image

PHP - somo la 25: Jinsi ya kukusanya taarifa kutoka kwenye html form kwa kutumia php

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kukusanya taarifa ambazo watu wamezijaza kwa kutumia fomu ya html. Kisha utajifunza jinsi ya kuzisoma hizo taarifa.

Katika somo hili ninakwenda kukufundisha jinsi ya kukusanya madodoso kwa kutumia html form na PHP. Katika somo hili utakwenda kuongeza data kwenye menu yetu kwa kutumia html form. Kufanya hivi tutatengeneza file la php lenye sehemu kuu 2. Moja ni kwa ajili ya kukusanya taarifa, na nyingine ni kwa ajili ya ku process taarifa na kuziweka kwenye database.

 

Sehemu ya kwanza (HTML FORM)

Kumbuka kuwa tumejifunza kwenye mafunzo ya php level 1 kuwa html form ina sehemu mbalimbali ambazo ni method, action, submit na sehemu ya kuweka data. Method nazo zipo mbili kuna POST na GET. Hizi ni njia ambazo taarifa zako hubebwa kutoka kwenye html form kwenda kwenye code za ku process hizo taarifa na kuziweka kwenye database.

 

Tafadhali rejea mafunzo ya PHP level 1 somo la 10 hadi 12 utajifunza jinsi html firm ilivyo na jinsi inavyokusanya taarifa. Faili tutakalolitengeneza kwenye somo hili litakuwa na sehemu kuu 2 kama nilivyokwisha kukueleza hapo awali.

 

  1. Sehemu ya kwanza: html code

Sehemu hii ni kwa ajili ya kukusanya taarifa kwa kutumia html form. Form yetu itakuwa hivi

<form method="post" action="">

   <input type="hidden" name="add" value="1">

   <label>Name</label><br>

   <input placeholder="Name la menu"  name="name"><br>

   <label>Description</label><br>

   <input placeholder="Inahusu Nini"  name="description"><br>

   <label>Price</label><br>

   <inputtype="number" placeholder="Weka Price "  name="price"><br>

  <input type="submit" value="save">

</form>

 

Kama html form inavyojionesha hapao, Method (njia) itakafotumika kubeba taarifa ni method="post"  na kwakuwa faili letu litajiprocess lenyewe hivyo kwenye action hatuhitaji kuweka chochote kama unavyoona hpo patupu action="" tungeweka link ya faili ambalo lina code za ku process data tutakazo kusanya, ila sisi hatuhitaji  faili lengine.

 

form yetu ina user input 5, yaani taarifa zinazotakiwa kubebwa. 

 <input type="hidden" name="add" value="1">

Hii ni kwa ajili ya kuwezesha utumwaji wa taarifa. Taarifa zote hapa zitachakatwa kwa kuanzia hapa. Nimeipa jina la add name="add" na haiwezi kuonekana wakati wa kujaza.

 

<input placeholder="Name la menu"  name="name">

Hii ni kwa ajili ya kukusanya taarifa zinazohusu jina la menu unayotaka kuweka. Place holder ni sehemu ambay inabeba jina ambalo mtumiaji ataliona nalitamjulisha kuwa kijumba hicho kinahitaji kujaza nini. Usern input hapa imepewa jina la name name="name   

   

Pia  <input type="number" placeholder="Weka Price "  name="price"> hapa utaona kuna kitu kimeongezeka a,bacho ni type="number" type maana yake ni aina unaweza kusema kuwa ni aina gani ya data unahitaji ziweze kuwekwa kwenye hiyo sehemu. hapo kwa kuwa ni price himeamuwa iwe namba. Hivyo hutaruhusiwa kuweka herufi hapo.

 

Mwisho kuna <input type="submit" value="save"> Hii kazi yake ni ku submit, yaani kutuma taarifa, Yaani hiyo ni kama batani, ukiibofya taarifa zinatumwa na kupelekwa kwenye sehemu ambayo kuna code za ku process. Sehemu hii ndio inayotajwa kwenye action.                           

 

  1. sehemu ya pili: php codes

<?php

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = "";

$dbname = "hotel";

 

 

if(isset($_POST["add"])){

   $conn = mysqli_connect($servername, $username, $password, $dbname);

   $name = ($_POST['name']);

   $description = ($_POST['description']);

   $price = ($_POST['price']);

 $sql = "INSERT INTO menu (name, description, price) VALUES ('$name', '$description', '$price')";

   if (mysqli_query($conn, $sql)) {

       echo "Data added";

   } else {

       echo "Error: " . $sql . "<br>" . mysqli_error($conn);

   }

   mysqli_close($conn);

}

 

?>

 

Hapa kuna vitu unatakiwa uvielewe mapema kabla ya kuenda mbele. NItakuchambulia kila part na kazi zake ili kwamba tuwe pamoja.

if(isset($_POST["add"])){}

">...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 220


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

PHP - somo la 45: Jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP
Katika soko hili takwenda kujufunza jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP. Hii itasaidia kama unataka kutuma OTP yaqni Onetime password Soma Zaidi...

PHP somo la 60: namespace na matumizi yake kwenye PHP
Katika somo hili utakwendakujifunza concept ya namespaces na jinsi inavyosaidi kwenye OOP Soma Zaidi...

PHP somo la 73: Maana ya http header
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http header, maana yake na jinsi ya kusoma taarifa zilizopo kwenye http header. Soma Zaidi...

PHP - somo la 47: Jifunze kuhusu sql injection na kuizuia
Katika somo hili utajwenda kujifunza jinsi ya kuzuia hacking kwenye website yako Soma Zaidi...

PHP BLOG - somo la 7: Jinsi ya kutengeneza ukurasa wa kusoma post kwenye blog
HApa utakwenda kujifunza sasa namna ya kuzisoma post kutoka kwenye blog Soma Zaidi...

PHP somo la 56:class interface na polymorphism kwenye PHP OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya interface na concept ya polymorphism kwenye PHP OOP. Soma Zaidi...

Jinsi ya kupata location ya mtu lwa kutumia IP address
Katika post hii utajifunza jinsi ya kupata taarifa muhimu za mtumiaji kw akutumia Ip address yake. Soma Zaidi...

PHP somo la 67: Project ya CUDE operaton wa utuma OOP na PDO
Katika somo hii utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya CRUDE operation kwa kutumia PDO. crude operation inahusu create, read, update. Delete. Soma Zaidi...

PHP - somo la 4: Aina za data zinazotumika kwenye PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye PHP Soma Zaidi...

PHP BLOG - somo la 12: Jinsi ya kutumia prepared statement kwenye kusoma post za blog
Katika somo hili tutakwenda kutumia prepared ststement kwenye ku fetch data kutoka kwenye database. Soma Zaidi...

PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file Soma Zaidi...

PHP somo la 72: Jinsi ya kuandaa PDF kutoana na data zilizopo kwenye database
hapa utawenda utuma database wa ajl ya utengeneza maudhu ya PDF. Soma Zaidi...