picha

PHP - somo la 29: Jinsi ya kaundika function kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function

PHP FUNCTIONS:

Function ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kwa zaidi ya mara moja. Function zipo katika aina mbi ambazo ni:-

Zile ambazo zimekuja moja kwa moja katika php yenyewe hizi huitwa built in functions

Zile ambazo unaweza kuzitengeneza wewe mwenyewe. Hizi huitwa user defined functions

 

Sifa za Functions:

Huweza kutumika zaidi ya mara moja

Haiload kila page inapoload

Hutumika pale tu itakapoitwa

 

USER DEFINED FUNCTIONS:

Sasa hebu tuone jinsi ya kutengeneza function yako mwenyewe. Ili uweze kufanya hivi itahitajika kutumia kanuni ifuatayo:-

function jina() {

   //weka code hapa

}

 

Jinsi ya kuandika function yako:

Kwanza anza na neno keyword function likifuatiwa na jina la hiyo function. Kwa mfano tunataka function ya kujumlisha namba mbili. Hivyo tutaipa jina la jumlisha. Kwahyo itakuwa kama hivi: function jumlisha kisha utaweka mabano haya (). Pia jina la function halitakiwi lianze na namba au special character. Kama ile ya dola tulioitumia kwenye variable.Baada ya hapo utaweka mabano haya {} ambapo ndani yake ndipo kutakuwa na code za hiyo function.

 

Mfano 1

Function jumlisha(){

Code zinakaa hapa.

}

 

Hebu sasa tuone mfano halisi wa function ya kujumlisha namba mbili:

Mfano 2:

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

?>

Hapo tumeshatengeneza function kwa ajili ya kujumlisha namba mbili. Sasa endappo uta load huo ukurasa hautaonyesha chochote, ni kwa sababu function haionyeshi kitu mpaka iitwe. Ili kuiita hiyo function unatakiwa urudie kuliandika jina lake likifuatiwa na mabano (). Mfano katika code hapo juu utaandakia jumlisha () hapo utakuwa umeiita function na itakupa majibu. Hivyo basi code nzima itakuwa:-

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

jumlisha()

?>

 

 

Jinsi ya kutatua matatizo kwa kutumia PHP function

Chukulia mfano unaandika program ya kuorodhesha majina ya wanafunzi kwa jinsia zao. Sasa una jinsia mbili ya kike na ya kiume. Sasa baada ya kila inapotaja jina la mwanafunzi uandike na jinsia yake. Kwa kutumia function hatutakuwa na haja ya kutaja jinsia kila wakati.

 

Mfano: 3

<?php

function mv() {

   echo "Mvulana <br>";

}

 

function ms() {

   echo "Msichana <br>";

}

 

echo "Juma " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Aisha " . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Baraka " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Neema" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Joharia" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>"

?>

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-18 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 789

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 web hosting    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

PHP somo la 76: Aina za cache header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Aina za cache header

Soma Zaidi...
PHP somo la 51: Jinsi ya kutumia consctuct na destruct function

Katika somo hili utakwenda kujifunza kazi na matumizi ya construct function na desctruct function kwenye OOP

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 12: Jinsi ya kutumia prepared statement kwenye kusoma post za blog

Katika somo hili tutakwenda kutumia prepared ststement kwenye ku fetch data kutoka kwenye database.

Soma Zaidi...
PHP somo la 87: Jinsi ya kuangalia error wakati wa ku decode na ku encode json data

Katika somo hili utakwenda kujifunza jisni ya kudhibiti error ambazo zinaweza kutokea wakati wa ku encode na ku decoe json data

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 5: Jinsi ya kuandika code za PHP kwa ajili ya kuweka post kwenye blog

Katika ukurasa huu utakwenda kujifunz jinsi ya kuandika code za php kwa ajili ya kutuma post yetu kwenye blog.

Soma Zaidi...
PHP somo la 75: Content-Type Header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu content-type header.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 11: Jinsi ya kutuma tarifa zilizojazwa kwenye form

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kukusanya taarifa za watumiaji kwa kutumia html form.

Soma Zaidi...
PHP somo la 86: JInsi ya ku decode json yaani kubadili json kuwa php data kama array ana object

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kubadili json data na kuwaphp array ama php object. Kwa ufupi tunakwend aku decode json data kuwa phparray amaobject

Soma Zaidi...
PHP somo la 66: Jinsi ya ku edit data na kufuta kwenye database kwa kutumia PDO

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi jinsi ya ku edit ama ku update data na kuzifuta kwenye database kwa kutumia PDO

Soma Zaidi...
PHP - somo la 26: Jinsi ya kutengeneza system ya ku chat kw akutumia PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutengeneza system ambayo mta atajisajili pamoja na kuchat na watumiaji wengine

Soma Zaidi...