MATUNDA YENYE VITAMINI C KWA WINGI
Matunda yenye vitamni C kwa wingi ni machungwa, maembe, ndimu na limao, endelea kusoma

MATUNDA YENYE VITAMINI C KWA WINGI
Vitamini C ni katika vitamini ambavyo wili unavihitajia kwa wingi kwa lengo la kuboresha mfumo wa kinga mwilini. Tunaweza kupata vitamini hivi sana kutoka kwenye matunda. Katika makala hii nitakwenda kukutajia matunda aina 7 ambayo yana vitamini c kwa wingi sana.
Aina ya matunda yenye vitamini C
1.Embe, embe linafahamika kwa utamu wake na uchachu wake. Vitamini C vinapatikana kwa wingi zaidi kwenye matunda yenye uchachu.
2.Mapera; tunda hili limeenea maeneo mengi, kula pera likiwa limewiva ama likiwa limekomaa na tayari kulila.
3.Papai, mapapai ni katika matunda mabyo yana rangi ya njano. Matunda haya yana sifa ya kuwa na vitamini hivi kwa wingi
4.Karoti, kitaalamu karoti si tunda. Lakini nimependa kuliweka kwenye orodha hii kwa sababu watu hutafuna karoti na kuifanya kama tunda.
5.Limao na ndimu, hapa ndipo penyewe kwa vitamini C. limao na ndimu ndio matunda yenye uchachu kwa wingi na hivyo kukusanya vitamini C.
6.Nanasi, tunda hili pia ni katika matunda yenye rangi ya njano. Sifa hii hufanya tunda hili liwe miongoni mwa vyanzo vikuu vya vitamini C.
7.Chungwa, machungwa yana faida nyingi mwilini ikiwemo kutupatia vitamini C kwa wingi.
8.Nyanya, pensheni, palachichi, tufaha na pilipili haya ni katika matunda mengine yenye vitamini C kwa wingi kabisa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Faida za kiafya za kula uyoga
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula uyoga
Soma Zaidi...Vyakula vyenye vitamini C kwa wingi
Vitamini C kwa wingi hupatikana kwenye machungwa, maembe, mananasi, limao na ndimu
Soma Zaidi...Vyakula kwa wagonjwa wa sukari na utaratibu wao wa lishe
Post hii inakwenda kukufundisha utaratibu wa lishe kwa wagonjwa wenye kisukari pamoja na vyakula salamakwao.
Soma Zaidi...FAIDA ZA MAJI MWILINI
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...vyakula vya kuongeza damu, dalili zake na sababu za upungufu wa damu
Zijuwe sababu za upungufu wa damu, dalili za upungufu wa damu na kazi za damu mwilini,n avyakula vya kuongeza damu
Soma Zaidi...Kazi kuu tatu za vitamini C mwilini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kazi kuu tatu za vitamini C
Soma Zaidi...