Python somo la 33: Jinsi ya kupata taarifa za faili
Katika somo hili utakwend akujifunz anamna ya kuwez akupata taarifa zinazohusu faili
Jinsi ya Kupata Taarifa za Faili Husika kwa Python
Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kupata taarifa muhimu kuhusu faili kwa kutumia Python. Tutatumia modules zinazohusiana na os na os.path kwa taarifa za ukubwa, location, na pia tutaongeza ujuzi wa kusoma idadi ya mistari kwa kutumia mbinu tofauti.
1. Hatua za Kwanza
-
Hakikisha faili lako lipo, na unajua jina na path yake.
-
Tunaweza kutumia Python standard library kufanya kazi hizi bila haja ya programu za ziada.
2. Kutambua Ukubwa wa Faili
Ili kujua ukubwa wa faili katika bytes, tunatumia method ya os.path.getsize().
import os
# Jina la faili
file_path = 'wanafunzi.csv'
# Pata ukubwa wa faili
file_size = os.path.getsize(file_path)
print(f"Ukubwa wa faili ni: {file_size} bytes")
Output (mfano):
Ukubwa wa faili ni: 68 bytes
3. Kupata Mahali (Location) ya Faili
Ili kupata absolute path ya faili, tumia os.path.abspath().
import os
# Jina la faili
file_path = 'wanafunzi.csv'
# Pata ukubwa wa faili
file_location = os.path.abspath(file_path)
print(f"Faili lipo katika: {file_location}")
Output (mfano):
Faili lipo katika: /home/user/projects/wanafunzi.csv
4. Muda Faili Lilipopata Sasisho (modification)
Tumia os.path.getmtime() kupata muda wa mwisho faili liliposasishwa (editing). Taarifa hii itarudiwa kama timestamp ya UNIX ambayo inaweza kubadilishwa kuwa fomati inayosomeka.
import os
import time
# Jina la faili
file_path = 'wanafunzi.csv'
# Muda wa mwisho wa kusasisha
last_modified = os.path.getmtime(file_path)
print(f"Faili lilisasishwa mwisho: {time.ctime(last_modified)}")
Output (mfano):
Faili lilisasishwa mwisho: Tue Dec 3 12:45:00 2024
5. Muda wa Mwisho wa Kutumika
Tumia os.path.getatime() kupata muda wa mwisho faili lilipotumika.
import os
import time
# Jina la faili
file_path = 'wanafunzi.csv'
last_accessed = os.path.getatime(file_path)
print(f"Mara ya mwisho faili lilipotumika: {time.ctime(last_acces...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Python somo la 23: Library kwenye python
Hapa utajifunza maana ya library, kazi zake aina zake na jinsi ya ku install lirary
Soma Zaidi...Python somo la 19: Aina za Function
Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Soma Zaidi...Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function
Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions
Soma Zaidi...Python somo la 56: Kuongeza Data Katika Database kwa Kutumia Django Admin na Django Shell
Katika somo hili tutajifunza njia mbili muhimu za kuongeza data kwenye database katika project yetu ya pybongo (app: menu). Njia hizi ni: Kutumia Django Admin Kutumia Django Shell Utafahamu pia jinsi ya kusajili models kwenye admin, jinsi ya kuingia admin panel, na namna ya kutengeneza entries mpya za MenuItem.
Soma Zaidi...Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif
Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia
Soma Zaidi...Python somo la 25: Sheria za uandishi wa class
Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi
Soma Zaidi...