Ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha
Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha hii ni chanjo wanayopewa watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa lengo la kuzuia kuharisha chanjo hiyo kwa kitaalamu huitwa Rotarix.
Ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha.
1.Aina hii ya chanjo inazuia kuharisha kwa watoto na utolewa mara mbili na kwa vipindi tofauti tofauti pia uweza kutunzwa kwenye temperature kuanzia mbili mpaka nane na ikizidi au kupungua itaweza kuleta madhara na kwa ujumla isitumike, chanjo hiyo utolewa kwenye kinywa kwa miilis Moja nukta tano, na chanjo hii baada ya kutolewa uwa na madhara madogo madogo kama ifuatavyo.
2.Watoto wanaweza kukosa hamu ya kula,kuharisha na kutapika,joto la mwili kupanda na homa, maumivu ya tumbo na kuhisi uchovu wa mara kwa mara hasa kusinzia kwa mtoto na chanjo hii hapaswi kupewa mtoto mwenye mzio au aleji kwa hiyo hizo Dalili zikitokea na kuchukua mda zaidi ya masaa ishirini na manne mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini ili kupata matibabu zaidi, ratiba ya chanjo ni kama ifuatavyo.
3.Chanjo ya kwanza unapaswa kutolewa kwenye wiki ya sita ambayo ni sawa na mwezi mmoja na wiki mbili, na kiasi ni sawa na mills moja nukta tano na pia utolewa kwa njia ya kinywa kwa hiyo ifikapo kila baada ya wiki sita walezi na wazazi wanapaswa kuwapeleka watoto kupata chanjo.
4.Chanjo ya pili inapaswa kutolewa baada ya wiki kumi ambazo ni sawa na miezi miwili na wiki mbili kwa hiyo ifikapo mda huu mama na walezi wanapaswa kutimiza wajibu wao wa kuwapeleka watoto wao kupata chanjo na kiasi ni kile kile cha kwenye chanjo ya kwanza na daima upitishwa kwenye kinywa.
5. Kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto kupata chanjo hii kwa sababu ina maana sana kwenye maisha ya watoto mbali tunajua wazi kuharisha kwa watoto ni hatari na upelekea maji kuisha mwilini na hatimaye mtoto anaweza kupata madhara makubwa zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 ai web app 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 web hosting 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Njia za kukabiliana na minyoo
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na minyoo
Soma Zaidi...Utaratibu wa lishe kwa vijana
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa vijana
Soma Zaidi...Vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda, ni vifaa muhimu ambavyo mara nyingi kutwa hospitalini.
Soma Zaidi...Zijue hasara za magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi hasara za magonjwa ya ngono, ni magonjwa yanayoambukizwa kwa kujamiiana bila kutumia kinga.
Soma Zaidi...Mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu, kama mtu amepoteza fahamu Kuna mambo muhimu yanapaswa kuangaliwa kwa makini kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Namna ya kumsaidia mtoto mwenye degedege
Degedege ni ugonjwa unaoshambulia sana watoto chini ya miaka mitano,na uwaletea matatizo mengi pamoja na kuwepo kwa ulemavu na vifo vingi vinavyosababishwa na ugonjwa huu.
Soma Zaidi...