Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali.
1. Kuwepo kwa lishe mbaya.
Kuna wakati mwingine akina Mama wakibeba mimba uanza kula mambo ya ajabu ambayo ni pamoja na kula udongo, mkaa,pemba na vitu kama hivyo na kuanza kuacha kutumia vyakula vya maana ambavyo vinaleta afya kwenye miili yao , kama vile folic acid na vyakula vyenye madini.
2. Kuwepo kwa matatizo kwenye tezi.
Kuna wakati mwingine kitendo cha kuwepo kwa tezi bila kitibiwa usababisha mimba kutoka hasa kwenye kipindi cha miezi minne mpaka sita.
3. Pia kama Kuna maambukizi kwenye njia ya uzazi.
Kwa sababu magonjwa mengine mama uyapata akiwa tayari ana mimba na pia kwa kuwa akina Mama wengi upima siku za mwanzo kwa hiyo usababisha mimba kutoka.
4. Pengine msongo wa mawazo.
Kuna kipindi kunakuwepo na msongo wa mawazo kwa akina Mama wakiwa na mimba na kusababisha mpaka mimba kutoka, msongo wa mawazo inawezekana ni kwa sababu Mama hapati matumizi ya kutosha au mme wake anamsumbua na mambo kama hayo.
5. Uzito mkubwa kupita kiasi.
Nii vizuri kupunguza Uzito wakati wa ujauzito Ili kuepuka tatizo la mimba kuharibika.
6. Kuwepo kwa maambukizi kwenye mlango wa kizazi.
Na hili ni tatizo kwa Sababu usababisha kuenea kwenye sehemu mbalimbali kwa mtoto na sehemu aliyojishikiza na kusababisha mimba kutoka.
7. Kulegea kwa mfuko wa mimba.
Kuna kipindi kwa sababu mbalimbali utokea ambapo usababisha mfuko wa uzazi kulegea na kusababisha mimba kutoka.
8. Shinikizo la damu kuwa juu.
Kwa hiyo akina Mama kila udhulio wanapaswa kupima kiwango cha shinikizo la damu Ili kuepuka mimba kutoka.
9. Matumizi ya dawa pasipo daktari.
Na hilo ni tatizo ambapo madawa mengine unakuta hayaruhusiwi kutumiwa na akina Mama wakati wa ujauzito ila wao wanatumia tu.
10. Matumizi ya chakula chenye Sumu.
Kuna wakati mwingine akina Mama wanaweza kutumia vyakula vyenye Sumu na kusababisha mimba kutoka.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za kujifungua hatua kwa hatua
Soma Zaidi...Posti hii inahusu namna unavyoweza kumtambua mtoto mwenye Ugonjwa wa Nimonia na tiba anayopaswa kupata mtoto mwenye Nimonia
Soma Zaidi...Idadi ya siku hatari za kupata mimba hutofautiana kutoka kwa mwanamke mmoja namwinhine. Kinda ambao idadivyavsikuvzao za hatari ni nyingi kuliko wengine.
Soma Zaidi...Abali mkuu Nina mdogo wangu anawashwa Sana sehemu ya Siri mpaka anatoka vipele vingi kwenye mapaja korodani zake zimebadilika kuwa nyekundu na zenye kutisha uume wake nao umekuwa unakama mabaka umebabuka aisee nime angaika Sana kumtibia mpaka nakata tamaa
Soma Zaidi...dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...