PHP somo la 56:class interface na polymorphism kwenye PHP OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya interface na concept ya polymorphism kwenye PHP OOP.
Interface ni nini?
Interface inafanana na abstract na hata ufanyaji kazi wake ila kuna utofauti kadhaa yutakuja kuuona hapo chini. Interface hasa yenewe hasa inarahisisha kwa class zaidi ya moja kufanya kazi sawa. Ikiwa kuna class zaidi ya moja zimetumia interface moja hii huulikana kama polymorphism.
Ili tuweze kutengeneza class yenye interface tutatumia keyword interface na ili kuitumia hiyo class yenye interface tutatumia keyword implement. Angalia mfano hapo chini:-
<?php
Interface gari {
}
class tangazo implements gari {
}
Utaona hapo kuna class mbili, ya kwanza ni gari na ya pili ni tangazo. Sasa class gari ndio ina interface na class tangazo inatumia interface ndio utaona hapo tmetumia keyword implement. Sasa hicho kitendo cha kutumia interface kwenye class nyingine ndio kinaitwa polymorphism.
<?php
Interface gari {
public function jina();
public function speed();
}
class tangazo implements gari {
public function jina() {
echo "Jina la gari ni toyota".'<br>';
}
public function speed(){
echo "speed ni 180 km/h";
}
}
echo "Tunauza gari <br>";
$obj = new tangazo();
$obj->jina();
$obj->speed();
?>
Utofauti kati ya insterface na abstract
- Interface haiwezi kuwa na property ambapo abstract inaweza kuwa
- Method zote za kwenye interface ni public ila kwenye abstract ni protected ama public
- Metod zote kwenye interface ni abstract ijapokuwa hakuna kutumia keyword abstract
- Class inaweza kutumia interface na hata kama itakuwa imerithi kutoka kwenye class nyingine.
Angalia mfano mwingine hapo chini
<?php
interface mnyama
{
public function analiaje();
}
class mbuzi implements mnyama
{
public function analiaje()
{
echo " Meee ";
}
}
class paka implements mnyama
{
public function analiaje()
{
echo " Nyau ";
}
}
class mbwa implements mnyama
{
public function analiaje()
{
echo " wow ";
}
}
$mbuzi = new mbuzi();
$paka = new paka();
$mbwa = new mbw...Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 ai web app 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
PHP somo la 88: Jisnsi ya kutengeneza json data kutoka kwenye database
Katika somo ili utakwenda kujifunz ahatuwa kwa hatuwa jinsi ya kutengeneza json data kutkana na data ambazo zio kwenye database
Soma Zaidi...PHP somo la 82: Content-Disposition
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina ya header inayoitwa Content-Disposition
Soma Zaidi...PHP -somo la 33: Matumizi ya while loop kwenye PHP
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP
Soma Zaidi...PHP somol la 55: PHP Abstract Class na abstract method
Katika somo hili utakwenda kujifunza concept mpya ya abstract class na abstract method kwenye OOP.
Soma Zaidi...PHP - somo la 44: Nini cURL na ni yapi matumizi yake?
Katika somo hilibutajifunza maana ya cURL pamoja na matumini yake
Soma Zaidi...PHP somo la 75: Content-Type Header
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu content-type header.
Soma Zaidi...