Karanga (groundnuts)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula karanga

. Karanga (ground nuts)

Karanga ni katika vyakula vya asili na ni kiungio cha mboga kwa jamii nyingi sana Tanzania na dunia kwa ujumla. Kama vilivyo vyakula vingine karanga ni katika vyakula vyenye virutubisho vingi. Ndani ya karanga kuna fotale, vitamin E, madini ya copper na arginine. Pia karanga ni chanzo kizuri cha omega-3 fatty acid, vitamin E na ijulikane kuwa fatty acid ni muhimu sana kwa afya ya moyo.

 

Ndani ya kjaranga kuna antioxidant iitwayo phenolic, polyphenol na resveratrol hizi husaidia katika kulinda mwili dhidi ya stress yaani misongo ya mawazo, na husaidia pia katika kulinda mwili dhidi ya maradhi ya saratani. Pia husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini yaani mfumo wa kupambamba na maradhi na mashambulizi ya magonjwa.

 

Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa aina ya mafuta (fat) yaliyomo kwenye karanga ni mafuta ambayo ni salama kwa afya ya moyo. Kitaalamu aina ya fat iliyomo kwenye karanga ni monosaturated fat na polyunsaturated fat kwa ufupi fat hizi ni salama kwa afya ya moyo na mfumo mzima wa usukiumwaji wa damu. Kwani fat hizi husaidia katika kupunguza cholesterol kwenye damu hivyo hupunguza hatari ya kupata maradhi ya moyo.

 

Karanga pia ni chanzo kizuri cha protini. Itambulike kuwa protini ni katika virutubisho muhimu na vinavyotakiwa kwa kiwango kikubwa ndani ya miili yetu. Seli za mwili zinahitaji protini kuweza kukuwa na kutengenezwa upya. Ukuaji wa mwili na uponaji wa vidonda na majeraha unahitaji protini.. watoto wanatakiwa wapewe vyakula vya protini kwa kiasi kikubwa zaidi ili kuwezesha maendeleo ya ukuaji wao.

 

Tofauti na protini mwili unahitaji madini kwa kiwango kinachohitajika. Katika karanga kuna aina mbalimbali za madini kama vile magnesium, phosphorus, potassium, zinc, calcium na sodium. Madini yote haya husaidia katika ukuaji wa mwili na mwili kufanya kazi vyema.

 

Mafuta ya karanga yana fatty acid ambayo hutambulika kuwa inaongeza lipoprotein ndani ya mwili inayojulikana kama “good cholesterol” yaani cholesterol iloyo safi. Hii ni muhimu katika kuimarisha afya ya moyo na ubongo. Pia madini ya copper yaliyomo kwenye karanga husaidia katika kuzuia maradhi ya moyo yaani “coronary heart diseases”. pia vitamin B1 (thiamine) ni virutubisho muhimu katika kulinda mwili dhidi ya ufanyaji dhaifu wa kazi wa moyo. Yaani “cardiac failure”. na pia husaidia katika kuimarisha afya ya moyo.

 

Karanga husaidia katika kuboresha ngozi. Virutubisho vilivyomo kwenye karanga pamoja na vitamin C husaidia katika kuilinda ngozi dhili ya mikunjo mikunjo, madowa madowa na kuifanya ngozi iwe ang’avu, yenye majimaji na iyoyokuwa na ukavu au mikunjomikunjo. Uwepo wa anti-ageing phytohemical inayotambulika kama reseveratrol husaidia katika kumfanya mtu asizeheke kwa haraka.

 

Karanga husaidia katika kuimarisha afya ya mifupa, kutokana na uwepo wa madini kama potassium, calcium, sodium, magnesium na phosphorus. Pia kwa wajawazito nivyema wakatumia chakula hiki kwani kuna protini na madini kwa ajili ya afya ya mama na mtoto

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 2535

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 web hosting    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Faida za kula viazi mbatata

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula viazi mbatata

Soma Zaidi...
Faida za kula parachichi

Somo Hili linakwenda kukuletea faida za kula parachichi

Soma Zaidi...
Vinywaji salama kwa mwenye kisukari

Vijuwe vinywaji salama kwa mgonjwa wa kisukari

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kitunguu maji

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kitunguu maji

Soma Zaidi...
Vyakula hatari kwa afya ya moyo

Hivi ni vyakula hatari kwa watu wenye maradhi ya moyo. Vyakula hivi si salama kwa afya ya moyo

Soma Zaidi...
FAIDA ZA VITAMINI C NA UMUHIMU WA VITAMINI C MWILINI

Utafahamu faida za vitamini C mwilini pamoja na kujuwa umuhimu wa vitamini C

Soma Zaidi...
Dalili za ukosefu wa madini ya iodini (goiter)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za upungufu wa iodini ambapo kitaalamu hujulikana Kama goiter. Goiter Ni Sababu ya kawaida ya goiter duniani kote ni ukosefu wa iodini katika chakula. Nchini Marekani, ambako utumiaji wa chumvi yenye iodini ni j

Soma Zaidi...
Fahamau protini na kazi zake, vyakula vya protini, na athari za upungufu wake.

unayopaswa kuyajuwa kuhusu protini na vyakula vya protini, faida zake na hasara zake. Madhara ya kiafya yanayohusiana na protini pamoja na kuyaepuka madhara hayo

Soma Zaidi...
Sababu zinazoweza kusababisha kukosa choo (kinyesi)

Kukosa choo aina ya kinyesi ni kutoweza kudhibiti kinyesi, hivyo kusababisha kinyesi kuvuja bila kutarajiwa kutoka kwenye puru. Pia huitwa kutoweza kudhibiti utumbo, Upungufu wa kinyesi hutoka kwa kuvuja mara kwa mara kwa kinyesi huku ukipitisha gesi had

Soma Zaidi...
Fida za kula uyoga

Uyoga pia ni katika vyakula vya asili, ijapokuwa upatikanaji wake umekuwa mchache siku hizi. Shukrani ziwaendee wataalamu wa kilimo, kwa sasa tunaweza kuzipata mbegu za uyoga kutoka maabara na kulima uyoga popote pale. Wataalamu wa mimea wanaamini kuwa uy

Soma Zaidi...