Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab



Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu." Na taifa moja miongoni mwao liliposema "Enyi, wenyeji wa Yathribu (Madina)! Hamna mahali pa kukaa nyinyi, basi rudini Na kundi jingine miongoni mwao likaomba ruhusa kwa Mtume kwa kusema: "Hakika nyumba zetu ni tupu, (hapana watu, tunakwenda zetu)," lakini hazikuwa tupu, hawakutaka ila kukimbia tu. Na lau kama yaliingia (Majeshi ya makafiri) juu yao katika pande zote , kisha wakaombwa kufanya vita (juu ya Waislamu) wangevifanya, na wasingelikaa humo (Madina tena) ila muda kidogo tu (33:12-1 4)


Na kwa yakini walikwishafanya ahadi na Mwenyezi Mungu zamani ya kwamba hawatageuza migongo ; na ahadi ya Mwenyezi Mungu ni yenye kuulizwa. (33:15)



Sema: "Kukimbia hakutakufaeni kama mkikimbia mauti au kuuawa, na kwa hivyo, hamtastareheshwa ila kidogo tu, (kisha mara mtakufa)." Sema: "Ni nani ambaye aweza kukulindeni na Mwenyezi Mungu kama (Mungu) akikutakieni uovu, au akikutakieni rehema?" Wala hawatapata mlinzi wala msaidizi kinyume cha Mwenyezi Mungu.Bila shaka Mwenyezi Mungu anawajua wale wanaojizuia miongoni mwenu (wasende vitani pamoja na Mtume) na wawaambiao ndugu zao; "Njooni kwetu (wala msende kwa Muhammad);" wala hawendi katika mapigano ila kidogo tu (ili kuwadanganya Waislamu). (33:16-1 8)


Wakakufanyieni choyo (kukusaidieni) lakini inapokuja hofu, utawaona wanakutazama, macho yao yanazungukazunguka kama yule aliyezimia kwa mauti; lakini hofu inapoondoka, wanakuudhini kwa ndimi zao kali, wanaifanyia choyo kheri, (hawataki kusaidia). Hao hawakuamini, kwa hivyo Mwenyezi Mungu ameviondoshea thawabu vitendo vyao; na hayo ni sahali kwa Mwenyezi Mungu. (Mpaka sasa kwa woga wao) Wanafikiri yale makundi (ya maadui) hayajaondoka. Na kama makundi hayo yangekuja (tena), wangependa laiti wangekua wako jangwani pamoja na Mabedui, wakiuliza tu habari zenu. Na kama wangalikuwa pamoja nanyi wasingalipigana ila kidogo tu. (Mara wangelikimbia kwa woga wao). (33:19-20)



Sifa za wanafiki zilizoainishwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo:
(i) Humdhania Mwenyezi Mungu na Mtume wake dhana mbaya. Walisema wakati ule wa Mtume (s.a.w): "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu."
(ii) Huwahofisha na kuwakatisha tamaa waumini ili warudi nyuma wasipambane na maadui wa Uislamu.
(iii) Hutoa nyudhuru za uwongo ili kuepa majukumu ya kuuhami Uislamu na kuuendeleza.
(iv) Huvunja ahadi kila wanapoahidi.
(v) Hawako tayari kupata misukosuko kwa ajili ya Uislamu na huogopa kufa. Hivyo hujitenga mbali na mapigano dhidi ya maadui wa Uislamu.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 89

Post zifazofanana:-

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPANDWA NA PRESHA
Presha ya kupanda hutokea pale kipimo kinaposoma zaidi ya 120/80mm Hg. Soma Zaidi...

SIKU HATARI ZA KUPATA UJAUZITO KWA MWENYE MZUNGURUKO WA SIKU KIDONGO AU NYUNGI
SIKU YA KUPATA UJAUZITO Kawaida wanawake walio wengi mzunguruko wa siku zao ni siku 28 lakini wapo ambao ni zaidi ya hapo na wapo ambao ni chini ya hapo. Soma Zaidi...

Historia ya adhana na nama ya kuadhini
Soma Zaidi...

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEKUNYWA SUMU
Maisha ya mtu yanaweza kuwa hatarini ama kupotea mara moja baada ya kunywa sumu. Soma Zaidi...

nikiamka asubuhi huwa nakojoa mkojo mchafu sana halafu najiskia vibaya Sana na mwili wote unaniuma je tatizo litakua ni nin
Soma Zaidi...

DARSA ZA TAWHID
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...

Ndoa ya kwanza ya kamaralzamani
NDOA YA HAMU Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISHAQA NA YAQUB
Soma Zaidi...

MAANA YA Quran
Maana na majina ya Quran Maana ya Wahyi. Soma Zaidi...

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii
31. Soma Zaidi...

walioruhusiwa kufungua (kula) mwezi wa ramadhani
Soma Zaidi...

HIKUMU YA BASMALLAH YAANI KUSOMA BISMILLAH
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...