Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function
PHP FUNCTIONS:
Function ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kwa zaidi ya mara moja. Function zipo katika aina mbi ambazo ni:-
Zile ambazo zimekuja moja kwa moja katika php yenyewe hizi huitwa built in functions
Zile ambazo unaweza kuzitengeneza wewe mwenyewe. Hizi huitwa user defined functions
Sifa za Functions:
Huweza kutumika zaidi ya mara moja
Haiload kila page inapoload
Hutumika pale tu itakapoitwa
USER DEFINED FUNCTIONS:
Sasa hebu tuone jinsi ya kutengeneza function yako mwenyewe. Ili uweze kufanya hivi itahitajika kutumia kanuni ifuatayo:-
function jina() {
//weka code hapa
}
Jinsi ya kuandika function yako:
Kwanza anza na neno keyword function likifuatiwa na jina la hiyo function. Kwa mfano tunataka function ya kujumlisha namba mbili. Hivyo tutaipa jina la jumlisha. Kwahyo itakuwa kama hivi: function jumlisha kisha utaweka mabano haya (). Pia jina la function halitakiwi lianze na namba au special character. Kama ile ya dola tulioitumia kwenye variable.Baada ya hapo utaweka mabano haya {} ambapo ndani yake ndipo kutakuwa na code za hiyo function.
Mfano 1
Function jumlisha(){
Code zinakaa hapa.
}
Hebu sasa tuone mfano halisi wa function ya kujumlisha namba mbili:
Mfano 2:
<?php
function jumlisha() {
$a = 4;
$b = 5;
$c = $a + $b;
echo "$c";
}
?>
Hapo tumeshatengeneza function kwa ajili ya kujumlisha namba mbili. Sasa endappo uta load huo ukurasa hautaonyesha chochote, ni kwa sababu function haionyeshi kitu mpaka iitwe. Ili kuiita hiyo function unatakiwa urudie kuliandika jina lake likifuatiwa na mabano (). Mfano katika code hapo juu utaandakia jumlisha () hapo utakuwa umeiita function na itakupa majibu. Hivyo basi code nzima itakuwa:-
<?php
function jumlisha() {
$a = 4;
$b = 5;
$c = $a + $b;
echo "$c";
}
jumlisha()
?>
Jinsi ya kutatua matatizo kwa kutumia PHP function
Chukulia mfano unaandika program ya kuorodhesha majina ya wanafunzi kwa jinsia zao. Sasa una jinsia mbili ya kike na ya kiume. Sasa baada ya kila inapotaja jina la mwanafunzi uandike na jinsia yake. Kwa kutumia function hatutakuwa na haja ya kutaja jinsia kila wakati.
Mfano: 3
<?php
function mv() {
echo "Mvulana <br>";
}
function ms() {
echo "Msichana <br>";
}
echo "Juma " . "jinsia "; mv() ; echo "<br>";
echo "Aisha " . "jinsia "; ms() ; echo "<br>";
echo "Baraka " . "jinsia "; mv() ; echo "<br>";
echo "Neema" . "jinsia "; ms() ; echo "<br>";
echo "Joharia" . "jinsia "; ms() ; echo "<br>"
?>
...
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya PHP na hapa tunaaza rasmi advanced PHP. tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye PHP. Ni vyema kabla ya kuanza course hii ya advanced PHP uwe una uelewa wa kutosha kuhusu mafunzo yetu ya PHP.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu content-type header.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya interface na concept ya polymorphism kwenye PHP OOP.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cross - Orgn Resource Sharing ama inafupishwa kama CORSE header
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika constant kwenye PHP. Pia utajifunza utofauti wake na variable
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya sqlite kwa kutumia PHP.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kuandika query ndani ya ORM. Hii inakupa uhuru wa kufanya kileunachotaka bila ya kuathiri usalama wa project
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifnza jinsi ya kufanya prepared statement kama njia ya kuzuia sql ingection kwenye PHP blog
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kujusu PHP variable, maana yake na sheria za uandishi wa variable
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia email() function ya PHP. Hii ni njia rahisi zaidi ya kutuma email. Ila hufanya kazi kwenye hosting.
Soma Zaidi...