image

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Mu’uminuun (23:1-11)

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Mu’uminuun (23:1-11)

3. Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Mu’uminuun (23:1-11)



Pia sifa za Waumini zinabainishwa katika Suratul-Muuminuun katika aya zifuatazo:


Hakika wamefuzu waumini ambao katika swala zao huwa wanyenyekevu. (23:1-2)


Na ambao hujiepusha na Lagh-wi (mambo ya upuuzi). Na ambao (nguzo ya) Zaka wanaitekeleza. (23:3-4)



Na ambao tupu zao wanazihifadhi isipokuwa kwa wake zao au kwa (wanawake) wale iliyomiliki mikono yao ya kuume. Basi hao ndio wasiolaumiwa. (23:5-6)


Lakini anayetaka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka. Na ambao amana zao na ahadi zao wanaziangalia. (23: 7-8).


Na ambao swala zao wanazihifadhi. Hao ndio warithi. (23:9-10)


Ambao watarithi Firdaus (Pepo ya daraja ya juu wakae humo milele. (23:11)



Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa, waumini wa kweli waliofuzu na watakaostahiki kupata Pepo ya Firdaus, (ya daraja ya juu kabisa) ni wale wanaojipamba na sifa zifuatazo:



(i)Wenye Khushui katika Swala
Waumini wa kweli waliofuzu huwa na khushui (unyenyekevu) katika swala. Yaani huswali kwa kutulizana kimwili, kimoyo na kifikra, huku wakizingatia yale wayasemayo mbele ya Mola wao wakiwa na yakini kuwa anawaona na anawasikia.



(ii)Wenye Kuhifadhi Swala
Waumini wa kweli waliofuzu huhifadhi swala kwa kutekeleza kwa ukamilifu sharti zote za swala, nguzo zote za swala na huswali kama alivyoswali Mtume (s.a.w) na hudumu na swala katika maisha yao yote. (Qur-an 70:23)



Zingatio:
Swala husimama kwa kuhifadhiwa na kuswaliwa kwa khushui na kudumu na swala katika maisha yote.


(iii) Wenye kuepuka Lagh-wi
Waumini wa kweli waliofuzu hujiepusha na Lagh-wi. Laghwi ni mambo ya upuuzi yanayomsahaulisha mtu kumkumbuka Mola wake, yanayosababisha ugomvi au bughudha baina ya watu na yanayomsahaulisha mtu kuswali (Qur-an 5:91). Mahala ambapo Allah (s.w) hakumbukwi, shetani huchukua nafasi. michezo yote ni lagh-wi isipokuwa ile tu inayochezwa kwa kuchunga mipaka yote ya Allah (s.w) kwa lengo la kukuza ukakamavu na siha ili kuwa imara katika kusimamisha Uislamu katika jamii.



(iv)Hutoa Zakat na Sadakat
Waumini wa kweli waliofuzu hutoa Zakati wakiwa na mali na hutoa misaada na huduma waziwezazo kwa wanaadamu wenziwe kwa kadiri ya haja ilivyojitokeza. Asiyejali binaadamu wenzake, huku ana uwezo si Muumini. Rejea Qur-an (107:1-3).



(v)Wenye kujiepusha na Zinaa na Tabia za Kizinifu.
Waumini wa kweli waliofuzu hujihifadhi na zinaa au hujiepusha kufanya jimai nje ya mipaka aliyoiweka Allah (s.w). Hatua ya kwanza ya kujilinda na zinaa ni kujiepusha na vishawishi vyote vinavyokurubisha watu kwenye zinaa. Muumini wa kweli hutekeleza pasina kusita ile amri ya Allah (s.w) ya katazo kuwa:


Wala usiikaribie zinaa; kwa hakika huo ni uchafu na ni njia mbaya kabisa. (17:32)



(vi)Huwa Muaminifu
Waumini wa kweli waliofuzu huchunga amana. Hutunza amana aliyopewa na kuirejesha au kuitumia kwa mujibu wa maelekezo ya mwenyewe. Amana kuu aliyopewa mwanaadamu na Mola wake ni kule kufadhilishwa kwake kuliko viumbe vingine vyote (Qur-an (17:70),(95:4) ili asimamishe Ukhalifa (utawala wa Allah) katika ardhi kama tunavyokumbushwa katika Qur-an:


"Kwa yakini Sisi tulidhihirisha amana kwa mbingu, ardhi na milima, vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini mwanaadamu aliichukua. Bila shaka yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana." (33:72)



(vii)Wenye Kutekeleza Ahadi
Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.w). Ahadi kubwa wanayotoa Waislamu mbele ya Allah (s.w) ni Shahada; pale wanapoahidi kuwa hawatamshirikisha Allah (s.w) na chochote na kwamba wataishi maisha yao yote kwa kufuata mwongozo wa Allah (s.w) kupitia kwa Mtume wake, Muhammad (s.a.w).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 402


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)
"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu Soma Zaidi...

Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)
Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako? Soma Zaidi...

Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...

DUA YA 1 - 10
1. Soma Zaidi...

Kuwafanyia Wema Wazazi
Allah (s. Soma Zaidi...

Kujiepusha na kula mali ya Yatima
Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6). Soma Zaidi...

Maamrisho ya kushikamana nayo
Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s. Soma Zaidi...

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab
Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa Soma Zaidi...

“Allah (s.w) humwingiza katika rahma zake amtakaye na kumwacha kupotea amtakaye”
Soma Zaidi...

Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake
Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu. Soma Zaidi...

Mitume wa uongo
Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s. Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Ilhamu katika uislamu?
Ilhamu ni moja katika njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu na kuwafundisha mambo mablimbali. Soma Zaidi...