Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun

Wanapokujia wanafiki, husema: "Tunashuhudia ya kuwa kwa yakini wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun

(7) Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun (63:1-8)


Wanapokujia wanafiki, husema: "Tunashuhudia ya kuwa kwa yakini wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu." Na Mwenyezi Mungu anajua kuwa wewe ni Mtume wake na Mwenyezi Mungu anashuhudia ya kuwa hakika wanafiki ni waongo, (wanasema wasiyoyasadiki). (63:1)


Wamevifanya viapo vyao ndizo ngao za kujikingia, wakajikinga na kupitishwa njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hakika ni mabaya kabisa waliyo kuwa wakifanya. Na hayo ni kuwa waliamini, kisha wakakufuru; kwa hivyo muhuri umepigwa juu ya nyoyo zao; kwa hivyo hawafahamu lolote. Na unapowaona, miili yao inakupendeza, na kama wakisema, unasikiliza usemi wao (kwa vile unavyopendeza); lakini wao ni kama boriti zilizoegemezwa; (wamekaa magogo tu hapo, hawafahamu lolote); wanadhani kila kishindo (kinachozuka) ni juu yao, (ni cha kuwatafuta wao). Hao ni maadui, jihadhari nao. Mwenyezi Mungu awaangamizilie mbali! Vipi wanapotoka na haki! (63:2-4)



Na wanapoamabiwa: "Njooni ili Mtume wa Mwenyezi Mungu akuombeeni msamaha (kwa makosa yenu mliyoyafanya), huvigeuza vichwa vyao (kwa kuonyesha kuwa hawataki); na unawaona wanajizuia na wakijiona wakubwa. Ni sawa kwao ukiwatakia msamaha au usiwatakie msamaha, Mwenyezi Mungu hatawasamehe; hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu maasi (wenye kutoka katika taa yake). Hao ndio wanaosema: "Msitoe mali kwa ajili ya wale walioko kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu ili waondokelee mbali (hapa nchini kwetu, Madina)." Na hazina za mbingu na ardhi ni za Mwenyezi Mungu; lakini wanafiki hawafahamu.(63:5-7)


Wanasema: "Tukirudi Madina, Mwenye utukufu atamfukuza mnyonge." Na utukufu hasa ni wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wa Waislamu; lakini wanafiki hawajui. (63:8)



Sifa za wanafiki zilizoainishwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo:
(i) Wanasema wasiyoyasadikisha katika nyoyo zao. Katika aya ya kwanza (63:1), Allah (s.w) amewaita wanafiki waongo kwasababu, pamoja na kudai kuwa wanashuhudia kuwa Muhammad (s.a.w) ni Mtume wa Allah (s.w), wanamkanusha Mtume nyoyoni mwao na katika matendo yao. Hawakuwa tayari kuufuata Uislamu ule aliofundisha Mtume Muhammad (s.a.w).
(ii)Hufanya viapo vyao kuwa blanketi la kufichia maovu wanayoyafanya dhidi ya Uislamu na Waislamu.
(iii)Huonesha Uislamu wao katika mavazi na maneno, lakini katika utendaji wako mbali kabisa na Uislamu.
(iv)Huishi kwa wasiwasi wakikhofia kuwa uovu wao waliouficha utafichuliwa.
(v)Wanazuia watu wasitoe sadaqa zao kuusaidia Uislamu na Waislamu wanaostahiki kusaidiwa.
(vi)Hawako tayari kurejea kwa Mwenyezi Mungu kwa makosa yao.
(vii)Wanaendekeza ubaguzi wa kikabila/ na cha warangi



Kwa kuhitimisha sehemu hii ya "sifa za wanafiki" tumejifunza kuwa wanafiki ni wale watu wanaodai kuwa ni Waislamu, na ilihali vitendo vyao katika maisha ya kila siku ni kinyume kabisa na Uislamu.


"Na katika watu wako wasemao "Tumeamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na hali ya kuwa wao si wenye kuamini." (2:8)
Si wenye kamini kwa sababu tabia na mwenendo wao katika mchakato wa maisha yao kila siku katika ngazi ya binafsi na ya jam ii ni sawa na tabia na mwenendo wa makafiri wanaomkanusha Allah (s.w) na siku ya mwisho. Mnafiki hajiiti mnafiki wala hana alama yoyote katika mwili wake ya kuonesha unafiki wake, bali huwa mnafiki kutokana na tabia yake hata kama atadai kuwa ni Muislamu kwa mavazi, kuswali, Kufunga, kuhiji, n.k. Hivyo Muumini wa kweli hanabudi kuwa Muislamu mtendaji kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah na hanabudi kujiepusha na tabia zote za kinafiki. Waislamu huangukia kwenye unafiki kutokana na moja ya sababu tatu zifuatazo:



(i)Kutokuwa na Elimu sahihi juu ya Uislamu. Elimu sahihi ni ile inayomuwezesha mtu kujua lengo la kuwepo kwake hapa duniani na namna ya kulifikia.
(ii)Kupupia maisha ya dunia kwa dhana kuwa dunia ni sehemu ya starehe.
(iii)Khofu inayotokana na kuogopa kufa au kukabiliwa na magumu mbali mbali yanayosababishwa na maadui wa Uislamu.




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 226


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Juhudi za Waislamu Katika Kuhuisha Harakati za Kiislamu Zama za Nyerere hadi leo
i. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME DHUL-KIFL(A.S)
Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia. Soma Zaidi...

MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA. Soma Zaidi...

KAZI ZA MALAIKA
Malaika wamepewa kazi ya kumtumikia Allah(SW) kwa kumtukuza na kumtakasa, kama wanavyosema wenyewe:Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi. Soma Zaidi...

UANDISHI WA HADITHI WAKATI WA TABI'INA
Wakati wa Wafuasi wa masahaba (Tabi'ina)101-200 A. Soma Zaidi...

Kumuandaa Maiti kabla ya kufa ama kukata roho
Soma Zaidi...

Vita vya Badr: Chanzo na sababu za vita vya Badr, Mafunzo ya Vita Vya Badr
Vita vya Badri. Soma Zaidi...

HUKUMU YA KUUWA MTU (KUMWAGA DAMU) KWENYE UISLAMU
' ' ' ' ' ' ': ' ' ' ' ' ' ' ' "' ' ' ' ' [ ' ' '?... Soma Zaidi...

Mbinu Alizozitumia Nabii Shu'ayb(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe Wake
Soma Zaidi...

Kifo cha Khalia Uthman kilivyotokea
Soma Zaidi...

Bani Israil Kuabudu Ndama
Wakati Nabii Musa(a. Soma Zaidi...