Menu



Adabu ya kuingia katika nyumba za watu

Enyi mlioamini!

Adabu ya kuingia katika nyumba za watu

(f) Adabu ya kuingia katika nyumba za watu


Enyi mlioamini! Msiingie nyumba ambazo si nyumba zenu mpaka muombe ruhusa, (mpige hodi) na muwatolee salamu waliomo humo. Hayo ni bora kwenu; huenda mtakumbuka (mkaona ni mazuri haya mnayoambiwa).



Na kama hamtamkuta humo yeyote, basi msiingie mpaka mruhusiwe . na mkiambiwa "Rudini," basi rudini; hili ni takaso kwenu. Na Mwenyezi Mungu Anajua mnayoyaatenda. Si vibaya kwenu kuingia majumba yasiyokaliwa, (yasiyofanywa maskani: kama mahoteli, maktaba), ( bila kupiga hodi), ambamo humo mna manufaa yenu; na Mwenyezi Mungu Anajua mnayoyadhihirisha na mna yoyaficha. (24:27-29)



Kutokana na aya hizi tunajifunza adabu za kuingia katika nyumba za watu kama ifuatavyo:


(i)Hairuhusiwi mtu kuingia nyumba ya mtu bila ya kubisha hodi. Hata kama utaukuta mlango uko wazi, huruhusiwi kuangaza macho ndani. Hivyo wakati wa kubisha hodi unatakiwa uwe pembeni mwa mlango, kiasi kwamba hata kama mlango umefunguliwa usiweze kumuona mtu au vitu vilivyomo ndani. Vile vile hairuhusiwi kubisha hodi kupitia mlango wa uani au madirishani. Hekima ya amri hii ya kubisha hodi, ni kulinda haki ya faragha (privacy) ambayo ni haki ya msingi kwa binaadamu katika mambo mema.



(ii)Hata baada ya kuruhusiwa kuingia katika nyumba za watu,hatutaingia mpaka kwanza tuwatolee salamu waliomo ndani.



(iii)Kama mtu atabisha hodi mara tatu bila ya kuitikiwa, hata kama atakuwa anawasikia watu wakiongea ndani, asiingie bali aondoke aende zake bila kinyongo.



(iv)Iwapo mtu ataitikiwa baada ya kubisha hodi na badala ya kukaribishwa ndani akaambiwa arudi, hanabudi kurudi kwa moyo mkunjufu bila ya manung'uniko yoyote.



(v)Hatuhitajiki kubisha hodi kwenye nyumba zenye kutoa huduma za kijamii kama vile hoteli, maktaba, msikiti, n.k.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 1438

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Kujiepusha na kuua nafsi bila ya Haki

Kuua nafsi bila ya Haki, ni kuiua nafsi isiyo na kosa linalostahiki hukumu ya kifo.

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun

Wanapokujia wanafiki, husema: "Tunashuhudia ya kuwa kwa yakini wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jeraha kwenye ngozi

Posti hii inaonyesha dalili,sababu na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyepata jeraha kwenye ngozi kwa kuingiliwa na kitu Kama mwiba,Pini,sindano n.k

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...