picha

PHP - somo la 25: Jinsi ya kukusanya taarifa kutoka kwenye html form kwa kutumia php

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kukusanya taarifa ambazo watu wamezijaza kwa kutumia fomu ya html. Kisha utajifunza jinsi ya kuzisoma hizo taarifa.

Katika somo hili ninakwenda kukufundisha jinsi ya kukusanya madodoso kwa kutumia html form na PHP. Katika somo hili utakwenda kuongeza data kwenye menu yetu kwa kutumia html form. Kufanya hivi tutatengeneza file la php lenye sehemu kuu 2. Moja ni kwa ajili ya kukusanya taarifa, na nyingine ni kwa ajili ya ku process taarifa na kuziweka kwenye database.

 

Sehemu ya kwanza (HTML FORM)

Kumbuka kuwa tumejifunza kwenye mafunzo ya php level 1 kuwa html form ina sehemu mbalimbali ambazo ni method, action, submit na sehemu ya kuweka data. Method nazo zipo mbili kuna POST na GET. Hizi ni njia ambazo taarifa zako hubebwa kutoka kwenye html form kwenda kwenye code za ku process hizo taarifa na kuziweka kwenye database.

 

Tafadhali rejea mafunzo ya PHP level 1 somo la 10 hadi 12 utajifunza jinsi html firm ilivyo na jinsi inavyokusanya taarifa. Faili tutakalolitengeneza kwenye somo hili litakuwa na sehemu kuu 2 kama nilivyokwisha kukueleza hapo awali.

 

  1. Sehemu ya kwanza: html code

Sehemu hii ni kwa ajili ya kukusanya taarifa kwa kutumia html form. Form yetu itakuwa hivi

<form method="post" action="">

   <input type="hidden" name="add" value="1">

   <label>Name</label><br>

   <input placeholder="Name la menu"  name="name"><br>

   <label>Description</label><br>

   <input placeholder="Inahusu Nini"  name="description"><br>

   <label>Price</label><br>

   <inputtype="number" placeholder="Weka Price "  name="price"><br>

  <input type="submit" value="save">

</form>

 

Kama html form inavyojionesha hapao, Method (njia) itakafotumika kubeba taarifa ni method="post"  na kwakuwa faili letu litajiprocess lenyewe hivyo kwenye action hatuhitaji kuweka chochote kama unavyoona hpo patupu action="" tungeweka link ya faili ambalo lina code za ku process data tutakazo kusanya, ila sisi hatuhitaji  faili lengine.

 

form yetu ina user input 5, yaani taarifa zinazotakiwa kubebwa. 

 <input type="hidden" name="add" value="1">

Hii ni kwa ajili ya kuwezesha utumwaji wa taarifa. Taarifa zote hapa zitachakatwa kwa kuanzia hapa. Nimeipa jina la add name="add" na haiwezi kuonekana wakati wa kujaza.

 

<input placeholder="Name la menu"  name="name">

Hii ni kwa ajili ya kukusanya taarifa zinazohusu jina la menu unayotaka kuweka. Place holder ni sehemu ambay inabeba jina ambalo mtumiaji ataliona nalitamjulisha kuwa kijumba hicho kinahitaji kujaza nini. Usern input hapa imepewa jina la name name="name   

   

Pia  <input type="number" placeholder="Weka Price "  name="price"> hapa utaona kuna kitu kimeongezeka a,bacho ni type="number" type maana yake ni aina unaweza kusema kuwa ni aina gani ya data unahitaji ziweze kuwekwa kwenye hiyo sehemu. hapo kwa kuwa ni price himeamuwa iwe namba. Hivyo hutaruhusiwa kuweka herufi hapo.

 

Mwisho kuna <input type="submit" value="save"> Hii kazi yake ni ku submit, yaani kutuma taarifa, Yaani hiyo ni kama batani, ukiibofya taarifa zinatumwa na kupelekwa kwenye sehemu ambayo kuna code za ku process. Sehemu hii ndio inayotajwa kwenye action.                           

 

  1. sehemu ya pili: php codes

<?php

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = "";

$dbname = "hotel";

 

 

if(isset($_POST["add"])){

   $conn = mysqli_connect($servername, $username, $password, $dbname);

   $name = ($_POST['name']);

   $description = ($_POST['description']);

   $price = ($_POST['price']);

 $sql = "INSERT INTO menu (name, description, price) VALUES ('$name', '$description', '$price')";

   if (mysqli_query($conn, $sql)) {

       echo "Data added";

   } else {

       echo "Error: " . $sql . "<br>" . mysqli_error($conn);

   }

   mysqli_close($conn);

}

 

?>

 

Hapa kuna vitu unatakiwa uvielewe mapema kabla ya kuenda mbele. NItakuchambulia kila part na kazi zake ili kwamba tuwe pamoja.

if(isset($_POST["add"...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: PHP Main: Masomo File: Download PDF Views 1050

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

PHP somo la 54: class constant kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class.

Soma Zaidi...
PHP somo la 100: Jinsi ya kutumia sql moja kwa moja kwenye ORM ya RedBeanPHP

Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kuandika query ndani ya ORM. Hii inakupa uhuru wa kufanya kileunachotaka bila ya kuathiri usalama wa project

Soma Zaidi...
PHP -somo la 6: Jinsi ya kusoma saa na tarehe kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma muda kama saa na tarehe kwa kutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 77: aina za http redirect

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http redirect header

Soma Zaidi...
PHP - somo la 47: Jifunze kuhusu sql injection na kuizuia

Katika somo hili utajwenda kujifunza jinsi ya kuzuia hacking kwenye website yako

Soma Zaidi...
PHP somo la 92: Jinsi ya kuunganisha php na database ya sqlite

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya sqlite kwa kutumia PHP.

Soma Zaidi...