Adabu ya kuingia katika nyumba za watu

Adabu ya kuingia katika nyumba za watu

Enyi mlioamini!

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Adabu ya kuingia katika nyumba za watu

(f) Adabu ya kuingia katika nyumba za watu


Enyi mlioamini! Msiingie nyumba ambazo si nyumba zenu mpaka muombe ruhusa, (mpige hodi) na muwatolee salamu waliomo humo. Hayo ni bora kwenu; huenda mtakumbuka (mkaona ni mazuri haya mnayoambiwa).



Na kama hamtamkuta humo yeyote, basi msiingie mpaka mruhusiwe . na mkiambiwa "Rudini," basi rudini; hili ni takaso kwenu. Na Mwenyezi Mungu Anajua mnayoyaatenda. Si vibaya kwenu kuingia majumba yasiyokaliwa, (yasiyofanywa maskani: kama mahoteli, maktaba), ( bila kupiga hodi), ambamo humo mna manufaa yenu; na Mwenyezi Mungu Anajua mnayoyadhihirisha na mna yoyaficha. (24:27-29)



Kutokana na aya hizi tunajifunza adabu za kuingia katika nyumba za watu kama ifuatavyo:


(i)Hairuhusiwi mtu kuingia nyumba ya mtu bila ya kubisha hodi. Hata kama utaukuta mlango uko wazi, huruhusiwi kuangaza macho ndani. Hivyo wakati wa kubisha hodi unatakiwa uwe pembeni mwa mlango, kiasi kwamba hata kama mlango umefunguliwa usiweze kumuona mtu au vitu vilivyomo ndani. Vile vile hairuhusiwi kubisha hodi kupitia mlango wa uani au madirishani. Hekima ya amri hii ya kubisha hodi, ni kulinda haki ya faragha (privacy) ambayo ni haki ya msingi kwa binaadamu katika mambo mema.



(ii)Hata baada ya kuruhusiwa kuingia katika nyumba za watu,hatutaingia mpaka kwanza tuwatolee salamu waliomo ndani.



(iii)Kama mtu atabisha hodi mara tatu bila ya kuitikiwa, hata kama atakuwa anawasikia watu wakiongea ndani, asiingie bali aondoke aende zake bila kinyongo.



(iv)Iwapo mtu ataitikiwa baada ya kubisha hodi na badala ya kukaribishwa ndani akaambiwa arudi, hanabudi kurudi kwa moyo mkunjufu bila ya manung'uniko yoyote.



(v)Hatuhitajiki kubisha hodi kwenye nyumba zenye kutoa huduma za kijamii kama vile hoteli, maktaba, msikiti, n.k.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1835

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida

Nao husema (kwa maskhara): "Je, tutakapopotea katika ardhi, (tukageuka mchanga) ndio tutarudishwa katika umbo jipya?

Soma Zaidi...
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)
Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)

Nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku
Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij
Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij

Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko.

Soma Zaidi...
Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?
Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?

Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu)

Soma Zaidi...
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun

Wanapokujia wanafiki, husema: "Tunashuhudia ya kuwa kwa yakini wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...