image

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Mu’uminuun (23:1-11)

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Mu’uminuun (23:1-11)

3. Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Mu’uminuun (23:1-11)



Pia sifa za Waumini zinabainishwa katika Suratul-Muuminuun katika aya zifuatazo:


Hakika wamefuzu waumini ambao katika swala zao huwa wanyenyekevu. (23:1-2)


Na ambao hujiepusha na Lagh-wi (mambo ya upuuzi). Na ambao (nguzo ya) Zaka wanaitekeleza. (23:3-4)



Na ambao tupu zao wanazihifadhi isipokuwa kwa wake zao au kwa (wanawake) wale iliyomiliki mikono yao ya kuume. Basi hao ndio wasiolaumiwa. (23:5-6)


Lakini anayetaka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka. Na ambao amana zao na ahadi zao wanaziangalia. (23: 7-8).


Na ambao swala zao wanazihifadhi. Hao ndio warithi. (23:9-10)


Ambao watarithi Firdaus (Pepo ya daraja ya juu wakae humo milele. (23:11)



Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa, waumini wa kweli waliofuzu na watakaostahiki kupata Pepo ya Firdaus, (ya daraja ya juu kabisa) ni wale wanaojipamba na sifa zifuatazo:



(i)Wenye Khushui katika Swala
Waumini wa kweli waliofuzu huwa na khushui (unyenyekevu) katika swala. Yaani huswali kwa kutulizana kimwili, kimoyo na kifikra, huku wakizingatia yale wayasemayo mbele ya Mola wao wakiwa na yakini kuwa anawaona na anawasikia.



(ii)Wenye Kuhifadhi Swala
Waumini wa kweli waliofuzu huhifadhi swala kwa kutekeleza kwa ukamilifu sharti zote za swala, nguzo zote za swala na huswali kama alivyoswali Mtume (s.a.w) na hudumu na swala katika maisha yao yote. (Qur-an 70:23)



Zingatio:
Swala husimama kwa kuhifadhiwa na kuswaliwa kwa khushui na kudumu na swala katika maisha yote.


(iii) Wenye kuepuka Lagh-wi
Waumini wa kweli waliofuzu hujiepusha na Lagh-wi. Laghwi ni mambo ya upuuzi yanayomsahaulisha mtu kumkumbuka Mola wake, yanayosababisha ugomvi au bughudha baina ya watu na yanayomsahaulisha mtu kuswali (Qur-an 5:91). Mahala ambapo Allah (s.w) hakumbukwi, shetani huchukua nafasi. michezo yote ni lagh-wi isipokuwa ile tu inayochezwa kwa kuchunga mipaka yote ya Allah (s.w) kwa lengo la kukuza ukakamavu na siha ili kuwa imara katika kusimamisha Uislamu katika jamii.



(iv)Hutoa Zakat na Sadakat
Waumini wa kweli waliofuzu hutoa Zakati wakiwa na mali na hutoa misaada na huduma waziwezazo kwa wanaadamu wenziwe kwa kadiri ya haja ilivyojitokeza. Asiyejali binaadamu wenzake, huku ana uwezo si Muumini. Rejea Qur-an (107:1-3).



(v)Wenye kujiepusha na Zinaa na Tabia za Kizinifu.
Waumini wa kweli waliofuzu hujihifadhi na zinaa au hujiepusha kufanya jimai nje ya mipaka aliyoiweka Allah (s.w). Hatua ya kwanza ya kujilinda na zinaa ni kujiepusha na vishawishi vyote vinavyokurubisha watu kwenye zinaa. Muumini wa kweli hutekeleza pasina kusita ile amri ya Allah (s.w) ya katazo kuwa:


Wala usiikaribie zinaa; kwa hakika huo ni uchafu na ni njia mbaya kabisa. (17:32)



(vi)Huwa Muaminifu
Waumini wa kweli waliofuzu huchunga amana. Hutunza amana aliyopewa na kuirejesha au kuitumia kwa mujibu wa maelekezo ya mwenyewe. Amana kuu aliyopewa mwanaadamu na Mola wake ni kule kufadhilishwa kwake kuliko viumbe vingine vyote (Qur-an (17:70),(95:4) ili asimamishe Ukhalifa (utawala wa Allah) katika ardhi kama tunavyokumbushwa katika Qur-an:


"Kwa yakini Sisi tulidhihirisha amana kwa mbingu, ardhi na milima, vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini mwanaadamu aliichukua. Bila shaka yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana." (33:72)



(vii)Wenye Kutekeleza Ahadi
Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.w). Ahadi kubwa wanayotoa Waislamu mbele ya Allah (s.w) ni Shahada; pale wanapoahidi kuwa hawatamshirikisha Allah (s.w) na chochote na kwamba wataishi maisha yao yote kwa kufuata mwongozo wa Allah (s.w) kupitia kwa Mtume wake, Muhammad (s.a.w).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 331


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Ni haramu kwa Waumini kuwaoa au kuolewa na Wazinifu, Washirikina na Mahabithi
Soma Zaidi...

Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.
Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu. Soma Zaidi...

Mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu
Ni upi mgawanyo sahihi wa elimu katika uislamu? Nini naana ya elimu ya muongizo. Je elimu ya mazingiravmaana yakeni nini. Ni upi utofauti wa elimu ya muongozo na elimu ya mazingira? Soma Zaidi...

Lengo la kuletwa mitume
Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:“Kwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere.. Soma Zaidi...

Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?
Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake. Soma Zaidi...

Mambo ya lazima kufanyiwa maiti ya muislamu
Mambo ya faradhi kuhusu maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Njia ambazo Allah hufundisha wanadamu elimu mbalimbali
Ni kipi chanzo cha Elimu, na ni kwa namna gani Allah hufundisha Elimu kwa wanadamu? Soma Zaidi...

Himizo la kuwasamehe waliotukosea
“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita). Soma Zaidi...

Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).
Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s. Soma Zaidi...

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu
Faradhi kwa maiti ya muislamu (edk form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia
Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s. Soma Zaidi...

KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...