ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1.
ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI
1.kutafuta msomaji mwenye sauti mzuri. Inapendeza mtu mwenye kusikiliza qurani asikilize kwa yule mwenye sauti ambayo ataipenda. Jambo hili litampa hamu ya kusikiliza qurani. Hata mtume alikuwa na wasomaji wake maalumu wa kumsomea qurani. Amesimulia Jabir kuwa mtume amesema “hakika mtu mwenye sauti nzuri anaposima qurani ni yule ambaye pindi mnapomsikia anasoma qurani mnamdhania kuwa anamuogopa Allah. (amepokea ibn majah).
2.Kuleta mazingatio pamoja na kufikiri kwa kina maana. Inatakiwa nayesikiliza qurani sio tu atosheke na sauti lakini anatakiwa awe na mazingatio juu ya kile ambacho kinasomwa.
3.Mwenye kusikiliza qurani awe ni mzuri wa kusikiliza na mwenye kunyamaza. Amesema Allah kuwa “na pindi inaposomwa qurani isikilizeni na nyamazeni ili mrehemewe. (surat al-a’araaf 204)
4.Kulia na kuwaidhika na kinachozungumzwa. Kama ilivyo kwa msomaji hata msikilizaji pia ni vema akalia kwa kuwaidhika na qurani. Amesema Allah “na pindi wanaposikia yale yaliyoteremswa kwa Mtume utayaona macho yao yanabubujika machozikutokana na yale walioyajua katika haki” (surat maaidah 83)
5.Kuleta khushui, unyenyekevu na kutukuza kitabu cha Allah. Mwenye kusikiliza qurani ahakikishe kuwa analeta khushui na unyenyekevu, awe na utulivu huku akijuwa ukubwa wa kitabu cha Allah.
6.Kusujudi pindi unaposikia aya ya kusujudi. Sijida hii ni sunnah na mbele za maimamu wa fikh wapo wanaiita ni swala kama ilivyo swala ya jeneza. Hivyo haipasi mtu kusujudi akiwa hana udhu. Atasema mwenye kusujudi sijida hii “SAJADA WAJHI LILLADHII KHALAQANIY WASHAQA SAM’AHU, WABASWARAHU, BIHAWLIHI, WAQUWATIHI” amsesimulia ‘Aisha. Aya hizi za sijida zipo 15 katika qurani ambazo ni aya ya mwisho ya surat al-araf, aya ya 15 ya surat rad, aya ya 50 ya surat nahli, aya ya 109 ya surat israa, aya ya 58 ya surat maryam, aya ya 18 ya surat haj, aya ya 77 ya ryrat haj, aya ya 60 ya surat furqan, aya ya 26 ya surat naml, aya ya 15 ya surat sajda, aya ya 38 ya surat fusilat, aya ya 62 ya surat najmi, aya ya 21 ya surat inshiqaq, aya ya 19 ya surat ‘alaq.
Umeionaje Makala hii.. ?
SURAT AL-QURAYSH Sura hii ina majina mawili.
Soma Zaidi...Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.
Soma Zaidi...Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet
Soma Zaidi...TAHADHARI KWA WASOMAJI WA QURAN Wasomaji wa qurani wawe na tahadhari katika usomaji wao.
Soma Zaidi...Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba
Soma Zaidi...Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu.
Soma Zaidi...