PHP - somo la 29: Jinsi ya kaundika function kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function

PHP FUNCTIONS:

Function ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kwa zaidi ya mara moja. Function zipo katika aina mbi ambazo ni:-

Zile ambazo zimekuja moja kwa moja katika php yenyewe hizi huitwa built in functions

Zile ambazo unaweza kuzitengeneza wewe mwenyewe. Hizi huitwa user defined functions

 

Sifa za Functions:

Huweza kutumika zaidi ya mara moja

Haiload kila page inapoload

Hutumika pale tu itakapoitwa

 

USER DEFINED FUNCTIONS:

Sasa hebu tuone jinsi ya kutengeneza function yako mwenyewe. Ili uweze kufanya hivi itahitajika kutumia kanuni ifuatayo:-

function jina() {

   //weka code hapa

}

 

Jinsi ya kuandika function yako:

Kwanza anza na neno keyword function likifuatiwa na jina la hiyo function. Kwa mfano tunataka function ya kujumlisha namba mbili. Hivyo tutaipa jina la jumlisha. Kwahyo itakuwa kama hivi: function jumlisha kisha utaweka mabano haya (). Pia jina la function halitakiwi lianze na namba au special character. Kama ile ya dola tulioitumia kwenye variable.Baada ya hapo utaweka mabano haya {} ambapo ndani yake ndipo kutakuwa na code za hiyo function.

 

Mfano 1

Function jumlisha(){

Code zinakaa hapa.

}

 

Hebu sasa tuone mfano halisi wa function ya kujumlisha namba mbili:

Mfano 2:

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

?>

Hapo tumeshatengeneza function kwa ajili ya kujumlisha namba mbili. Sasa endappo uta load huo ukurasa hautaonyesha chochote, ni kwa sababu function haionyeshi kitu mpaka iitwe. Ili kuiita hiyo function unatakiwa urudie kuliandika jina lake likifuatiwa na mabano (). Mfano katika code hapo juu utaandakia jumlisha () hapo utakuwa umeiita function na itakupa majibu. Hivyo basi code nzima itakuwa:-

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

jumlisha()

?>

 

 

Jinsi ya kutatua matatizo kwa kutumia PHP function

Chukulia mfano unaandika program ya kuorodhesha majina ya wanafunzi kwa jinsia zao. Sasa una jinsia mbili ya kike na ya kiume. Sasa baada ya kila inapotaja jina la mwanafunzi uandike na jinsia yake. Kwa kutumia function hatutakuwa na haja ya kutaja jinsia kila wakati.

 

Mfano: 3

<?php

function mv() {

   echo "Mvulana <br>";

}

 

function ms() {

   echo "Msichana <br>";

}

 

echo "Juma " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Aisha " . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Baraka " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Neema" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Joharia" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>"

?>

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 426

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

PHP somo la 71: Jinsi ya kutengeneza PDF kwa kutumia PHP na library ya tcpdf

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku generate PDF automatik kutoka kwenye php code , html, javascript na css.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 38: Jinsi ya ku upload mafaili zaidi ya moja kwa kutumia PHP

katika somo hili utajifunza jinsi ya ku upload multiple file yaani mafaili mengi kwa wakati mmoja kwa kutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 68: Jinsi ya kutuma email kwa kutumia PHPMailer

Katika somo hili utakwenda kujifunza jisniya kutuma email kwa kutumia PHPMailer kwenye project ya PHP. Katika somo hili tutakwend akutuma email kwa kutumia localhost.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 30: Baadhi function za PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ktumia baadhi ya function za php

Soma Zaidi...
PHP somo la 57: class traits kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance

Soma Zaidi...
PHP - somo la 7: Jinsi ya kaundika function yakwako

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe yaani user defined function

Soma Zaidi...
PHP somo la 54: PHP OOP class constant

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 40: Jinsi ya kutumia htaccess file kubadilisha muonekano wa link

Katika somo hili uatakwenda kujifunza jinsi ya kutumia htaccess ili kubadili muonekano wa link ya website ama blog ili kuifanya iwe rafiki zaidi.

Soma Zaidi...
PHP somo la 72: Jinsi ya kuandaa PDF kutoana na data zilizopo kwenye database

hapa utawenda utuma database wa ajl ya utengeneza maudhu ya PDF.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 1: Maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

Soma Zaidi...