PHP - somo la 25: Jinsi ya kukusanya taarifa kutoka kwenye html form kwa kutumia php
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kukusanya taarifa ambazo watu wamezijaza kwa kutumia fomu ya html. Kisha utajifunza jinsi ya kuzisoma hizo taarifa.
Katika somo hili ninakwenda kukufundisha jinsi ya kukusanya madodoso kwa kutumia html form na PHP. Katika somo hili utakwenda kuongeza data kwenye menu yetu kwa kutumia html form. Kufanya hivi tutatengeneza file la php lenye sehemu kuu 2. Moja ni kwa ajili ya kukusanya taarifa, na nyingine ni kwa ajili ya ku process taarifa na kuziweka kwenye database.
Sehemu ya kwanza (HTML FORM)
Kumbuka kuwa tumejifunza kwenye mafunzo ya php level 1 kuwa html form ina sehemu mbalimbali ambazo ni method, action, submit na sehemu ya kuweka data. Method nazo zipo mbili kuna POST na GET. Hizi ni njia ambazo taarifa zako hubebwa kutoka kwenye html form kwenda kwenye code za ku process hizo taarifa na kuziweka kwenye database.
Tafadhali rejea mafunzo ya PHP level 1 somo la 10 hadi 12 utajifunza jinsi html firm ilivyo na jinsi inavyokusanya taarifa. Faili tutakalolitengeneza kwenye somo hili litakuwa na sehemu kuu 2 kama nilivyokwisha kukueleza hapo awali.
-
Sehemu ya kwanza: html code
Sehemu hii ni kwa ajili ya kukusanya taarifa kwa kutumia html form. Form yetu itakuwa hivi
<form method="post" action="">
<input type="hidden" name="add" value="1">
<label>Name</label><br>
<input placeholder="Name la menu" name="name"><br>
<label>Description</label><br>
<input placeholder="Inahusu Nini" name="description"><br>
<label>Price</label><br>
<inputtype="number" placeholder="Weka Price " name="price"><br>
<input type="submit" value="save">
</form>
Kama html form inavyojionesha hapao, Method (njia) itakafotumika kubeba taarifa ni method="post" na kwakuwa faili letu litajiprocess lenyewe hivyo kwenye action hatuhitaji kuweka chochote kama unavyoona hpo patupu action="" tungeweka link ya faili ambalo lina code za ku process data tutakazo kusanya, ila sisi hatuhitaji faili lengine.
form yetu ina user input 5, yaani taarifa zinazotakiwa kubebwa.
<input type="hidden" name="add" value="1">
Hii ni kwa ajili ya kuwezesha utumwaji wa taarifa. Taarifa zote hapa zitachakatwa kwa kuanzia hapa. Nimeipa jina la add name="add" na haiwezi kuonekana wakati wa kujaza.
<input placeholder="Name la menu" name="name">
Hii ni kwa ajili ya kukusanya taarifa zinazohusu jina la menu unayotaka kuweka. Place holder ni sehemu ambay inabeba jina ambalo mtumiaji ataliona nalitamjulisha kuwa kijumba hicho kinahitaji kujaza nini. Usern input hapa imepewa jina la name name="name
Pia <input type="number" placeholder="Weka Price " name="price"> hapa utaona kuna kitu kimeongezeka a,bacho ni type="number" type maana yake ni aina unaweza kusema kuwa ni aina gani ya data unahitaji ziweze kuwekwa kwenye hiyo sehemu. hapo kwa kuwa ni price himeamuwa iwe namba. Hivyo hutaruhusiwa kuweka herufi hapo.
Mwisho kuna <input type="submit" value="save"> Hii kazi yake ni ku submit, yaani kutuma taarifa, Yaani hiyo ni kama batani, ukiibofya taarifa zinatumwa na kupelekwa kwenye sehemu ambayo kuna code za ku process. Sehemu hii ndio inayotajwa kwenye action.
-
sehemu ya pili: php codes
<?php
$servername = "localhost";
$username = "root";
$password = "";
$dbname = "hotel";
if(isset($_POST["add"])){
$conn = mysqli_connect($servername, $username, $password, $dbname);
$name = ($_POST['name']);
$description = ($_POST['description']);
$price = ($_POST['price']);
$sql = "INSERT INTO menu (name, description, price) VALUES ('$name', '$description', '$price')";
if (mysqli_query($conn, $sql)) {
echo "Data added";
} else {
echo "Error: " . $sql . "<br>" . mysqli_error($conn);
}
mysqli_close($conn);
}
?>
Hapa kuna vitu unatakiwa uvielewe mapema kabla ya kuenda mbele. NItakuchambulia kila part na kazi zake ili kwamba tuwe pamoja.
if(isset($_POST["add"...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
PHP somo la 67: Project ya CUDE operaton wa utuma OOP na PDO
Katika somo hii utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya CRUDE operation kwa kutumia PDO. crude operation inahusu create, read, update. Delete.
Soma Zaidi...PHP - somo la 23: Jinsi ya kutumia condition statement kwenye database kwa kutumia PHP
Katika somo hili utakwenda kuona namna ya kutuia if else kwenye data zilizopo kwenye database kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...PHP - somo la 7: Jinsi ya kaundika function yakwako
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe yaani user defined function
Soma Zaidi...PHP - somo la 21: Jinsi ya kutafuta kitu kwenye database kwa mutumia PHP
Katika somo hili utakwenda kujifundisha jinsi ya kutafuta taarifa maalumu kwenye database kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...PHP - somo la 35: Jinsi ya ku upload mafaili kwa kutumia PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku upload mafaili kwenye server kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...PHP somo la 72: Jinsi ya kuandaa PDF kutoana na data zilizopo kwenye database
hapa utawenda utuma database wa ajl ya utengeneza maudhu ya PDF.
Soma Zaidi...