Mtume hakufundishwa quran na Jabir na Yasir

Mtume hakufundishwa quran na Jabir na Yasir

(c)Dai la Kufundishwa na Jabir na Yasir:



Makafiri wengine wanadai kuwa Mtume (s.a.w) alifundishwa na Jabir na Yasir waliokuwa watumwa kutoka Ethiopia (Uhabeshi) na wakasilimu mbele ya Mtume (s.a.w). Wanadai hivyo kwa kuwa bwana wao aliyekuwa akiwatesa sana kwa sababu ya kusilimu kwao alikuwa akiwapiga sana na kuwaambia: "Mnamfundisha Muhammad?" na walikuwa wakijibu "Kwa jina la Allah hatumfundishi bali ndiye anayetufundisha na kutuongoza".



Bila ya kuangalia majibu ya Jabir na Yasir, wameshikilia swali alilouliza bwana wao kuwa ndio ushahidi wao kuwa Mtume (s.a.w) alifundishwa Qur-an na watu hao.
Makafiri wengine wamedai kuwa Mtume (s.a.w) aliiandika Qur-an kwa kusaidiwa na Salman aliyekuwa Mfursi (Persian). Salman alikuwa Mzoroastian kabla ya kuwa Mkristo huko Sham (Syria). Baadaye Salman alisafiri kwenda Madina ambapo alikutana na Mtume (s.a.w) na kusilimu.



Madai haya ni dhaifu kwa sababu mbili. Kwanza, karibu theluthi mbili ya Qur-an ilishuka Makka kabla Mtume (s.a.w) hajahamia Madina ambapo alikutana na Salman. Pili, fasihi ya lugha iliyotumika katika Qur-an ni ya hali ya juu mno kiasi ambacho wanafasihi mashuhuri wa Kiarabu walijaribu kwa miaka mingi kuigiza Qur-an bila ya mafanikio yoyote, itakuwaje Mfursi awe ndiye aliyeiandika?



Madai haya yamerejewa kwenye Qur-an kama tunavyosoma katika aya ifuatayo:



"Na bila shaka tunajua kwamba wanasema:"Yuko mtu anayemfundisha," (lakini) lugha ya yule wanayemuelekezea (kuwa anamfundisha Mtume) ni ya kigeni na hii (lugha iliyotumika katika Qur-an) ni lugha ya Kiarabu fasaha (bulbul)." (16:103)



Madai yote haya pamoja na madai mengine mengi ambayo yamekuwa yakitolewa katika muda wote wa historia tangu ishuke Qur-an mpaka hivi leo, ni madai dhaifu mno ambayo hayana ushahidi wowote wa kiakili au wa kihistoria kuwa mwandishi (mtunzi) wa Qur-an ni mwengine asiye kuwa Allah (s.w).



Historia ya Mtume (s.a.w) imeandikwa na kuhifadhiwa vema kuliko historia ya mtu yeyote ulimwenguni, lakini hatuoni katika historia hiyo mahali popote tunapofahamishwa kuwa alikaa kitako kwa mtu yeyote kujifunza chochote. Kwani kama Muhammad (s.a.w) angelikuwa amesoma kwa Makasisi na Mapadri wa Kiyahudi na Kikristo au kwa mtu yeyote yafuatayo yangelijitokeza.



(a)Muhammad (s.a.w) hangelificha kueleza hayo kwani alikuwa mashuhuri katika maisha yake yote kwa kuhubiri na kusema ukweli. Aliitwa As-swadiq - Mkweli.
Ndani ya Qur-an yenyewe yamezungumzwa mambo yake ya ndani lakini bado hakuyaficha bali aliyadhihirisha kama yalivyo.



(b)Hangelifundisha imani iliyo tofautiana sana na Ukristo na Uyahudi hasa kuhusu misingi ya dini hizo. Lakini imani ya Kiislamu ni mbali na ni kinyume kabisa na imani ya Kikristo na Kiyahudi.


(c)Yeyote yule aliyemfundisha angeliweza kuandika kitabu mfano wa Qur-an angalau sura moja. Lakini hakutokea mtu yeyote mwenye uwezo huo.



