picha

PHP - somo la 29: Jinsi ya kaundika function kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function

PHP FUNCTIONS:

Function ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kwa zaidi ya mara moja. Function zipo katika aina mbi ambazo ni:-

Zile ambazo zimekuja moja kwa moja katika php yenyewe hizi huitwa built in functions

Zile ambazo unaweza kuzitengeneza wewe mwenyewe. Hizi huitwa user defined functions

 

Sifa za Functions:

Huweza kutumika zaidi ya mara moja

Haiload kila page inapoload

Hutumika pale tu itakapoitwa

 

USER DEFINED FUNCTIONS:

Sasa hebu tuone jinsi ya kutengeneza function yako mwenyewe. Ili uweze kufanya hivi itahitajika kutumia kanuni ifuatayo:-

function jina() {

   //weka code hapa

}

 

Jinsi ya kuandika function yako:

Kwanza anza na neno keyword function likifuatiwa na jina la hiyo function. Kwa mfano tunataka function ya kujumlisha namba mbili. Hivyo tutaipa jina la jumlisha. Kwahyo itakuwa kama hivi: function jumlisha kisha utaweka mabano haya (). Pia jina la function halitakiwi lianze na namba au special character. Kama ile ya dola tulioitumia kwenye variable.Baada ya hapo utaweka mabano haya {} ambapo ndani yake ndipo kutakuwa na code za hiyo function.

 

Mfano 1

Function jumlisha(){

Code zinakaa hapa.

}

 

Hebu sasa tuone mfano halisi wa function ya kujumlisha namba mbili:

Mfano 2:

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

?>

Hapo tumeshatengeneza function kwa ajili ya kujumlisha namba mbili. Sasa endappo uta load huo ukurasa hautaonyesha chochote, ni kwa sababu function haionyeshi kitu mpaka iitwe. Ili kuiita hiyo function unatakiwa urudie kuliandika jina lake likifuatiwa na mabano (). Mfano katika code hapo juu utaandakia jumlisha () hapo utakuwa umeiita function na itakupa majibu. Hivyo basi code nzima itakuwa:-

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

jumlisha()

?>

 

 

Jinsi ya kutatua matatizo kwa kutumia PHP function

Chukulia mfano unaandika program ya kuorodhesha majina ya wanafunzi kwa jinsia zao. Sasa una jinsia mbili ya kike na ya kiume. Sasa baada ya kila inapotaja jina la mwanafunzi uandike na jinsia yake. Kwa kutumia function hatutakuwa na haja ya kutaja jinsia kila wakati.

 

Mfano: 3

<?php

function mv() {

   echo "Mvulana <br>";

}

 

function ms() {

   echo "Msichana <br>";

}

 

echo "Juma " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Aisha " . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Baraka " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Neema" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Joharia" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>"

?>

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-18 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 799

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 ai web app    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 web hosting    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

PHP somo la 60: namespace na matumizi yake kwenye PHP

Katika somo hili utakwendakujifunza concept ya namespaces na jinsi inavyosaidi kwenye OOP

Soma Zaidi...
PHP - somo la 10: Jinsi ya kundika condition statement if, ifelse na switch case

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu condition statements if, ifelse na switch case. Hata utajifunza jnsi ya kuziandika na zinavyofanya kazi

Soma Zaidi...
PHP - somo la 41: Jinsi ya kufanya hashing kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsiya kufanya hashing taarifa muhimu kama password. Kufanya hashing kunaongeza usalama wa taarifa za waumiaji kwenye blog yako.

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 8: Jinsi ya kufuta post kwenye database

katika post hii utajifunza jinsi ya kufuta post kwenye database. pia utajifunza jinsi ya kufuta picha kwenye server

Soma Zaidi...
PHP somo la 58: static method kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static method na inavtotumika kwenye OOP

Soma Zaidi...
PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file

Soma Zaidi...
PHP - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza table kwenye database kwa kutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia PHP kutengeneza tabale kwenye database ya mysql .

Soma Zaidi...
PHP somo la 82: Content-Disposition

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina ya header inayoitwa Content-Disposition

Soma Zaidi...
PHP - somo la 44: Nini cURL na ni yapi matumizi yake?

Katika somo hilibutajifunza maana ya cURL pamoja na matumini yake

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula Viazi mbatata

Viazi mbatata ni katika vyakula ambavyo hupatikana karibia dunia yote. Viazi hivi vimekuwa ni lishe kubwa sana. Ila je unajuwa hasa ni faida gani za kiafya hupatikana kwenye viazi hivi?

Soma Zaidi...