Mazingatio kabla ya kuosha maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
- Baada ya kufanyiwa hatua hizo, sasa ni lazima maiti kufanyiwa yafuatayo:
- Mambo haya ni faradh Kifaya, wakifanya wachache wanawakilisha wengine.
- Kuoshwa (Kukoshwa).
- Mazingatio kabla ya kuosha maiti.
- Maiti ya kiume ioshwe na wanaume na maiti ya kike ioshwe na wanawake pia.
- Maiti ya mtoto yaweza kuoshwa na yeyote.
- Ni Sunnah mke kumuosha mumewe na mume kumuosha mkewe pia
- Ni mtu mmoja tu ndiye anayeosha na mwingine ni kwa ajili ya kumpa msaada inapobidi.
- Ni muhimu muoshaji afahamu masharti ya kuosha maiti muislamu kama vile;
- Muoshaji awe muislamu.
- Mahali pakuoshea pawe faragha (pamesitirika).
- Maiti aoshwe huku amefunikwa gubi-gubi na nguo nyepesi inayoruhusu maji kupenya kwa urahisi.
- Ni vyema muoshaji asiishike maiti bali aoshe akiwa amevaa ‘gloves’.
- Kuzingatia masharti ya mwenye kuoga josho la wajibu; kama vile kuwa na maji mengi na safi, pasiwe na kizuizi cha maji kupenya, n.k.
- Ni muhimu muoshaji afahamu nguzo na sunnah za kuosha maiti kama ifuatavyo;
- Nguzo za kuosha maiti ni mbili:
- Nia
- Kueneza maji mwili mzima wa maiti.
- Ni Sunnah kumuosha maiti mara tatu au zaidi kwa idadi ya witiri.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 ai web app 👉5 web hosting 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 ai web app 👉5 web hosting 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?
Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.
Soma Zaidi...Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini
Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake
Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.
Soma Zaidi...Kwa nini uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza
Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.
Soma Zaidi...