image

ADABU ZA KUSOMA QURAN

Adabu wakati wa kusoma quran 1.

ADABU ZA KUSOMA QURAN

imageimage Adabu wakati wa kusoma quran
1.kuwa na ikhlas. Hapa jinachokusudiwa ni kuwa na nia iliyo takata kuwa unasoma kwa ajili ya Allah na si vinginevyo. Kama ilivyokuwa ibada zote anatakiwa afanyiwe Allah kama Mtume alivyosea katika hadithi sahihi aliyoipokea Bukhari, Muslim kwa mtume amesema “hakika si vinginevyo amali (hulipwa) kwa (kuzingatia) nia...” . Hivyo msomaji asifanye ili watu wamsikie eti yeye ndo bigwa ila asome kwa kutaraji radhi za Allah.

2.Kuwa na khushui, na kuleta mazingatio. Mwenye kusoma qurani ajitahidi ahudhurishe moyo wake wote kwenye lile analolifanya nalo ni kusoma qurani. Pia alete mazingatio kama anaelewa nini qurani inazungumza. Amesema Ibraahim Khawas kuwa: dawa ya nyoyo ni mambo matano ambayo nui: kusoma Qurani kwa mazingatio, kufunga, kusimama usiku na kukaa na watu wema.

3.Kulia wakati wa kusma Qurani. Mwenye kusoma qurani huenda ikamfanya alie, hivi ni vizuri sana na ni sifa ya watu wema. Hata mtume alikuwa naposomewa qurani alikuwa akilia.

4.Kusoma kwa sauti. Mzomaji wa qurani anatakiwa atoe sauti yake yaani asome kwa sauti kwa namna ambayo hatawaudhi watu walio karibu nae kama mtu aliolala, anayeswali ama waliokuwepo kwenye mazungumzo yake.

5.Kusoma kwa sauti nzuri. Msomaji wa qurani anatakiwa ajitahidi kuwa na sauti nzuri. Zipo riwaya nyingi ambazo zinaonesha msisitizo juu ya kuremba sauti. Mapaka mtume akasema “mtu amabye hasomi qurani vizuri sio katika sisi.” katika mapokezi mengina ya Bukhari, muslim na Abuu Dawd ni kuwa Allah amemuamrisha mtume kusoma qurani kwa sauti nzuri.

6.Tajweed. Maana ya tajweed ni kuisoma qurani kwa hukumu zake. Qurani ina hukumu zake katika kusoma. Kila herufi inatakiwa itamkwe kwa namna ileile inayotakiwa. Kila herufi ipewe haki yake katika idh-hari, ikh-fai, id-ghami, mada, ghunnah na ntingineso nyingi.

7.Kudhihirisha maana. Mwenye kusoma qurani ajitahidi kudhihirisha maana wakati anaposoma. Mtu anatakiwa ajuwe kitu ambacho kinazungumziwa katika aya anayoisoma.

8.Kusoma kwa kupumzika. Kwenye kusoma qurani natakiwa asisome mfululizo ila awe ana viu vya kupumzika. Amesimulia Ummu salama kuwa alikuwa mtume anapumzika kwenye usomaji wake alikuwa akisoma AL-HAMDU LILLAHI RABIL-ALAMIIN kisha hupumzika kisha anasoma AR-RAHMAANIR-RAHIIM kisha hupumzika, kisha husoma MALIKI YAUMIDIIN (amepokea Tirmidh).

9.Kuchunga hukumu za waqfu. Waqfu unaweza kusema ni vituo vya kupumzikia au kutokupumzika au kuunga maneno wakati wa kusoma qurani. Kuna ambavyo inajuzu kuunganisha (صلي), au kujuzu kusimama (قلي), au kujuzu kusimama ila kwa ufupi (ج), au vya lazima kusimama (ه) au ambavyo haitakiwi kusimama (لا).

10.Kutokusoma harakaharaka (mbiombio). Basi mwenye kusoma Qurani ajitahidi kusoma katika mpangilio unaopendeza. Sio mbiombio kiasi kwamba inaweza kuwa rahisi kufanya makosa ya kiusomaji.

11.Inapendeza pia kutwaharisha kinywa kwa kupiga mswaki kabla ya kusoma qurani.

12.Kusoma kwenye msahafu. Hili ni jambo ambalo linapendeza kwa wale wanaotaka kuhifadhi qurani. Tofauti na kusikiliza ikisomwa wawe wanaangalia maandishi ya qurani hasa kwenye msahafu.

13.Kumuomba Allah unaposoma qurani. Amesema Mtume “mwenye kusoma qurani basi na amuombe Allah kwayo, kwani hakika watakuja watu watasoma qurani na wataomba kwayo watu” (amepokea tirmidh)

14.Msomji awe ni twahara. Hili ni jambo linalipendeza sana kwa anayesoma qurani awe na tahara. halikadhalika mtu mwenye janaba haruhusiwi kusoma qurani ila kama ataisoma kama dua. Kwa mfano akisoka adhkari za kulala ambazo zina qurani ndani yake.

15.Kuanza kusoma qurani kwa kujikinga na shetani yaani kusema “A’UDHU BILLAHI MINAS-SHAYTWANIR-RAJIIM”

16.Kuomba dua unapofika sehemu za heri. Amepokea hadithi Muslimu kuwa Abuu ‘Abdallah Hudhaifiya amesimulia kuwa alikuwa Mtume “… Anaposoma aya yenye tasbih huleta tasbih, na anaposoma aya yenye maombi(dua) huomba (dua), anaposoma aya yenye t’awdh (kutakahifadha) hutaka hifadha”

17.Kujikinga na shari anaposoma aya za shari. Yaani anaposoma aya ambazo zinataja adhabu za makafiri na watu waovu humuomba Allah amuepushe kuwa katika kundi hilo.

18.Kleta sijdat tilawa unapofika sehemu za kusujudi.


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 891


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Sababu za kushuka surat al Quraysh
Qurayh ni jina la kabila la Mtume Muhammad S.A.W. Sura hii itakwenda kukujulisha neema ambazo Maquraysh wamepewa na hawataoewa wao wowote baada ya wao. Soma Zaidi...

Saratul-asr 103
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid
Hapa utajifunza maana ya iqlab katika usomaji wa Quran kwa tajwid Soma Zaidi...

Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake
Soma Zaidi...

Hukumu za mim sakina na tanwinkwenye hukumu za tajwid
Hukumu za kim sakina na tanwin ni idgham shafawiy, idh-har shafawiy, na Ikhfau shafawiy Soma Zaidi...

HUKUMU ZA QALQALA
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Sababu za Kushuka Surat Al-Masad (tabat yadaa) na fadhila zake
4. Soma Zaidi...

Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran
Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq
Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq. Soma Zaidi...

quran na sunnah
Soma Zaidi...

Hukumu ya tafkhim na tarqiq katika usomaji wa Quran tajwid
Tarqiq ni kuisoma herufi kwa kuipa wepesi na tqfkhim ni kuisoma herufi kwa kuipa uzito. Soma Zaidi...

Hukumu za Tajwid katika usomaji wa bismillah (basmalah)
Hapa utajifunza kanuni za tajwid katika kusoma bismillah au basmalah. Soma Zaidi...