image

Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia, sababu zake na dalili zzake

Hapa utajifunza sababu za kupatwa na maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia

Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia, sababu zake na dalili zzake

MAUMIVU YA TUMBO KWA CHINI UPANDE WA KULIA




Sehemu ya tumbo kwa chini upande wa kulia ndipo ambapo baadhi ya viungo kupatikana kama utumbo mkubwa, appendix, na kwa baadhi ya wanawake ni ovari hupatikana maeneo haya.katika hali za kawaid maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia huwa yanaondoka yenyewe ndni ya siku mbili ama tatu. Ila kwa baadhi ya nyakati kama yanahusiana na shida za afya zaidi matibabu ni lazima yafanyike.



Maumivu haya yatahidaji uangalizi wa karibu wa daktari endapo yatafungamana na dalili zifuatazo:
1.Maumivu na mkandamizo kwenye kifua
2.Homa
3.Damu kwenye kinyesi
4.Kuendelea kwa kichefuchefu na kutapika kwa masiku kadhaa.
5.Ngozi kuwa na rangi ya njano
6.Kukaza kwa tumbo sana unapoligusa
7.Kujaa kwa tumbo




Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia
1.Ugonjwa wa Appendix:
Appendix ni sehemu ndigo ambapo utumbo mkubwa hukutana na utumbo mdogo. Sasa sehemu hii hutokea kuathiriwa hivyo hujaa na kuvimba ugonjwa huu unaitwa appendicitis. Hii ni katika sababu kuu za maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia. Tofauti na maumivu haya ugonjwa wa appendix hufungama na na dalili zifuatazo:-
1.Kichefuchefu
2.Kutapika
3.Homa
4.Kuharisha
5.Kukosa hamu ya kula
6.Kujaa kwa tumbo
7.Kukosa hamu ya kula.



2.Kujaa gesi tumboni. Kikawaida ndani ya tumbo kuna gesi, ambayo husababishwa na vuakula tunavyokula. Sasa kila chakula mbacho hakijameng’enywa kinapoongezeka tumboni, yaani unapokula gesi zaidi hujitengeneza tumboni. Wakati gesi inapoongezeka inapelekea kujaa kwa tumbo na maumivu ya tumbo.



Pia mgonjwa atahisi kucheua gesi kwa sauti kutoka mdomoni, pia kujamba mara kwa mara ili kupunguza gesi.endapo tatizo hili litakuwa ni kubwa na endelevu linaweza kuashiria shida nyingine kama kisukari



Sababu nyingine za gesi tumboni:-
1.Kumeza gesi
2.Kula zaidi kupitiliza
3.Kutafuna bigjii
4.Kuvuta sigara




3.kukosa choo
Kukosa choo huleta maumivu baada ya kula ama kunywa kitu. Maumivu haya kikawaida yanatokea sehemu ya juu ya tumbo lakini unayahiisi sehemu ya chini kwa upande wa kulia.



Dalilo za kukosa choo:-
Tofauti na maumivu haya ya tumbo lakini yanaambatana na dalili zifuatazo:-
A.Kiungulia
B.Kujaa tumbo
C.Kushiba mapema
D.Kujuhisi mgonjwa
E.Kucheua gesi mdomoni
F.Kujamba
G.Kucheua chakula ama majimaji machungu




4.Kuwa na henia hutokea pale shehemu ya ya ndani ya tumbo inaponasa kwenye misuli nsani ya tumbo na kupelekea maumivu. Dalili za henia ni pamoja na:-
A.Kuvumba kwa sehemu husika
B.Kuongezeka kwa maumivu
C.Mamivu wakati unaponyanyua kitu, unapocheka, unapolia ama unapokohoa
D.Kuhisi tumbo kushiba, ama kukosa choo.



5.Kuwa na vijijiwe kwenye figo.
Hutokea pale vijichpe vijidogo vigumu vilivyotengenezwa kwa chumvi vikijikusanya kwenye figo. Hali hii ikitokea huleta maumivu mgongoni, chini ya mbavu na chini ya tumbo upande wa kulia.



