image

Vyakula vya vitamini na faida zake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya vitamini na faida zake

VYAKULA VYA VITAMINI NA FAIDA ZAKEVitamin ni muhimu katika kuhakikisha kuwa mwili unatumia virutubisho vingine kufanya kazi zake. Kuna vitamin A,B,C,D,E na K. vitamin B vimegawanyika katika makundi kama vitamin B1,B2,B6, na B12. Ukosefu wa vitamin vyovyote kati ya hivi unaweza ukapelekea matatizo makubwa kwa afya ya mtu.Vitamin A,D,E na K, vinaitwa fat soluble vitamin. Hivi nhuweza kuhifadhiwa ndani ya mwili. Hivyo hatuhitaji kula vyakula kuvipata kwa kila siku. Kwa upande mwengingine vitamin B na C huitwa water soluble vitamin, hivi havihifadhiwi ndani ya mwili, hivyo tunahitaji kula vyakula vyenye vitamin hivi kwa kila siku.Vitamin A hupatikana kwenye maziwa, maini, karoti,machungwa, na mboga za rangi nya njano.. vitamin hivi ni muhimu kwa kusaidia afya ya macho na mfumo wa upumuaji (respiratory track). Ukosefu wa vitamin hivi unapelekea mtu kushindwa kuona wakati wa usiku. Mwili unakuwa ni rahisi kupata mashambulio pindi mtu akiwa na vitamin A kwa uchache.Vitamin B1 hivi hupatikana kwenye nyama, maini, mayai,hamira na mchele. Husaidia katika kuhakikisha michakato ya kikemikali ndani ya seli inafanyika vizuri (metabolism). Pia husaidia katika kuunganisha taarifa za misuli. Ukosefu wa vitamin hivi unapelekea ugonjwa wa beriberi ambopo mtu anakosa hamu ya kula. Misuli kukaza pia ni dalili ya upungufu wa vitamin hivi. Wakati mwingine moyo kushindwa kufanya kazi ni kutokana na upungufu wa vitamin hivi.Vitamin B2 hivi hupatikana kwenye nyama, maini, nafaka na hamira. Husaidia katika ufanyikaji wa michakato ya kikemia ndani ya seli (metabolism). Kupasuka kwa midomo ni dalili ya ukosefu wa vitamin hiviVitamin B3 hupatikana kwenye samaki, karanga,nyama, mchele usio kobolewa na hamira.. huhitajika kwa ajili ya kuwasaidia enzymes kubadilimchakula kuwa energy. Pellagra ni ugonjwa unaotokana na upungufu wa vitamin hivi. Mgonjwa anakosa hamu ya kula, misuli kukosa nguvu na kuharibika kwa ngozi.Vitamin B12 hivi hupatikana kwenye samaki,nyama, mayai,maziwa na maini. Husaidia katika utengezaji wa damu, na utengezaji wa genetic meterials. Ugonjwa wa anaemia, upungufu wa uzito na nerve damage hutokana na upungufu wa vitamin hivi.Vitamin C hivi hupatikana kwenye matunda yenye uchachu kama limao na machungwa. Mboga za kijani,na nyanya. Husaidia mwili kufyonza madini ya chuma. Kukosa nguvu za misuli,na maumivu ya viungio(joints)kutokwa na damu kwenye mafinzi kuchelewa kupona kwa vidonda na kuumwa mara kwa mara ni dalili ya upungufu wa vitamin hivi.Vitamin D hupatikana kwenye mayai, maziwa, samaki na maini. Husaidia katika kukuwa na kuimarisha meno na mifupa. Ugonjwa wa matege kwa watoto na osteoporosis yaani mifupa kuwa milaini husababishwa na upungufu wa vitamin D.Mitamini E hupatikana kwenye alizeti, butter, mchele na peanuts. Husaidi akatika kulinda utando uliopo ndani ya mwili. Mfumo wa fahamu kutokuwa katika hali ya kawaida ni dalili ya upungufu wa vitamin EVitamin K hupatikana kwnye maini na mboga za majani. Husaidia katika kuganda kwa damu baada ya kupata jeraha. Damu kutoka kwa wingi baada ya jeraha ni upungufu wa vitamin K.Mtu atapata matatizo pia kama hata kunywa maji ya kutosha kwa siku. Maumivu ya kishwa huweza kusababishwa na kutokunywa maji ya kutosha. Choo kuwa kigumu huweza kusababishwa na uchache wa kunywa maji.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1703


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Faida kula fenesi
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula fenesi Soma Zaidi...

Fahamu vitamini K na kazi zake, vyakula vya vitamini k na athari za upungufu wake
kuhusu vitamini K, wapi tutavipata, ni zipi athari zake na ni zipi kazi zake mwilini. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula fyulisi/ peach
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula fyulisi/peach Soma Zaidi...

Asili ya Madini ya shaba
Posti hii inahusu zaidi asili ya madini ya Shaba, ni sehemu ambapo madini ya Shaba yanaweza kupatikana ni katika mimea na wanyama Soma Zaidi...

Vyakula vya kupunguza presha ya kupanda
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula ambavyo vinaweza kupunguza presha ya kupanda Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula kitunguu maji
Soma Zaidi...

Faida za ubuyu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula ubuyu Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula maboga
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula maboga Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamin C
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za vyakula vya vitamin C Soma Zaidi...

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA BAMIA (OKRA)
Makala hii inakwenda kukuonyesha faida za kula bamia kwa afya afya Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula bamia
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula bamia Soma Zaidi...

Faida za kiafya za viazi vitamu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula viazi vitamin Soma Zaidi...