PHP somo la 57: class traits kwenye PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance
Traits ni nini?
Miongoni mwa changamoto za inheritance ni kuwa inakuwaga ni moja tu, yaani class haiwezi kurithi kutoka kwenye class zaidi ya moja. Kw alugha rahisi child class haiwezi kurithi kutoka kwenye class zaidi ya moja. Kwenye maisha ya kawaida ni sawa na kusema mtoto hawezi kuwa na mzazi zaidi ya mmoja.
Sasa hapo utaona kuna shida, ni kwa sababu mtoto ana wazazi wawili, lamda kwa Yesu, Adamu na Hawa (Eva) ila tuliobakia tuna wazazi wawili. Ukiachana na hiyo pia mtoto anaweza kuridhi baadhi ya sifa kutoka kwa mababu zake na mabibi kupitia kwa wazazi wake. Sasa concept ya inheritance itatulazimisha mtoto arithi kwa mzazi mmoja tu.
Traits itatuwezesha sasa child class ku inherit kutoka kwa class zaidi ya moja. Hivyo trait itawezesha method moja iweze kutumika kwenye class zaidi ya moja. Na method inaweza kuwa na access modifier yryote ile hata kama hiyo method ni abstract. Traits hutengenezawa kwa kutumia keyword trait
Mfano:
<?php
trait gari {
}
?>
Ili uweze kutumia trait class utatumia key word use
Mfabno:
<?php
trait gari {
public function tangazo() {
echo "Tunauza magari <br>";
}
public function mawasiliano() {
echo "Mawasiliano yetu ni : dukag@gmailcom ";
}
}
class ujumbe {
use gari;
}
class contact {
use gari;
}
$obj = new ujumbe();
$obj->tangazo();
$obj->mawasiliano();
?>
Maelezo zaidi
Hapa ni ufafanuzi wa msimbo wako:
1. Traits (gari na duka):
- Traits ni class inavyoweza kutumika upya katika PHP.
- Trait `gari` ina method moja, `tangazo1`, ambayo inachapisha ujumbe "tunauza gari aina zote."
- Trait `duka` ina method nyingine, `tangazo2`, ambayo inachapisha ujumbe "tunatengeneza gari aina zote."
2. Classes (mauzo na matengenezo):
- Class `mauzo` inatumia trait `gari` kupitia use yaani inachukua sifa na method za trait hiyo.
- Class `matengenezo` inatumia traits zote mbili, `gari` na `duka`, na hivyo inarithi sifa na method zote za hizo traits.
3. Matumizi ya Objects:
- Unajenga object la class `mauzo` na kuita method `tangazo1`, ambayo itachapisha "tunauza gari aina zote."
- Kisha, unajenga object la class `matengenezo` na kuita method `tangazo2`, ambayo itachapisha "tunatengeneza gari aina zote."
Msimbo wako unaonyesha jinsi traits zinavyoweza kutumika kuongeza sifa na method kwa classes mbalimbali bila kubadilisha urithi wa class yenyewe.
Nakuletea mfano mwingie uone jinsi ambavyo class moja inaweza kurithi kutoka class zaidi ya ...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
PHP somo la 67: Project ya CUDE operaton wa utuma OOP na PDO
Katika somo hii utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya CRUDE operation kwa kutumia PDO. crude operation inahusu create, read, update. Delete.
Soma Zaidi...PHP somo la 98: Library za PHP ambazo unaweza kutumia ORM
Somo hili litakwenda kukutajia baadhi ya library za php ambazo hutumika kwa matumizi ya ORM
Soma Zaidi...PHP somo la 77: aina za http redirect
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http redirect header
Soma Zaidi...PHP - somo la 45: Jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP
Katika soko hili takwenda kujufunza jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP. Hii itasaidia kama unataka kutuma OTP yaqni Onetime password
Soma Zaidi...PHP -somo la 31: Matumizi ya include() na require() function kwenye php
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za PHP kama require() na iclude()
Soma Zaidi...PHP - somo la 34: Jinsi ya kutumia do loop, while loop na foreach kwenye PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za loop DO, FOR, FOREACH LOOPS kwenye PHP
Soma Zaidi...