image

Faida za kiafya za kula bamia/okra

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula bamia

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA BAMIA (OKRA)

 

Bamia ni katika matunda ambayo ni mboga na karibia maeneo mengi mboga hii inapatikana. Bamia ni katika mboga muhimu sana kwani ina faida nyingi sana. Ndani ya bamia kuna vitamin, madini na kambakamba. Bamia hutumiwa kuanzia majani, mbegu, bamia lenyewe , maua, kikonyo na matawi. Kwa ufupi mbamia wote ni mboga na huliwa.

 

Ndani ya bamia kuna fiber (kambakamba), folate, vitamin K na madini. Bamia husaidia katika kuboresha na kuimarisha afya ya moyo pia hulinda mwili dhini ya saratani. Jitahidi ukinunua bamia lisikae zaidi ya siku tatu ama nne. Madini ya potassium na sodium hupatikana katika bamia bila ya kusahau vitamin A ambavyo hupatikana pia kwenye bamia.

 

Ndani ya bamia kuna aina ya protin inayoitwa lectin, ambayo pia huweza kupatikana kwenye maharage na nafaka nyingine. Wataalamu wa afya walitumia lectin inayozalishwa na bamia kwa ajili ya kutibu seli za saratani ya matiti (breast cancer). matokeo ya utafiti huu ulionesha kuwa seli za saratani zilipunguwa kwa asilimia 63 na zilikufa kwa asilimia 73. tafiti nyingi zinahitajika kufanywa kuhusu swala hili.

 

Pia ndani ya bamia kuna folate. Tafiti za kisayansi zinaonesha kuwa watu ambao hawapati kula fotate za kutosha wapo hatarini zaidi ya kupata saratani ya matiti, nyia ya uzazi, ini na aina zingine za saratani. Pia baadhi ya tafiti zilizofanya mwaka 2016 zainaonesha kuwa fotate inaweza kuzuia athari za saratani ya matiti.

 

Tafiti pia zinaonesha kuwa folate ambayo hupatikana kwenye bamia husaidia katika kuzuia matatizo wakati wa ujauzito. Tafiti zinaonesha mwanamke ambaye hana folate za kutosha anakuwa hatarini kupoteza ujauzito wake au mtoto akajapata matatizo ya kiafya baadaye. Fotate ni muhimu sana kwa mwanamke wakati wa ujauzito na wakati wa kunyonyesha.

 

Mwaka 2011 tafiti za kisayansi zilikuwa zikichunguza athari ya bamia kwa wenye kisukari. Wataalamu walitengeneza poda kutokana na maganda ya bamia na mbegu zake. Kisha wakatumia katika kutibu kisukari kwa panya kama majaribio. Panya huyu alikuwa na tatizo la sukari ya kushuka. Matokeo haya yakaleta athari chanya. Hivyo inashauriwa kwa wenye kisukari kutumia sana bamia.

 

Tafiti zilizofanya na AHA (American Heart Association) zimesema kuwa kula chakula chenye kambakamba (fiber) hupunguza athari hasi za cholesterol ndani ya damu. Vyakula hivi pia hupunguza hatari ya kupata magonjwa ya moyo na stroke (kupalalaizi).

 

Tafiti zinaonesha kuwa vyakula vyenye vitamin K kwa wingi kama bania ni mujarabu sana katika kuimarisha afya ya mifupa. Vitamin hivi husaidia mifupa kufyonza madini ya calcium. Watu wenyekula vitamin K kwa wingi wana mifupa imara na isiyokuwa na mipasuko (hii ni nadharia tu).

 

Bamia husaidia katika kuzuia kupata tatizo la kukosa choo kwani kuna kambakamba ndani ya bamia, hizi husaidia katika mmeng’enyo wa chakula na kusafiri kwa chakula kutoka tumboni kuelekea maeneo mengine kwenye almentary canal. Bamia hupunguza hamu ya kula, hivyo husaidia katika kupunguza uzito.

 

Pia itambulike kuwa zipo athari hasi za kula bamia kwa kupitiliza. Kwa mfano bamia hupunguza hamu ya kula, pia bamia huweza kupelekea kujaa gesi tumboni na kujaza tumbo. Kula bamia nyingi zaidi huweza kupelekea kupata vijiwe ndani ya figo kwani bamia zina madini ya calcium kwa wing





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1935


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Faida za kiafya za kula maboga
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula maboga Soma Zaidi...

Kitunguu saumu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kitunguu saumu Soma Zaidi...

Uyoga (mushrooms)
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula uyoga Soma Zaidi...

Madhara ya upungufu wa protini mwilini
Madhara ya upungufu wa protini ni mengi kiafya. Miongoni mwa madhara hayo ni.. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Fenesi
Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamini D na faida zake
Soma Zaidi...

Kazi za protini mwilini ni zipi?
Virutubisho vya protini vina kazi nyingi mwilini. Zifuatazo ndio kazi protini mwilini Soma Zaidi...

Faida za kula Ndizi
Kuna faida kubwa za kiafya kwa kula ndizi, soma makala hii mpaka mwisho Soma Zaidi...

Nini maana ya protini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya protini Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Fyulisi
Soma Zaidi...

Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume.
Tatizo la nguvu za kiume linawwza kuzuiliwa ama kupunguzwa kwa kutumia muunganimo wa njiankadhaa kama kubaduki vyakula, kutumia dawa, kupata ushauri kwa wataalamu wa afya ya mahusiano ama kufanya nazoezi. Je na wewe unasumbuliwa na tatizo hili? Makala hii Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Tikiti
Soma Zaidi...