Dalili nyingine za vijiwe vya kwenye figo
A.Maumivu wakati wa kukojoa
B.Mkojo wenye rangi ya kahawia, nyekundu ama damu ya mzee
C.Mkojo wenye mawinguwingu na unatoa harufu kali
D.Kichefuchefu
E.Kutapika
F.Kuhisi kukojoa mara kwa mara
G.Homa na baridi.



Sababu zinazoathiri wanwake tu
1.Tumbo la hedhi
Maumivu haya yanaweza kutokea kabla na baada ya kubata hedhi. Yanaweza kutokea pande zote yaani kulia na kushoto kwa chini. Maumiv haya yana dalili kama:
A.Maumivu endelevu
B.Maumivu ya chini mgongoni na mapajani
C.Kichefuchefu
D.Kupata kinyesi kilaini
E.Maimivu ya kichwa
F.Kizunguzungu



2.Kuota kwa tishu za tumbo la uzazi mje ya tumbo la uzazi. Kitaalamu hufahamika kama endometriosis. Hali hii inapelekea maumivu ya tumbo kkwa chini, pia huandamana na yafuatayo:
A.Maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada
B.Maumivu unapokojoa
C.Maumivu makali ya umbo la hedhi
D.Hedhi yenye damu nyingi
E.Kutokwa na matone ya damu



3.Matatizo katika ovari au ovarian cyst. Mara nyingi maumivu yanayosabavishw ana atizo hili huondaka yenyewe. Yanaweza kuonyesha dalili kama kujaa kwa tumbo, kuhisi kujaa sana. Kuhisi kushiba sana, maumivu makali ya tumbo kwa chini. Muone daktari kama maumivu yatakuwa na:-
A.Makali sana kupiitiliza
B.Homa
C.Kutapika
D.Baridi kwenye ngozi
E.Kuhema mbiombio
F.Uchovu



4.Ujauzito uliotungia nje (ectopic pregnancy). mgonjwa ataona dalili kama kutokwa na damu ukeni, maumivu mwisho wa mabega na mwanzoni mwa mikono, maumivu wakti wa kukojoa.



5.Ugonjwa wa PID
Dalili za PID
A.Homa
B.Kutokwa na uchafu ukeni
C.Maumivu makali ya chango
D.Kuhisi kama kuunguwa wakati wa kukojoa
E.Kutokwa na damu wakati wa hedhi





                   







           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 8626


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Aina 20 za Vitamini, kazi zake, vyanzo vyeke na madhara ya upungufu wake
Katika post hii utakwenda kujifunza aina 20 za vitamini. Utajifunza kazu zake mwilini, vyanzo vyake na madhara yanayoweza kutokea kutokana na upungufu wake. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Maini
Soma Zaidi...

matunda
Soma Zaidi...

Faida za kula embe
Somo hili linakwenda kukuletea faida za embe na umuhimu wake kiafya Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula kungumanga
Soma Zaidi...

Vyakula vya madini kwa wingi, na kazi za madini mwilini
Utajifunza vyakula vyenye madini kwa wingi, kazi za madini mwilini na athari za upungufu wake Soma Zaidi...

Vyakula muhimu kwa kulinda afya ya macho - Epuka upofu kwa kula vyakula hivi
Matatizo ya macho yanaweza kuruthiwa kutoka kwa wazazi kwenda kwa mtoto. hata hivyo shughuli zetu na vyakula tunavyokula vinaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa matatizo haya. Hapa nitakuletea vyakula muhimu kwa afya ya macho yako. Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamin D
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya vitamin D Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Tango
Soma Zaidi...

MATUNDA YENYE VITAMINI C KWA WINGI
Matunda yenye vitamni C kwa wingi ni machungwa, maembe, ndimu na limao, endelea kusoma Soma Zaidi...

Ulaji wa protini unasaidia kupunguza unene
Soma Zaidi...

ijuwe namna ya kufanya ihram na Vazi la ihram
Soma Zaidi...