Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab



Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu." Na taifa moja miongoni mwao liliposema "Enyi, wenyeji wa Yathribu (Madina)! Hamna mahali pa kukaa nyinyi, basi rudini Na kundi jingine miongoni mwao likaomba ruhusa kwa Mtume kwa kusema: "Hakika nyumba zetu ni tupu, (hapana watu, tunakwenda zetu)," lakini hazikuwa tupu, hawakutaka ila kukimbia tu. Na lau kama yaliingia (Majeshi ya makafiri) juu yao katika pande zote , kisha wakaombwa kufanya vita (juu ya Waislamu) wangevifanya, na wasingelikaa humo (Madina tena) ila muda kidogo tu (33:12-1 4)


Na kwa yakini walikwishafanya ahadi na Mwenyezi Mungu zamani ya kwamba hawatageuza migongo ; na ahadi ya Mwenyezi Mungu ni yenye kuulizwa. (33:15)



Sema: "Kukimbia hakutakufaeni kama mkikimbia mauti au kuuawa, na kwa hivyo, hamtastareheshwa ila kidogo tu, (kisha mara mtakufa)." Sema: "Ni nani ambaye aweza kukulindeni na Mwenyezi Mungu kama (Mungu) akikutakieni uovu, au akikutakieni rehema?" Wala hawatapata mlinzi wala msaidizi kinyume cha Mwenyezi Mungu.Bila shaka Mwenyezi Mungu anawajua wale wanaojizuia miongoni mwenu (wasende vitani pamoja na Mtume) na wawaambiao ndugu zao; "Njooni kwetu (wala msende kwa Muhammad);" wala hawendi katika mapigano ila kidogo tu (ili kuwadanganya Waislamu). (33:16-1 8)


Wakakufanyieni choyo (kukusaidieni) lakini inapokuja hofu, utawaona wanakutazama, macho yao yanazungukazunguka kama yule aliyezimia kwa mauti; lakini hofu inapoondoka, wanakuudhini kwa ndimi zao kali, wanaifanyia choyo kheri, (hawataki kusaidia). Hao hawakuamini, kwa hivyo Mwenyezi Mungu ameviondoshea thawabu vitendo vyao; na hayo ni sahali kwa Mwenyezi Mungu. (Mpaka sasa kwa woga wao) Wanafikiri yale makundi (ya maadui) hayajaondoka. Na kama makundi hayo yangekuja (tena), wangependa laiti wangekua wako jangwani pamoja na Mabedui, wakiuliza tu habari zenu. Na kama wangalikuwa pamoja nanyi wasingalipigana ila kidogo tu. (Mara wangelikimbia kwa woga wao). (33:19-20)



Sifa za wanafiki zilizoainishwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo:
(i) Humdhania Mwenyezi Mungu na Mtume wake dhana mbaya. Walisema wakati ule wa Mtume (s.a.w): "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu."
(ii) Huwahofisha na kuwakatisha tamaa waumini ili warudi nyuma wasipambane na maadui wa Uislamu.
(iii) Hutoa nyudhuru za uwongo ili kuepa majukumu ya kuuhami Uislamu na kuuendeleza.
(iv) Huvunja ahadi kila wanapoahidi.
(v) Hawako tayari kupata misukosuko kwa ajili ya Uislamu na huogopa kufa. Hivyo hujitenga mbali na mapigano dhidi ya maadui wa Uislamu.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 742

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Nguzo za imani

Zifuatazo Ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kwa nini uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza

Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.

Soma Zaidi...
KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Makundi ya dini za wanaadamu

Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.

Soma Zaidi...
Nafsi ya mwanadamu inavyothinitisha uwepo wa Allah

Mwanadamu ukifikiria vyema. Kuhusu nafsi yako, hakika utapatabfikra yabuwepp wa Mwenyezi Mungu

Soma Zaidi...
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake

Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.

Soma Zaidi...