(d)Mayahudi ambao katika Qur-an wameitwa "Ahlul-Kitaabi" au wana wa Israil (Bani Israil) wamekuwa katika muda wote wa utume wake wakimhoji-hoji Mtume Muhammad (s.a.w) na kumcheza shere na walikuwa wakimficha Mtume vitabu vyao. Kunawezekanaje watu hawa kama ndio waliomfundisha Mtume Qur-an wawe wanamhoji hoji tena juu ya Qur-an? Kama wangalikuwa wamemfundisha Mtume chochote, kwa nini wasingelikuwa watu wa kwanza kutangaza kwa watu kuwa wao ndio waliomfundisha ili kuonesha uongo wa utume wake?



(e)Mtume Muhammad (s.a.w) asingelikuwa mkweli katika utume wake na mwaminifu katika kutoa ujumbe aliotumwa autowe kwa watu, wafuasi wake wasingelikuwa wanyenyekevu kwake kiasi hicho na wasingelijizatiti katika kusimamisha mafundisho yake kiasi hicho katika mazingira magumu ya kufa na kupona. Historia inaonesha kuwa Waumini waliomfuata hawakumsaliti hata chembe.



Qur-an Inasadikisha Ukweli:
Sifa ya Qur-an ni kuwa inasadikisha yaliyo ya kweli katika vitabu vilivyopita. Hivyo Muislamu anaweza kujua kwa urahisi kabisa lipi ni sahihi katika Biblia na lipi si sahihi. Lolote lililomo katika vitabu vilivyotangulia ambalo linawafikiana na Qur-an ni sahihi. Na lolote linalokwenda kinyume na Qur-an ni batili.



Jambo la kusisitiza hapa ni kuwa kuhusu vitabu vilivyotangulia Qur-an imevitaja kuwa ni Suhf, Zabur, Taurat na Injili. Muislamu anayevikana vitabu hivi katika asili yake anakoma kuwa Muislamu.


Kama tulivyokwishasema Biblia inavyo kwa uchache vitabu 66. Agano la Kale lina vitabu 39 na Jipya inavyo 27. Katika vile 39 vya Agano la Kale ni vitano tu ndivyo vinavyoitwa Taurati ya Musa.



Qur-an inapotaja Taurati haikusudii Biblia au vitabu 39 vya Agano la Kale wala hivyo vitano vinavyodaiwa kuwa viliandikwa na Musa. Qur-an imeitaja Taurati kama ni ufunuo kutoka kwa Allah. Lakini tunaona kitabu cha Mwanzo ambacho kina taarifa za zamani sana kabla ya yeye (Musa) kuzaliwa. Hatuna uhakika kama kitabu hicho cha Mwanzo ilikuwa ni sehemu ya ufunuo alioupata kwenye mlima Sinai.



Isitoshe nusu ya kitabu cha Kutoka inazungumzia habari za kutoka kwa Wayahudi Misri. Hayo pia yalitokea kabla ya Musa kupata Taurati. Kitabu cha Kumbukumbu la Torati ambacho inadaiwa kiliandikwa na Musa kimeandikwa pia habari za kufariki kwa Musa:



Basi Musa, mtumishi wa BWANA, akafa huko, katika nchi ya Moabu, kukabili Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo. Musa alikuwa mtu wa miaka mia na ishirini alipokufa; jicho lake halikupofuka, wala nguvu za mwili wake hazikupunguka. Wana wa Israeli wakamwombolezea Musa katika uwanda wa Moabu siku thelathini; basi siku za maombolezo ya matanga ya Musa zikaisha. (Kumbukumbu la Torati 34:4-1 2)



Ni dhahiri kuwa upo wasiwasi kama Nabii Musa (a.s) ndiye mwandishi wa kitabu hiki kwa sababu asingeweza kusimulia habari ya kifo chake na matanga yake mwenyewe.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1538

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

HUKUMU ZA QALQALA

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?

Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo

Soma Zaidi...
Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid

Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu.

Soma Zaidi...
Adabu za kusikiliza quran

ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA IDGHAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka suratul al-quraysh na fadhila zake

SURAT AL-QURAYSH Sura hii ina majina mawili.

Soma Zaidi...
Asbab nuzul surat at Tin, Sababu za kushuka surat at Tin (watin wazaitun)

Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun).

Soma Zaidi...
Maswali yanayohusu quran

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...