PHP somo la 50: Jinsi ya kutengeneza CLASS na OBJECT kwenye PHP OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza class na object. Tunakwenda kutumia mfano wetu wa hapo juu kwa ajili ya kukamilisha somo hili.
Kutengeneza class utaanza na kuandika neno class likifuatiwa na jina la hiyo class, ikifuatiwa na mabano mawili, ambapo ndani ya mabano hayo ndio utaweka code za hiyo class.
class gari{
}
Mwanzo utaanza kuandika property za hiyo class. Property itaandikea kwa kuanza na access modifier yake. Mfano property ni jina, modifier ni public. Elewa public maana yake hiyo property inaweza kutumia kwenye hiyo class bila ya kizuizi.
class gari{
public $name;
public $speed;
public $transition;
}
Kinachofuata hapo ni kuweka method (functions) kwa ajili ya ku access hizo property
kama method itawekwa ndani ya class tutatumia $this keyword. Kama itakuwa nje hatutatumia. Sasa Wacha tuanze ya ndani ya class.
Tunaposema ndani ya class tunamanisha ndani ya mabano ya hiyo class Yako.
class gari {
//mwanzo wa class
function set_name($name){
$this->name = $name;
}
function set_speed($speed){
$this->speed = $speed;
}
function set_transition($transition){
$this->transition = $transition;
}
//mwisho wa class
}
Sasa tutakwenda kutengeneza function kwa ajili ya kupata value za Kila object. Function yetu ita return value ya object.
function get_name(){
return $this->name;
}
function get_speed(){
return $this->speed;
}
function get_transition (){
return $this->transition ;
}
Mpaka kufikia hapa tayari tumesha set propert za kila class yetu. ila bado hatujatengeneza object . hivyo sasa hatuwa inayofuata ni kutengeneza object
Object tunaweka nje ya class. Ili kutengeneza object tutatumia new keyword likifuatiwa na jina la class.
$toyota = new gari()
$speed = new gari()
$transition = new gari()
Mpaka kufikia hapo tumesha tengeneza object zeta tatu. Sasa kinachofuata ni kutengeneza method kwa ajili ya ku access hizo object ili kuzipa values. Tunaweza kurahisisha kwa kusema kuwa hatuwa inayofuata ni kuweka value kwenye object kutokana na propert zetu. prperty ni name, speed na transition.
$toyota -> set_name("toyota")
$speed ->set_speed("180")
$transition-> set_transition('manual')
Hapo tayari tumeshaipa Kila object value yake. Hatuwa inayofuata ni matumizi ya hizo object. Kwa mfano ngoja tuangalie value hizo
Code zote hizi hapa:
<?php
class gari{
public $name;
public $speed;
public $transition;
function set_name($name){
$this->name = $name;
}
function set_speed($sp...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file
Soma Zaidi...PHP somo la 87: Jinsi ya kuangalia error wakati wa ku decode na ku encode json data
Katika somo hili utakwenda kujifunza jisni ya kudhibiti error ambazo zinaweza kutokea wakati wa ku encode na ku decoe json data
Soma Zaidi...PHP - somo la 34: Jinsi ya kutumia do loop, while loop na foreach kwenye PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za loop DO, FOR, FOREACH LOOPS kwenye PHP
Soma Zaidi...PHP - somo la 16: Jinsi ya kufuta tabale na database kwa kutumia php
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufuta table ya databse kwa kutumia PHP. Pia utajifunza jinsi ya kututa database yeto
Soma Zaidi...PHP somo la 102: Cron job
atika somo hli tutakwenda kujifunza kuhusu kitu kinachitwa cron job. ni moja ya teknolojia zinazotumika kufanya kazi zinazofanyika automatic
Soma Zaidi...PHP somo la 86: JInsi ya ku decode json yaani kubadili json kuwa php data kama array ana object
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kubadili json data na kuwaphp array ama php object. Kwa ufupi tunakwend aku decode json data kuwa phparray amaobject
Soma Zaidi...