PHP - somo la 30: Baadhi function za PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ktumia baadhi ya function za php
BUILT IN FUNCTIONS
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu functions ambazo zimetengenezwa moja kwa moja kutoka kwa watengenezaji wa PHP. Hapa nitakuchagulia baadhi tu ya function ambazo hatukuziona kwenye level 1. Hivyo kama utahitaji kujuwa functions zaidi rudi kwenye PHP level 1.
pi()
Function hii hutumika kwa ajili ya kupata tyhamani ya pi (pai) kwa wale wa hesabu wanaelewa pi ni nini kwenye kutafuta eneo la duara, nusu duara n.k
Mfano 1:
<?php
echo(pi());
?>
min() na max()
Hizi kwa pamoja hutumika kutafuta namba kubwa na ndogo. max() ni kwa ajili ya kutafuta nmab kubwa kwenye orodha ya namba. Na min() kazi yake ni kutafuta namba ndogo kwenye orodha ya namba.
Mfano2:
<?php
echo(min(16, 450, 70, 20, 18, 35) . "<br>");
echo(max(67, 210, 51, 20, -16, -12));
?>
sqrt()
Function hii hutumika katika kutafuta square root ya namba. Wale wa hesabau wanafaham vyema hii function.
Mfano 4
<?php
echo(sqrt(9) . "<br>");
echo(sqrt(50) . "<br>");
echo(sqrt(16) . "<br>");
echo(sqrt(81));
?>
5. rand()
Function hii hutumika kwa ajili ya kutengeneza random namba. Hii inaweza kutumika kama kutengeneza unique id. Japo tutaona function nyinginezo zitakazotumika sawa na hii.
Mfano 5:
<?php
echo(rand());
?>
Sasa endapo kwa mfano unahitaji random namba hizi zitokee katika mpangilio fulani. Kwa mfano unataka random namba ziwe kati ya 18 na 67. Yaani namba ndogo iwe ni 18 na namba kubwa iwe ni 67. Hivyo random namba zicheze humo. Kufanya hivi itakubiidi utumie parameter ndani ya functuin. Kwa mfano kwenye maelezo hayo itakuwa hivi:
Mfano 6:
<?php
echo(rand(18, 67));
?>
6. uniqid()
Function hii hutumika kuzalisha namba ambazo ni unique yaani haziwezi kufanana. Hii ni muhimu katika ktengeneza id za item kwenye database.
Mfano 6:
<?php
echo uniqid();
?>
7. session_start()
Function hii hutumika kwa ajili ya kuanzisha session ama kupata taarifa...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
PHP - somo la 13: Jinsi ya kuunganisha database na website
Katika somo hili utajifunza jinsi ya ku connect database, kwa kutumia php
Soma Zaidi...PHP - somo la 16: Jinsi ya kufuta tabale na database kwa kutumia php
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufuta table ya databse kwa kutumia PHP. Pia utajifunza jinsi ya kututa database yeto
Soma Zaidi...PHP somo la 53: class inheritance kwenye PHP Object Oriented Programming
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class inheritance kwenye object oriented programming.
Soma Zaidi...PHP somo la 54: class constant kwenye php
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class.
Soma Zaidi...PHP somo la 66: Jinsi ya ku edit data na kufuta kwenye database kwa kutumia PDO
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi jinsi ya ku edit ama ku update data na kuzifuta kwenye database kwa kutumia PDO
Soma Zaidi...PHP -somo la 33: Matumizi ya while loop kwenye PHP
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP
Soma Zaidi...