PHP somo la 50: Jinsi ya kutengeneza CLASS na OBJECT kwenye PHP OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza class na object. Tunakwenda kutumia mfano wetu wa hapo juu kwa ajili ya kukamilisha somo hili.
Kutengeneza class utaanza na kuandika neno class likifuatiwa na jina la hiyo class, ikifuatiwa na mabano mawili, ambapo ndani ya mabano hayo ndio utaweka code za hiyo class.
class gari{
}
Mwanzo utaanza kuandika property za hiyo class. Property itaandikea kwa kuanza na access modifier yake. Mfano property ni jina, modifier ni public. Elewa public maana yake hiyo property inaweza kutumia kwenye hiyo class bila ya kizuizi.
class gari{
public $name;
public $speed;
public $transition;
}
Kinachofuata hapo ni kuweka method (functions) kwa ajili ya ku access hizo property
kama method itawekwa ndani ya class tutatumia $this keyword. Kama itakuwa nje hatutatumia. Sasa Wacha tuanze ya ndani ya class.
Tunaposema ndani ya class tunamanisha ndani ya mabano ya hiyo class Yako.
class gari {
//mwanzo wa class
function set_name($name){
$this->name = $name;
}
function set_speed($speed){
$this->speed = $speed;
}
function set_transition($transition){
$this->transition = $transition;
}
//mwisho wa class
}
Sasa tutakwenda kutengeneza function kwa ajili ya kupata value za Kila object. Function yetu ita return value ya object.
function get_name(){
return $this->name;
}
function get_speed(){
return $this->speed;
}
function get_transition (){
return $this->transition ;
}
Mpaka kufikia hapa tayari tumesha set propert za kila class yetu. ila bado hatujatengeneza object . hivyo sasa hatuwa inayofuata ni kutengeneza object
Object tunaweka nje ya class. Ili kutengeneza object tutatumia new keyword likifuatiwa na jina la class.
$toyota = new gari()
$speed = new gari()
$transition = new gari()
Mpaka kufikia hapo tumesha tengeneza object zeta tatu. Sasa kinachofuata ni kutengeneza method kwa ajili ya ku access hizo object ili kuzipa values. Tunaweza kurahisisha kwa kusema kuwa hatuwa inayofuata ni kuweka value kwenye object kutokana na propert zetu. prperty ni name, speed na transition.
$toyota -> set_name("toyota")
$speed ->set_speed("180")
$transition-> set_transition('manual')
Hapo tayari tumeshaipa Kila object value yake. Hatuwa inayofuata ni matumizi ya hizo object. Kwa mfano ngoja tuangalie value hizo
Code zote hizi hapa:
<?php
class gari{
public $name;
public $speed;
public $transition;
function set_name($name){
$this->name = $name;
}
function set_speed($sp...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 web hosting 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
PHP - somo la 18: Jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database kwa kutumia PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database kwa kutumia PHP.
Soma Zaidi...PHP somo la 74: aina za http headerna server variable
Katika somo hii utakwenda kujifunza aina za http header na server variable. Hapa tutakwenda kuchambuwa mgawanyiko wa httpheader na kazi zake.
Soma Zaidi...PHP - somo la 12: Jinsi ya kufanyia kazi taarifa zilizokusanywa kutoka kwa mtumiaji
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia taarifa ambazo zimekusanywa kutoka kwa mtumiaji ili kuweka kutatuwa hoja mbalimbali
Soma Zaidi...PHP - somo la 39: Jinsi ya kutengeneza mafaili na mafolda kwenye server kwa kutumia PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuzungumza na server ili kutengeneza mafaili, mafolda, kufuta na ku edit kwa kutumia PHP.
Soma Zaidi...PHP somo la 81: Cross - Orgn Resource Sharing - CORSE header
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cross - Orgn Resource Sharing ama inafupishwa kama CORSE header
Soma Zaidi...PHP somo la 99: Jinsi ya kutumia ORM kwa kutumia library ya RedBeanPHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza Jinsi ya kutumia ORM kwa kutumia library ya RedBeanPHP
Soma Zaidi...