumbikumbi

Soma Zaidi...
Vyakula na vinywaji hatari na vilivyo salama kwa mgonjwa wa kisukari

Hapa utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa kisukari, pia utajifunza vyakula salama anavyotakiwa ale mgonjwa wa kisukari, Pia ujajifunza njia za kujikinga na kisukari

Soma Zaidi...