Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula karanga
. Karanga (ground nuts)
Karanga ni katika vyakula vya asili na ni kiungio cha mboga kwa jamii nyingi sana Tanzania na dunia kwa ujumla. Kama vilivyo vyakula vingine karanga ni katika vyakula vyenye virutubisho vingi. Ndani ya karanga kuna fotale, vitamin E, madini ya copper na arginine. Pia karanga ni chanzo kizuri cha omega-3 fatty acid, vitamin E na ijulikane kuwa fatty acid ni muhimu sana kwa afya ya moyo.
Ndani ya kjaranga kuna antioxidant iitwayo phenolic, polyphenol na resveratrol hizi husaidia katika kulinda mwili dhidi ya stress yaani misongo ya mawazo, na husaidia pia katika kulinda mwili dhidi ya maradhi ya saratani. Pia husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini yaani mfumo wa kupambamba na maradhi na mashambulizi ya magonjwa.
Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa aina ya mafuta (fat) yaliyomo kwenye karanga ni mafuta ambayo ni salama kwa afya ya moyo. Kitaalamu aina ya fat iliyomo kwenye karanga ni monosaturated fat na polyunsaturated fat kwa ufupi fat hizi ni salama kwa afya ya moyo na mfumo mzima wa usukiumwaji wa damu. Kwani fat hizi husaidia katika kupunguza cholesterol kwenye damu hivyo hupunguza hatari ya kupata maradhi ya moyo.
Karanga pia ni chanzo kizuri cha protini. Itambulike kuwa protini ni katika virutubisho muhimu na vinavyotakiwa kwa kiwango kikubwa ndani ya miili yetu. Seli za mwili zinahitaji protini kuweza kukuwa na kutengenezwa upya. Ukuaji wa mwili na uponaji wa vidonda na majeraha unahitaji protini.. watoto wanatakiwa wapewe vyakula vya protini kwa kiasi kikubwa zaidi ili kuwezesha maendeleo ya ukuaji wao.
Tofauti na protini mwili unahitaji madini kwa kiwango kinachohitajika. Katika karanga kuna aina mbalimbali za madini kama vile magnesium, phosphorus, potassium, zinc, calcium na sodium. Madini yote haya husaidia katika ukuaji wa mwili na mwili kufanya kazi vyema.
Mafuta ya karanga yana fatty acid ambayo hutambulika kuwa inaongeza lipoprotein ndani ya mwili inayojulikana kama “good cholesterol” yaani cholesterol iloyo safi. Hii ni muhimu katika kuimarisha afya ya moyo na ubongo. Pia madini ya copper yaliyomo kwenye karanga husaidia katika kuzuia maradhi ya moyo yaani “coronary heart diseases”. pia vitamin B1 (thiamine) ni virutubisho muhimu katika kulinda mwili dhidi ya ufanyaji dhaifu wa kazi wa moyo. Yaani “cardiac failure”. na pia husaidia katika kuimarisha afya ya moyo.
Karanga husaidia katika kuboresha ngozi. Virutubisho vilivyomo kwenye karanga pamoja na vitamin C husaidia katika kuilinda ngozi dhili ya mikunjo mikunjo, madowa madowa na kuifanya ngozi iwe ang’avu, yenye majimaji na iyoyokuwa na ukavu au mikunjomikunjo. Uwepo wa anti-ageing phytohemical inayotambulika kama reseveratrol husaidia katika kumfanya mtu asizeheke kwa haraka.
Karanga husaidia katika kuimarisha afya ya mifupa, kutokana na uwepo wa madini kama potassium, calcium, sodium, magnesium na phosphorus. Pia kwa wajawazito nivyema wakatumia chakula hiki kwani kuna protini na madini kwa ajili ya afya ya mama na mtoto
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula panzi senene na kumbikumbi
Soma Zaidi...Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula mihogo
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula peazi
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna nzuri ya kuandaa mchai chai kwa ajili ya matumizi mbalimbali, Ili kutumia mmea wa mchai chai zifuatazo ni mbinu za kuandaa mmea huu.
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha madhara ya kuwa na mafuta mengi mwilimi
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi juu ya madini ya zinki na faida zake katika mwili wa binadamu,
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula fenesi
Soma Zaidi...Pera ni tunda bora lakini pia ni dawa, tambua umuhimu wa tunda hili kiafya
Soma Zaidi...