Sababu za mimba ya miezi 4-6 kutoka.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali.
Sababu ya mimba kuanzia miezi 4_6 kutoka.
1. Kuwepo kwa lishe mbaya.
Kuna wakati mwingine akina Mama wakibeba mimba uanza kula mambo ya ajabu ambayo ni pamoja na kula udongo, mkaa,pemba na vitu kama hivyo na kuanza kuacha kutumia vyakula vya maana ambavyo vinaleta afya kwenye miili yao , kama vile folic acid na vyakula vyenye madini.
2. Kuwepo kwa matatizo kwenye tezi.
Kuna wakati mwingine kitendo cha kuwepo kwa tezi bila kitibiwa usababisha mimba kutoka hasa kwenye kipindi cha miezi minne mpaka sita.
3. Pia kama Kuna maambukizi kwenye njia ya uzazi.
Kwa sababu magonjwa mengine mama uyapata akiwa tayari ana mimba na pia kwa kuwa akina Mama wengi upima siku za mwanzo kwa hiyo usababisha mimba kutoka.
4. Pengine msongo wa mawazo.
Kuna kipindi kunakuwepo na msongo wa mawazo kwa akina Mama wakiwa na mimba na kusababisha mpaka mimba kutoka, msongo wa mawazo inawezekana ni kwa sababu Mama hapati matumizi ya kutosha au mme wake anamsumbua na mambo kama hayo.
5. Uzito mkubwa kupita kiasi.
Nii vizuri kupunguza Uzito wakati wa ujauzito Ili kuepuka tatizo la mimba kuharibika.
6. Kuwepo kwa maambukizi kwenye mlango wa kizazi.
Na hili ni tatizo kwa Sababu usababisha kuenea kwenye sehemu mbalimbali kwa mtoto na sehemu aliyojishikiza na kusababisha mimba kutoka.
7. Kulegea kwa mfuko wa mimba.
Kuna kipindi kwa sababu mbalimbali utokea ambapo usababisha mfuko wa uzazi kulegea na kusababisha mimba kutoka.
8. Shinikizo la damu kuwa juu.
Kwa hiyo akina Mama kila udhulio wanapaswa kupima kiwango cha shinikizo la damu Ili kuepuka mimba kutoka.
9. Matumizi ya dawa pasipo daktari.
Na hilo ni tatizo ambapo madawa mengine unakuta hayaruhusiwi kutumiwa na akina Mama wakati wa ujauzito ila wao wanatumia tu.
10. Matumizi ya chakula chenye Sumu.
Kuna wakati mwingine akina Mama wanaweza kutumia vyakula vyenye Sumu na kusababisha mimba kutoka.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Habar doctor mm nahc kuwa ni mjamzito tumbo la chin ya kitovu linaniuma muda mwingine linaacha chuchu zinawasha na cku niliyokutana na mume wangu ni cku 11
Kuna uwezekano una ujauzito ila hujajijuwa, huwenda hujapata dalili zozote. Unataka kujuwa kama una ujauzito baada ya tendo la ndoa.
Soma Zaidi...mpenzi wangu nimeshiriki nae tendo la ndoa akiwa siku zake za hatar kwa siku 3 lakin hajashika mimba tatizo linaweza kuwa ni nini?
Kupata ujauzito hufungamana na mambo mengi ikiwepo afya vya wawili yaani me na mume na mengineyo. Unaweza kushiriki sikuvhatari na usiupate mimba. Postivhii ibakwendavkukufahamisha undani wa jambo hili.
Soma Zaidi...Uvimbe kwenye kizazi (Fibroids): Dalili, ukubwa na tiba yake.
Uvimbe kwenye kizazi, unaojulikana kitaalamu kama Uterine Fibroids au Leiomyomas, ni hali ya kawaida ambapo uvimbe usio wa kansa hukua kwenye misuli ya mji wa mimba. Hali hii huwapata wanawake wengi katika umri wa kuzaa. Ingawa uvimbe huu mara nyingi si hatari, unaweza kusababisha usumbufu mkubwa na changamoto za uzazi. Makala hii inaangazia sifa za uvimbe huu, jinsi ya kuutambua, na mbinu za matibabu
Soma Zaidi...Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID
Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.
Soma Zaidi...Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba
Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...