Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function
PHP FUNCTIONS:
Function ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kwa zaidi ya mara moja. Function zipo katika aina mbi ambazo ni:-
Zile ambazo zimekuja moja kwa moja katika php yenyewe hizi huitwa built in functions
Zile ambazo unaweza kuzitengeneza wewe mwenyewe. Hizi huitwa user defined functions
Sifa za Functions:
Huweza kutumika zaidi ya mara moja
Haiload kila page inapoload
Hutumika pale tu itakapoitwa
USER DEFINED FUNCTIONS:
Sasa hebu tuone jinsi ya kutengeneza function yako mwenyewe. Ili uweze kufanya hivi itahitajika kutumia kanuni ifuatayo:-
function jina() {
//weka code hapa
}
Jinsi ya kuandika function yako:
Kwanza anza na neno keyword function likifuatiwa na jina la hiyo function. Kwa mfano tunataka function ya kujumlisha namba mbili. Hivyo tutaipa jina la jumlisha. Kwahyo itakuwa kama hivi: function jumlisha kisha utaweka mabano haya (). Pia jina la function halitakiwi lianze na namba au special character. Kama ile ya dola tulioitumia kwenye variable.Baada ya hapo utaweka mabano haya {} ambapo ndani yake ndipo kutakuwa na code za hiyo function.
Mfano 1
Function jumlisha(){
Code zinakaa hapa.
}
Hebu sasa tuone mfano halisi wa function ya kujumlisha namba mbili:
Mfano 2:
<?php
function jumlisha() {
$a = 4;
$b = 5;
$c = $a + $b;
echo "$c";
}
?>
Hapo tumeshatengeneza function kwa ajili ya kujumlisha namba mbili. Sasa endappo uta load huo ukurasa hautaonyesha chochote, ni kwa sababu function haionyeshi kitu mpaka iitwe. Ili kuiita hiyo function unatakiwa urudie kuliandika jina lake likifuatiwa na mabano (). Mfano katika code hapo juu utaandakia jumlisha () hapo utakuwa umeiita function na itakupa majibu. Hivyo basi code nzima itakuwa:-
<?php
function jumlisha() {
$a = 4;
$b = 5;
$c = $a + $b;
echo "$c";
}
jumlisha()
?>
Jinsi ya kutatua matatizo kwa kutumia PHP function
Chukulia mfano unaandika program ya kuorodhesha majina ya wanafunzi kwa jinsia zao. Sasa una jinsia mbili ya kike na ya kiume. Sasa baada ya kila inapotaja jina la mwanafunzi uandike na jinsia yake. Kwa kutumia function hatutakuwa na haja ya kutaja jinsia kila wakati.
Mfano: 3
<?php
function mv() {
echo "Mvulana <br>";
}
function ms() {
echo "Msichana <br>";
}
echo "Juma " . "jinsia "; mv() ; echo "<br>";
echo "Aisha " . "jinsia "; ms() ; echo "<br>";
echo "Baraka " . "jinsia "; mv() ; echo "<br>";
echo "Neema" . "jinsia "; ms() ; echo "<br>";
echo "Joharia" . "jinsia "; ms() ; echo "<br>"
?>
...
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku generate PDF automatik kutoka kwenye php code , html, javascript na css.
Soma Zaidi...katika somo hili utajifunza jinsi ya ku upload multiple file yaani mafaili mengi kwa wakati mmoja kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jisniya kutuma email kwa kutumia PHPMailer kwenye project ya PHP. Katika somo hili tutakwend akutuma email kwa kutumia localhost.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ktumia baadhi ya function za php
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe yaani user defined function
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class.
Soma Zaidi...Katika somo hili uatakwenda kujifunza jinsi ya kutumia htaccess ili kubadili muonekano wa link ya website ama blog ili kuifanya iwe rafiki zaidi.
Soma Zaidi...hapa utawenda utuma database wa ajl ya utengeneza maudhu ya PDF.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi
Soma Zaidi...