picha

Sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa

Posti hii inahusu zaidi sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa, Mgonjwa akiwa anaumwa na pia anakula chakula ni lazima asafishwe kinywa Ili kuweza kuepuka madhara mengine yanayoweza kujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kinywani.

Sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa.

1.Tunamsafisha Mgonjwa kinywa ili tuweze kusafisha mdomo na meno kwa sababu kuna baadhi ya masalia ubaki mdomoni pindi tunapimlisha mgonjwa na pia kufanya meno ya mgonjwa juwa safi.

 

2. Tunamsafisha mgonjwa kinywa ili kuweza kuzuia kuaribika kwa meno na pia kuzuia maambukizi zaidi ya meno kwa sababu kuna vyakula vingine vinakuwa na sukari kwa hiyo vikikaa kwa mda bila kusafishwa Mgonjwa anaweza kupata Maambukizi kutokana na uchafu au meno kuoza.

 

3. Kuongeza mzunguko wa damu kwenye sehemu za kinywa, kama kuna uchafu ni vigumu damu kuzunguka kwa urahisi ila kama hakuna uchafu damu inaweza kusafili kwa urahisi kwenye kinywa cha mgonjwa.

 

4. Pia tunamsafisha Mgonjwa kinywa ili aweze kuwa huru na kuzuia harufu mbaya kwenye mdomo kwa hiyo kinywa likiwa kisafi na hamu ya kula ya mgonjwa uongezeka na pia katika kumfanyia mgonjwa usafi kinywani tunaweza kuondoa mabaki kinywani mwa mgonjwa.

 

5.Kwa hiyo tunapaswa kuwahudumia wagonjwa wetu vizuri na kuwaweka kwenye hali ya usafi kwa sababu na wenyewe wana hamu ya kuwa safi kwa hiyo tukiwa na wagonjwa nyumbani tuwahudumie na kwa kufanya hivyo tunaweza kuepusha hatari mbalimbali.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1180

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 ai web app     ๐Ÿ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game     ๐Ÿ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii     ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Dalili za fizi kuvuja damu

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa fizi ambapo fizi huweza kuwa na maumivu, kuambukizwa, kuvuja damu kwenye fizi na Vidonda.

Soma Zaidi...
Zijue kazi za chanjo ya DTP au DPT (Donda Koo,Pepopunda, na kifaduro))

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya DTP au DPT ambayo Inazuia magonjwa ya Donda Koo, Pepopunda na kifaduro.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENGโ€™ATWA NA NYUKI

Kungโ€™atwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujikinga na U.T.I inayijirudia rudia.

Endapo U.T.I inajirudiarudia baada yavkutibiwa inawezabkuwa ikakupa mawazo mengi. Katika post hii nitakufafanulia nini ufanye.

Soma Zaidi...
Njia za kufuata unapohudumia watu waliopata ajali

Post hii inahusu zaidi namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa watu waliopata ajali. Ajali ni tukio lisilotarajiwa ambalo kinaweza kumkuta mtu yeyote, tunapotoa huduma ya kwanza tnazingatia rangi ambazo huwakilisha jinsi watu walivyoumia.

Soma Zaidi...
Ijue rangi ya mkojo isiyo ya kawaida

Post hii inahusu zaidi rangi isiyo ya kawaida kwenye mkojo, kawaida mkojo huwa na rangi ya kahawia Ila ukiona rangi zifuatazo Kuna shida kwenye mkojo.

Soma Zaidi...