picha

PYHON - somo la 5: Aina za data list, turple, dictionary na boolean

Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.

AINA ZA DATA KWENYE PYTHON SEHEMU YA PILI

Hapa tutakwenda kujifunza aina nyingine  za data ambazo hutumika kwenye python. Aina hizi zina mfanano kidogo na array lakini ni tofauti. 

  1. List data type

Hii ji aina ya data ambazo huwasilishwa kwa njia ya list yaani orodha. Aina hii ya data inaweza kukusanya data zilizo katika makundu tofautootofauti. Kwa mfano inaweza kuwa na namba tupu, ama hstring tupu amna ikachanganya string, float na namba.

 

Katika aina hii ya data tutatumia mabano ya bracket ambayo ni [] ili kutengeneza list yetu. Kila data moja hutenganisha na nyingine kwa kutumia alama ya koma (,). Jambo la kuzingatia ni kuwa data hizi husomwa kwa kupuata kanuni za array, yaani tunaanza 0. Kw amfano kwenye lista hii [1,2,3,4,5] hapo tukitaka kujuwa 5 ni yangapi tutasema ni ya 3 kwenye orodha kwa kuwa tunahesabu kuanzia sifuri. Kwahiyo orodha hiyo ina data 4 tu na sio 5. Angalia mifano hiyohapo chini:-

 

Mfano 1: kwa namba tupu

a = [1,2,3,4]

print(a)

Hapo itakupa matokeo haya

Mafano 2: kwa string tupu

b = ['Google'"Amazon""Bongoclass" ,"Youtube"]

print(b)

 

Code hizo zitakupa matokeo haya

Mfano wa 3: kwa mchanganyiko

c = [2023, "python", 2011, "java", 16.5]

print(c)

 

Code hizo zitakupa matokeo haya



 

Pia unaweza kuweka list ndani ya list nyingine (nested list). Mfano 

b = ['Google', "Amazon", "Bongoclass" ,"Youtube", ["blog", "web", "app"]]

print(b)

 

Hapo utapata matokeo haya:-

 

Jinsi ya ku display value mahususi ndani ya list data:

Kwa mfano kwenye list hii ['Google', "Amazon" "Bongoclass" "Youtube"] Na  unataka ku display Bongoclass kutoka kwenye hiyo lista hapo. Kwa nza itakupasa kujuwa hiyo bongoclass ni ya ngapi kwenye list. Kumbuka utatakiwa kuhesabu kuanzia 0. Hivyo basi hapo bongoclass itakuwa ni ya 2. Sasa endapo utataka ku display hiyo tu itakubidi utumie hiyo index yake ambayo ni 2.

Mfano:

 b = ['Google'"Amazon""Bongoclass" ,"Youtube"]

print(b[2])

 

Hii itadisplay Bongoclass

    

 

Sasa tuseme kuwa tunataka ku display Bongoclass na Google kwanza tutatakiwa kuzijuwa index namba zao. Kumbuka kuanzia 0. Hivyo kwenye list hiyo Google ina index 0 na Bongoclass ina index 2. Kwa maana hiyo sasa tutatumia index hizo ku display kama tulivyofanya hapo juu

b = ['Google', "Amazon", "Bongoclass" ,"Youtube"]

print(b[2],b[0])

 

Hizo zita display Bongoclass  Google

 

Na endapo utahitaji ku display list iliyo ndani ya list

Hapa utafanya vilevile kwa ja ujuwe index ya hiyo lista. Mfano tuna hii lista 

Hapo list iliyoyopo ndani ya list ina index ya 4. Hivyo tutatumia index ya 4 ku rint hiyo list. Mfano

b = ['Google', "Amazon", "Bongoclass" ,"Youtube", ["blog", "web", "app"]]

print(b[4])

Hiyo itatupatia matokeo haya

 

Na endapo tunataka ku display data maalumu, kwa mfano tunataka ku display app hapo kwanza tutatakiw akujuwa index ya list yote ambayo ni 4 kisha tujuwe index ya hilo neno app kwenye list ndogo ambayo ni 2. Hivyo tutatsena print(b[4][2])

b = ['Google'"Amazon""Bongoclass" ,"Youtube", ["blog""web""app"]]

print(b[4][2])

Ha">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-21 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 753

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 web hosting    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Python somo la 38: Kubadilisha landing page ya Django Framework

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubadili ukurasa wa landing page wa Django na kuweka ukurasa tunaoutaka sisi.

Soma Zaidi...
Python somo la 54: Jinsi ya Kusoma Data Kutoka Database kwenye Django

Katika somo hili tutajifunza namna ya kusoma data kutoka kwenye database kupitia Django ORM, jinsi ya kuzipeleka kwenye view, na jinsi ya kuzionyesha kwenye HTML template.

Soma Zaidi...
Python somo la 42: Template tag

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhsu Template Tag nini na kazi zake. Pia utajifunza sheria za uandishi wake.

Soma Zaidi...
Python somo la 31: Jinsi ya kutengeneza faili na folder

Katika somo hili utajifunz ajinsi ya kutengeneza folda, faili na kuweka data kwneye faili

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 2: Sheria za uandishi wa pyhton yaani syntax za python

Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria na kanuni za kuandika code za python

Soma Zaidi...
Python somo la 14: Jinsi ya kutumia For loop

Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python

Soma Zaidi...
Python somo la 50: database kwneye django

Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model

Soma Zaidi...
Python somo la 26: Sheria za uandishi wa object

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.

Soma Zaidi...
Python somo la 37: Jinsi ya ku install Django na kutengeneza project na app

Katika somo ili utajifunza hatuwa kwa hatuwa za ku install Django, kutengeneza project na kutengeneza app

Soma Zaidi...