PHP - somo la 25: Jinsi ya kukusanya taarifa kutoka kwenye html form kwa kutumia php

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kukusanya taarifa ambazo watu wamezijaza kwa kutumia fomu ya html. Kisha utajifunza jinsi ya kuzisoma hizo taarifa.

Katika somo hili ninakwenda kukufundisha jinsi ya kukusanya madodoso kwa kutumia html form na PHP. Katika somo hili utakwenda kuongeza data kwenye menu yetu kwa kutumia html form. Kufanya hivi tutatengeneza file la php lenye sehemu kuu 2. Moja ni kwa ajili ya kukusanya taarifa, na nyingine ni kwa ajili ya ku process taarifa na kuziweka kwenye database.

 

Sehemu ya kwanza (HTML FORM)

Kumbuka kuwa tumejifunza kwenye mafunzo ya php level 1 kuwa html form ina sehemu mbalimbali ambazo ni method, action, submit na sehemu ya kuweka data. Method nazo zipo mbili kuna POST na GET. Hizi ni njia ambazo taarifa zako hubebwa kutoka kwenye html form kwenda kwenye code za ku process hizo taarifa na kuziweka kwenye database.

 

Tafadhali rejea mafunzo ya PHP level 1 somo la 10 hadi 12 utajifunza jinsi html firm ilivyo na jinsi inavyokusanya taarifa. Faili tutakalolitengeneza kwenye somo hili litakuwa na sehemu kuu 2 kama nilivyokwisha kukueleza hapo awali.

 

  1. Sehemu ya kwanza: html code

Sehemu hii ni kwa ajili ya kukusanya taarifa kwa kutumia html form. Form yetu itakuwa hivi

<form method="post" action="">

   <input type="hidden" name="add" value="1">

   <label>Name</label><br>

   <input placeholder="Name la menu"  name="name"><br>

   <label>Description</label><br>

   <input placeholder="Inahusu Nini"  name="description"><br>

   <label>Price</label><br>

   <inputtype="number" placeholder="Weka Price "  name="price"><br>

  <input type="submit" value="save">

</form>

 

Kama html form inavyojionesha hapao, Method (njia) itakafotumika kubeba taarifa ni method="post"  na kwakuwa faili letu litajiprocess lenyewe hivyo kwenye action hatuhitaji kuweka chochote kama unavyoona hpo patupu action="" tungeweka link ya faili ambalo lina code za ku process data tutakazo kusanya, ila sisi hatuhitaji  faili lengine.

 

form yetu ina user input 5, yaani taarifa zinazotakiwa kubebwa. 

 <input type="hidden" name="add" value="1">

Hii ni kwa ajili ya kuwezesha utumwaji wa taarifa. Taarifa zote hapa zitachakatwa kwa kuanzia hapa. Nimeipa jina la add name="add" na haiwezi kuonekana wakati wa kujaza.

 

<input placeholder="Name la menu"  name="name">

Hii ni kwa ajili ya kukusanya taarifa zinazohusu jina la menu unayotaka kuweka. Place holder ni sehemu ambay inabeba jina ambalo mtumiaji ataliona nalitamjulisha kuwa kijumba hicho kinahitaji kujaza nini. Usern input hapa imepewa jina la name name="name   

   

Pia  <input type="number" placeholder="Weka Price "  name="price"> hapa utaona kuna kitu kimeongezeka a,bacho ni type="number" type maana yake ni aina unaweza kusema kuwa ni aina gani ya data unahitaji ziweze kuwekwa kwenye hiyo sehemu. hapo kwa kuwa ni price himeamuwa iwe namba. Hivyo hutaruhusiwa kuweka herufi hapo.

 

Mwisho kuna <input type="submit" value="save"> Hii kazi yake ni ku submit, yaani kutuma taarifa, Yaani hiyo ni kama batani, ukiibofya taarifa zinatumwa na kupelekwa kwenye sehemu ambayo kuna code za ku process. Sehemu hii ndio inayotajwa kwenye action.                           

 

  1. sehemu ya pili: php codes

<?php

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = "";

$dbname = "hotel";

 

 

if(isset($_POST["add"])){

   $conn = mysqli_connect($servername, $username, $password, $dbname);

   $name = ($_POST['name']);

   $description = ($_POST['description']);

   $price = ($_POST['price']);

 $sql = "INSERT INTO menu (name, description, price) VALUES ('$name', '$description', '$price')";

   if (mysqli_query($conn, $sql)) {

       echo "Data added";

   } else {

       echo "Error: " . $sql . "<br>" . mysqli_error($conn);

   }

   mysqli_close($conn);

}

 

?>

 

Hapa kuna vitu unatakiwa uvielewe mapema kabla ya kuenda mbele. NItakuchambulia kila part na kazi zake ili kwamba tuwe pamoja.

if">...

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 414

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

PHP somo la 72: Jinsi ya kuandaa PDF kutoana na data zilizopo kwenye database

hapa utawenda utuma database wa ajl ya utengeneza maudhu ya PDF.

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 10: Jinsi ya kufanya sanitization

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufanya sanitization kwenye user input ili kuzuia sql injection kwenye database.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 45: Jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP

Katika soko hili takwenda kujufunza jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP. Hii itasaidia kama unataka kutuma OTP yaqni Onetime password

Soma Zaidi...
PHP - somo la 40: Jinsi ya kutumia htaccess file kubadilisha muonekano wa link

Katika somo hili uatakwenda kujifunza jinsi ya kutumia htaccess ili kubadili muonekano wa link ya website ama blog ili kuifanya iwe rafiki zaidi.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 35: Jinsi ya ku upload mafaili kwa kutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku upload mafaili kwenye server kwa kutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 86: JInsi ya ku decode json yaani kubadili json kuwa php data kama array ana object

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kubadili json data na kuwaphp array ama php object. Kwa ufupi tunakwend aku decode json data kuwa phparray amaobject

Soma Zaidi...
PHP somo la 81: Cross - Orgn Resource Sharing - CORSE header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cross - Orgn Resource Sharing ama inafupishwa kama CORSE header

Soma Zaidi...
PHP - somo la 26: Jinsi ya kutengeneza system ya ku chat kw akutumia PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutengeneza system ambayo mta atajisajili pamoja na kuchat na watumiaji wengine

Soma Zaidi...
Jinsi ya kupata location ya mtu lwa kutumia IP address

Katika post hii utajifunza jinsi ya kupata taarifa muhimu za mtumiaji kw akutumia Ip address yake.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 17: Jinsi ya kuingiza data kwenye database kwa kutumia PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuingiza data kwenye dtabase kwa kutumia PHP.

Soma Zaidi...