image

Dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14

DALIILI YA MIMBA KATIKA WIKI YA KWANZA NA PILI (SIKU 7 MPAKA 14)1.Kuendelea kwa joto la mwili. Kama ulikuwa makini na siku ambayo joto la mwili wako lilikuwa kubwa, kama ulishiriki tendo siku moja ama mbili kabla ama siku ile, basi endapo joto la mwili litakuwa endelevu hii huashiria huwenda ulibeba ujauzito. Kwa nini, ni kwa sababu joto la mwili hutokea baada ya mabadiliko ndani ya mwili hususani homoni mpya huzaliwa kwa ajili ya kuandaa ukuaji wa ujauzito. Mabadiliko haya ya joto yasifananishwe na joto la homa.

 

2.Katika wiki hii ya kwanza unaweza kuona mabadiliko ya majimaji kwenye uke. Majimaji yaliyokuwa siku za nyuma kidongo yanaweza kuanza kuchukuwa sura ya mfanano wa majimaji meupe ya yai lililovunjwa. Halikadhalika matarajio ni kuwa uke unatakiwa urudi katika hali ya ukavu baada ya kupita siku hatari. Lakini kama ujauzito ulitungwa uke hautarudi katika hali yake ya kawaida ya ukavu hivyo huanza kuzalisha majimaji kwa wingi. Mabadiliko haya si rahisi kuyaona ila endapo utakuwa manini zaidi unaweza kugundua.

 

3.Kutokwa na damu kidogo (implantation bleeding). damu hii inaweza kutokea mwishoni mwa wiki ya kwanza ama katikati ya wiki ya pili. Damu hii ni kidogo na inaweza kuwa ni matone kadhaa. Haifanani na damu ya hedhi na wala haitoki na maumivu. Damu hii si endelevu inaweza kutoka kwa muda mchache na kukata. Mwanamke anaweza kuona nguo yake ya ndani inamadoa ya damu. Kwa damu hii mwanamke hatahitai kuvaa pedi.

 

4.Maumivu ya kichwa ama kichwa kuwa chepesi. Hali hii inaweza kuandamana na kizunguzungu. Hali hii si lazima kuipata, hata hivyo wanawake wengine wanaipata ila hawafikirii kuwa ni tatizo kwani hutokea na kuondoka bila ya kuathiri mwili kwa muda mrefu. Hapa anaweza kuona ni hali ya kawaida kama hatatilia maanani mabadiliko haya.

 

Kumbuka dalili hizo tajwa hapo juu ni ngumu kuziona mpaka uwe makini sana kwani zinaweza kuathiriwa na hali nyingine za kiafya. Kwa mfano joto la mwili linaweza kusababishwa na mambo mengi kama maradhi, uchovu na stress. Majimaji ya ukeni yanaweza kuongezeka kwa sababu ya njia za uzazi wa mpango ama mabadiliko ya homoni.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2639


Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Fahamu ugonjwa wa kifafa cha mimba.
Post hii inahusu zaidi Ugonjwa wa kifafa cha mimba ambapo kwa kitaalamu huitwa eclampsia, utokea pale ambapo Mama anapokuwa na degedege wakati wa mimba na baada ya kujiunga. Soma Zaidi...

Zijuwe hatuwa za ukuwaji wa ujauzito na dalili za ujauzito katika miezi mitatu, miezi sita na miezi tisa
Soma Zaidi...

Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia Soma Zaidi...

Je ?kipimo kikionyesha misitar miwili mmoja hafifu mwingine umekolea ni mimba au sio
Kipimo chamimba cha mkojo, huonyesha nestory miwili kuwa una mimba, na mmoja kuwa huna mimba. Sasa je ukitokea mmoja umekoleana mwingine hafifu? Endelea na pasti Òœï¸ hadi mwisho Soma Zaidi...

Changamoto za ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu changamoto za ujauzito na dalili zake endelevu Soma Zaidi...

MAJIMAJI YA KWENYE UKE YANATUELEZA NINI?
Soma Zaidi...

Haya maji meupe hutokea wakat mimba ishatungwa au ukifanya tendo la ndoa lazima utokee?
Majimaji yanayitoka kwenye uke yanafungamana na taarifa nyingi kuhusu afya vya mwanamke. Ujauzito, maradhi, mabadiliko ya homoni na zaidi. Soma Zaidi...

Hatua Saba za kutibu au kuepuka uvimbe kwenye kizazi
Posti hii inahusu zaidi hatua ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kutibu uvimbe au kwa kitaalamu huitwa fibroids. Hizi hatua zikitumika uweza kusaidia kupunguza kiwango cha kupata au kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi. Soma Zaidi...

Dalili za Ujauzito mchanga Siku Saba Baada ya Ovulation
Unaweza kujiuliza ikiwa inawezekana kupata dalili za ujauzito mchanga kama siku 7 baada ya kudondoshwa kwa yai (DPO yaani Days Past Ovulation). Soma Zaidi...

Njia za kuondoa fangasi sehemu za siri
Makala hii itakujuza baadhi ya njia utakaoweza kuzifuata ili kukabiliana na fangasi sehemu za siri kwa wanaume Soma Zaidi...

Madhara ya mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtoto alizaliwa na uzito mkubwa. Soma Zaidi...

Dalili za maumivu ya hedhi
Maumivu ya hedhi (dysmenorrhea) ni maumivu makali au ya kubana sehemu ya chini ya tumbo. Wanawake wengi hupatwa na Maumivu ya hedhi kabla tu na wakati wa hedhi zao. Kwa wanawake wengine, usumbufu huo ni wa kuudhi tu. Kwa wengine,  Soma Zaidi...