Virutubisho vya mwili

Posti hii inahusu zaidi virutubisho vya mwili, ni aina tano za vyakula ambayo ufanya kazi mbalimbali kwenye sehemu za mwili wa binadamu.

Virutubisho vya mwili ni nini?

1.  Virutubisho vya mwili ni makundi yote matano ya vyakula yanayohitajika kwenye mwili wa binadamu Ili kuweza kurutubisha mwili, virutubisho hivi vimegawanyika katika makundi makuu matano ambayo ni wanga, kundi la pili ni protini, kundi la tatu ni vitamin, kundi la nne ni madini na kundi la tano ni maji, makundi haya matano kila kundi huwa na virutubisho tofauti tofauti ambavyo usaidia kujenga mwili.pia virutubisho hivi vina umuhimu mkubwa kwa watoto kama ifuatavyo.

 

2. Uongeza damu kwa watoto.

Tunajua wazi kuwa baadhi ya vyakula kama vile mboga mboga za majani na madini ya chuma usaidia kuongeza damu kwenye mwili kwa hiyo watoto ambao wameweza kula wanaweza kutumia mboga Ili kuepuka tatizo la kupungukiwa kwa damu.

 

3. Pia hivi virutubisho  uongeza hamu ya kula kwa watoto hasa hasa wale kwa wale watoto ambao hawapendi kula mpaka wakabwe, kwa hiyo tunajua wazi kuwa chakula ni dawa kwa hiyo katika chakula Kuna dawa ambayo usaidia kuwepo kwa hamu ya kula.

 

4. Vile vile virutubisho hivi uongeza uchangamfu kwa watoto waliozorota na kufanya mtoto awe na mwonekano Bora wa ki afya, kwa hiyo mtoto alichanganyiziwa vyakula mbalimbali uweza kuwa na virutubisho vyote vya mwili na kufanya awe na furaha kuliko kutumia aina Moja tu ya vyakula.

 

5. Huondoa unyafuzi na kiriba tumbo kwa mtoto.

Kuna watoto wengine ambao huwa na unyafuzi pamoja na kiriba tumbo hali hii uwapata kwa sababu ya kukosa vyakula vyenye mlo kamili kwa hiyo Akiongezewa vyakula mbalimbali anaweza kuwa na afya nzuri na mwonekano Bora.

 

6. Pia uondoa kudumaa kwa mtoto na kuongeza akili kwa mtoto.

Kwa kawaida tunajua wazi kuwa chanzo cha mtoto kudumaa na kuwa na akili ndogo usababishwa kukosekana na chakula Bora kwa wakati wa siku zake za mwanzoni, kwa hiyo mtoto akipewa vyakula mbalimbali na vilivyochanganywa vizuri na kwa wakati tofauti ana uwezekano mkubwa wa kutokudumaaa na kuwa na akili timamu katika makuzi yake.

 

7. Uweka kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Tunajua kuwa chakula ni dawa hasa hasa kama mtoto anakula vyakula mbalimbali na vyenye mchanganyiko mzuri na kwa mda tofauti na vilivyoandaliwa kwa usafi nakuhakikishia kuwa mtoto hawezi kupata magonjwa, kwa hiyo virutubisho kwenye chakula usaidia kukinga mtoto dhidi ya magonjwa.

 

8. Virutubisho kwenye mwili usaidia kufanya mwili watoto kuwa na mwonekano mzuri,kucha za mtoto kuwa nzuri pamoja na nywele za mtoto, hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa vyakula vya kujenga mwili kwenye chakula na kufanya sehemu za mwili za mtoto kuonekana safi kama vile ngozi, kucha na nywele.

 

9. Pia umfanya mtoto aweze kuona vizuri.

Kwa sababu ya kuwepo kwa vitamin mbalimbali kwenye vyakula hasa vitamin A umfanya mtoto aweze kuona vizuri, kwa hiyo ni vizuri kabisa kumpatia mtoto vyakula vyenye wingi wa vitamin A Ili aweze kuona vizuri.

 

10. Pia virutubisho kwenye mwili usaidia kuimarisha mifupa na meno kwa sababu ya kuwepo kwa madini mbalimbali kama vile calcium, kwa kula vyakula vyenye madini yanayoimarisha meno na mifupa usaidia kuepuka hatari ya kuwepo kwa matatizo ya meno na mifupa.

 

11. Upunguza sumu mwili kwa kuon doa antioxidant mwili  hivyo kupunguza kiasi cha macromolecules ambazo ni sumu kwenye mwili wa mtoto,kwa hiyo walezi wote na akina mama wanapaswa kuwapatia watoto vyakula mbalimbali vyenye mchanganyiko mzuri Ili kuweza kuepuka kuongeza kiwango cha sumu mwilini.

 

12. Pia virutubisho vya chakula mbalimbali uondoa tatzo la aleji au mzio kwa watoto kwa sababu ya kuwepo kwa mchanganyiko wa vyakula mbalimbali, kwa hiyo tuache tabia ya kutumia chakula cha aina Moja kwa watoto.

 

13. Pia usaidia mtoto apate usingizi mzuri kwa sababu ya kuwepo kwa dawa kwenye mchanganyiko wa vyakula ambazo uzuia matatizo ya kutopata usingizi.

 

14. Vile vile usaidia mtoto aweze kupata choo vizuri bila ya kuwepo choo kigumu au kuharisha kwa sababu ya kuwepo kwa mchanganyiko wa vyakula mbalimbali. Pia mchanganyiko wa vyakula mbalimbali uondoa homa kwa watoto.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 2270

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Vyakula vya vitamin B

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya vitamin B

Soma Zaidi...
Faida za kula tikiti

Somo hili linalenga kukujuza juu ya umuhimu wa tikiti kwenye afya ya mwili

Soma Zaidi...
Kazi ya Piriton

Posti hii inahusu zaidi kazi ya Piriton katika kutibu mzio au akeji ni dawa ambayo kwa lingine huitwa chlorpheniramine Maleate.

Soma Zaidi...
Ulaji wa protini kupitiliza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu athari za ulaji wa protini kupitiliza

Soma Zaidi...
Vyakula salama na vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo

Kamala hii inakwenda kufundisha vyakuna na vinjwaji salama anavyopaswa kutumia mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Pia utajifunza vyakula na vinywaji hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Soma Zaidi...
Faida za kula tikiti

Ukubwa wa tikiti unasadifu yaliyopo, kwani kuna fgaida akubwa sana za kiafya katika kula tikiti

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula samaki

Posti hii itakwenda kukupa faida za kula samaki kwenye mwili wako.

Soma Zaidi...