Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function
PHP FUNCTIONS:
Function ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kwa zaidi ya mara moja. Function zipo katika aina mbi ambazo ni:-
Zile ambazo zimekuja moja kwa moja katika php yenyewe hizi huitwa built in functions
Zile ambazo unaweza kuzitengeneza wewe mwenyewe. Hizi huitwa user defined functions
Sifa za Functions:
Huweza kutumika zaidi ya mara moja
Haiload kila page inapoload
Hutumika pale tu itakapoitwa
USER DEFINED FUNCTIONS:
Sasa hebu tuone jinsi ya kutengeneza function yako mwenyewe. Ili uweze kufanya hivi itahitajika kutumia kanuni ifuatayo:-
function jina() {
//weka code hapa
}
Jinsi ya kuandika function yako:
Kwanza anza na neno keyword function likifuatiwa na jina la hiyo function. Kwa mfano tunataka function ya kujumlisha namba mbili. Hivyo tutaipa jina la jumlisha. Kwahyo itakuwa kama hivi: function jumlisha kisha utaweka mabano haya (). Pia jina la function halitakiwi lianze na namba au special character. Kama ile ya dola tulioitumia kwenye variable.Baada ya hapo utaweka mabano haya {} ambapo ndani yake ndipo kutakuwa na code za hiyo function.
Mfano 1
Function jumlisha(){
Code zinakaa hapa.
}
Hebu sasa tuone mfano halisi wa function ya kujumlisha namba mbili:
Mfano 2:
<?php
function jumlisha() {
$a = 4;
$b = 5;
$c = $a + $b;
echo "$c";
}
?>
Hapo tumeshatengeneza function kwa ajili ya kujumlisha namba mbili. Sasa endappo uta load huo ukurasa hautaonyesha chochote, ni kwa sababu function haionyeshi kitu mpaka iitwe. Ili kuiita hiyo function unatakiwa urudie kuliandika jina lake likifuatiwa na mabano (). Mfano katika code hapo juu utaandakia jumlisha () hapo utakuwa umeiita function na itakupa majibu. Hivyo basi code nzima itakuwa:-
<?php
function jumlisha() {
$a = 4;
$b = 5;
$c = $a + $b;
echo "$c";
}
jumlisha()
?>
Jinsi ya kutatua matatizo kwa kutumia PHP function
Chukulia mfano unaandika program ya kuorodhesha majina ya wanafunzi kwa jinsia zao. Sasa una jinsia mbili ya kike na ya kiume. Sasa baada ya kila inapotaja jina la mwanafunzi uandike na jinsia yake. Kwa kutumia function hatutakuwa na haja ya kutaja jinsia kila wakati.
Mfano: 3
<?php
function mv() {
echo "Mvulana <br>";
}
function ms() {
echo "Msichana <br>";
}
echo "Juma " . "jinsia "; mv() ; echo "<br>";
echo "Aisha " . "jinsia "; ms() ; echo "<br>";
echo "Baraka " . "jinsia "; mv() ; echo "<br>";
echo "Neema" . "jinsia "; ms() ; echo "<br>";
echo "Joharia" . "jinsia "; ms() ; echo "<br>"
?>
...
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowHApa utakwenda kujifunza sasa namna ya kuzisoma post kutoka kwenye blog
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina ya header inayoitwa Content-Disposition
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu cronjob na matumizi yake kwenye PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutengeneza system ambayo mta atajisajili pamoja na kuchat na watumiaji wengine
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia email() function ya PHP. Hii ni njia rahisi zaidi ya kutuma email. Ila hufanya kazi kwenye hosting.
Soma Zaidi...Katika somo il utajifunza kutuma email kwa watu wengi kwa kutumia PHPMailer. Pia utajifunza jinsi ya kuweka Carbon Copy na Blind Carbon Copy
Soma Zaidi...Katika somo hili utaweza kujifunza ni kwa nambna gani utaweza kutengeneza blog post na kuisoma kwa kutumia data za json
Soma Zaidi...Katika somo hii utakwenda kujifunza aina za http header na server variable. Hapa tutakwenda kuchambuwa mgawanyiko wa httpheader na kazi zake.
Soma Zaidi...katika somo hili utajifunza jinsi ya ku upload multiple file yaani mafaili mengi kwa wakati mmoja kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya sqlite kwa kutumia PHP.
Soma Zaidi...