PHP - somo la 29: Jinsi ya kaundika function kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function

PHP FUNCTIONS:

Function ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kwa zaidi ya mara moja. Function zipo katika aina mbi ambazo ni:-

Zile ambazo zimekuja moja kwa moja katika php yenyewe hizi huitwa built in functions

Zile ambazo unaweza kuzitengeneza wewe mwenyewe. Hizi huitwa user defined functions

 

Sifa za Functions:

Huweza kutumika zaidi ya mara moja

Haiload kila page inapoload

Hutumika pale tu itakapoitwa

 

USER DEFINED FUNCTIONS:

Sasa hebu tuone jinsi ya kutengeneza function yako mwenyewe. Ili uweze kufanya hivi itahitajika kutumia kanuni ifuatayo:-

function jina() {

   //weka code hapa

}

 

Jinsi ya kuandika function yako:

Kwanza anza na neno keyword function likifuatiwa na jina la hiyo function. Kwa mfano tunataka function ya kujumlisha namba mbili. Hivyo tutaipa jina la jumlisha. Kwahyo itakuwa kama hivi: function jumlisha kisha utaweka mabano haya (). Pia jina la function halitakiwi lianze na namba au special character. Kama ile ya dola tulioitumia kwenye variable.Baada ya hapo utaweka mabano haya {} ambapo ndani yake ndipo kutakuwa na code za hiyo function.

 

Mfano 1

Function jumlisha(){

Code zinakaa hapa.

}

 

Hebu sasa tuone mfano halisi wa function ya kujumlisha namba mbili:

Mfano 2:

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

?>

Hapo tumeshatengeneza function kwa ajili ya kujumlisha namba mbili. Sasa endappo uta load huo ukurasa hautaonyesha chochote, ni kwa sababu function haionyeshi kitu mpaka iitwe. Ili kuiita hiyo function unatakiwa urudie kuliandika jina lake likifuatiwa na mabano (). Mfano katika code hapo juu utaandakia jumlisha () hapo utakuwa umeiita function na itakupa majibu. Hivyo basi code nzima itakuwa:-

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

jumlisha()

?>

 

 

Jinsi ya kutatua matatizo kwa kutumia PHP function

Chukulia mfano unaandika program ya kuorodhesha majina ya wanafunzi kwa jinsia zao. Sasa una jinsia mbili ya kike na ya kiume. Sasa baada ya kila inapotaja jina la mwanafunzi uandike na jinsia yake. Kwa kutumia function hatutakuwa na haja ya kutaja jinsia kila wakati.

 

Mfano: 3

<?php

function mv() {

   echo "Mvulana <br>";

}

 

function ms() {

   echo "Msichana <br>";

}

 

echo "Juma " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Aisha " . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Baraka " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Neema" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Joharia" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>"

?>

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 618

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

PHP somo la 73: Maana ya http header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http header, maana yake na jinsi ya kusoma taarifa zilizopo kwenye http header.

Soma Zaidi...
PHP somo la 60: namespace na matumizi yake kwenye PHP

Katika somo hili utakwendakujifunza concept ya namespaces na jinsi inavyosaidi kwenye OOP

Soma Zaidi...
PHP somo la 49: utangulizi wa Object Oriented Programming katika PHP

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya PHP na hapa tunaaza rasmi advanced PHP. tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye PHP. Ni vyema kabla ya kuanza course hii ya advanced PHP uwe una uelewa wa kutosha kuhusu mafunzo yetu ya PHP.

Soma Zaidi...
PHP somola 69: jinsi ya kutuma email kwa watu zaidi ya mmoja kwa kutumia PHPMailer

Katika somo il utajifunza kutuma email kwa watu wengi kwa kutumia PHPMailer. Pia utajifunza jinsi ya kuweka Carbon Copy na Blind Carbon Copy

Soma Zaidi...
PHP somo la 86: JInsi ya ku decode json yaani kubadili json kuwa php data kama array ana object

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kubadili json data na kuwaphp array ama php object. Kwa ufupi tunakwend aku decode json data kuwa phparray amaobject

Soma Zaidi...
PHP - somo la 43: Jinsi ya kutuma email kwa kutumia PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia email() function ya PHP. Hii ni njia rahisi zaidi ya kutuma email. Ila hufanya kazi kwenye hosting.

Soma Zaidi...
PHP somo la 92: Jinsi ya kuunganisha php na database ya sqlite

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya sqlite kwa kutumia PHP.

Soma Zaidi...
PHP somo la 98: Library za PHP ambazo unaweza kutumia ORM

Somo hili litakwenda kukutajia baadhi ya library za php ambazo hutumika kwa matumizi ya ORM

Soma Zaidi...
PHP - somo la 16: Jinsi ya kufuta tabale na database kwa kutumia php

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufuta table ya databse kwa kutumia PHP. Pia utajifunza jinsi ya kututa database yeto

Soma Zaidi...
PHP somo la 57: class traits kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance

Soma Zaidi...