vyakula vya kuongeza damu, dalili zake na sababu za upungufu wa damu

vyakula vya kuongeza damu, dalili zake na sababu za upungufu wa damu

Zijuwe sababu za upungufu wa damu, dalili za upungufu wa damu na kazi za damu mwilini,n avyakula vya kuongeza damu

vyakula vya kuongeza damu, dalili zake na sababu za upungufu wa damu

Upungufu wa damu, dalili zake na vyakula vya kuongeza damu


VYAKULA VYA KUONGEZA DAMU



Damu ni tishu iliyo katika kimiminika. Katika miili yetu damu ina kazi ya kusafirisha viinilishe na hewa ya oksijeni na kuondoa hewa chafu ya kabonidaiyoksaidi mwilini. Pia urekebishwaji wa joto na usafirishwaji wa homoni ndani ya mwili hutegemea damu. Kwa ufupi damu in akazi nyingi. Upungufu wowote wa damu mwilini unaweza kuleta athari nyingi mbaya za kiafya mwilini. Makala hii inakwenda kukueleza njia ya kuongeza damu kwa haraka.


Kazi za damu mwilini
1.Kusafirisha viinilishe kutoka katika mfumo wa mmengโ€™enyo wa chakula kwenda maeneo mbalimbali ya mwili.
2.Kusafirisha hewa ya oksijeni kutokakwenye mapafu kwenda maeneo mengine ya mwli.
3.Kusafirisha hewa ya kabonikaiyoksaidi kutoka kwenye seli na kpeleka kwenye mapafu kwa ajili ya kutolewa nje
4.Kudhibiti joto la mwili kwa kulipooza inapohitajika na kuliongeza inapohitajika
5.Kusafirisha homoni kwenda maeneo mbalimbali ya mwili.


Vyakula vya kuongeza damu mwilini
1.Nyama nyekundu kama nyama ya ngโ€™ombe, mbuzi. Kondoo
2.Maini
3.Nyama ya figo
4.Mboga za rangi ya kijani kama mchicha na apinachi
5.Maharagwe
6.Kunde
7.Mayai
8.Nafaka nyinginezo
9.Njegere
10.Koeosho na karanga
11.Samaki
12.Nyama ya ndege
13.Karoti
14.Matikiti
15.Zabibu
16.Viazi vitamu
17.Matunda yenye uchachu kama machungwa, ndimu na limao.
18.Polipili nyekundu


Dalili za kupungua kwa damu mwilini
1.Uchovu wa hali ya juu
2.Udhaifu wa mwili
3.Ngozi kuwa na rangi ya njano au mauko
4.Kupumua kwa shida
5.Mapigo ya moyo kutokuwa ya kawaida
6.Kizunguzungu na kichwa kuhisi chepesi
7.Maumivu ya kifua
8.Miguu na mikono kuwa ya ubaridi
9.Maumivu ya kichwa



Sababu za upungufu wa damu mwilini
1.Upungufu wa madini ya chuma mwilini
2.Upungufu wa vitamini A na B-12 mwilini
3.Maradhi kama HIV, UKIMWI, saratani, mardhi ya figo haya huweza kuleta upungufu wa damu
4.Mfumo wa kinga mwilini kuuwa na kuharibu seli hai nyekundu (autoimmune)
5.Uharibifu wa seli hai nyekundu kufanyika kwa haraka kuliko utengenezwaji.
6.Kuwa na maradhi ya sickle cell




                   


Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views: 8070

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game     ๐Ÿ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii     ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰5 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰6 web hosting    

Post zinazofanana:

Vijuwe vyakula vinavyoongeza damu kwa haraka

Post hii itakufundisha aina za vyakula ambavyo vinaweza kuongeza damu kwa haraka.

Soma Zaidi...
Je ulaji wa boga unafaa kwa mgonjwa wa kisukari?

Je ulaji wa boga unafaa kwa mgonjwa wa kisukari?

Soma Zaidi...
Faida za vyakula vya asili

Posti hii inahusu zaidi faida za matumizi ya vyakula vya asili, kama tunavyojua kwamba mababu na mabibi zetu walitumia vyakula vya asili wakaishi miaka mingi kweli.

Soma Zaidi...
Faida za kitunguu swaumu wakati wa ujauzito

Posti hii inahusu zaidi faida za kitunguu swaumu wakati wa ujauzito, kuna kipindi ambacho wanawake wakati wa ujauzito uchaguza vyakula mbalimbali kuna ambao wanaweza kutumia vitunguu saumu na kupata faida kubwa

Soma Zaidi...
JITIBU KWA KITUNGUU THAUMU: faida za kiafya za kitunguu thaumu

Kitunguu thaumu ni katika viungo vya mboga na chakula.

Soma Zaidi...
Faida za kula Tango

Matunda ya zamani na ya asili, zijuwe faida za kiafya za tango

Soma Zaidi...