Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

1.Njia mojawapo ni ile ya kuwapatia wajawazito dawa za kutumia kwa mwezi mzima, dawa hizo ni ferrous sulphate ambayo ina milligram mia mbili na  follic asidi ambayo ina milligram 0.4mg hizi dawa kazi yake ni kuongeza damu kwa wajawazito kwa hiyo ni lazima kwa kila mjamzito kutumia dawa hizi na kuepuka mila na desturi za baadhi ya makabila ambayo yanapingana na matumizi ya dawa hizi.

 

2.Kupima wingi wa damu kwa kila mwanamke ambaye anaanza mahudhurio ya kwanza kwenye kliniki. Kila mjamzito anapogundulika kuwa ana mimba kitu cha kwanza ni kupima wingi wa damu, akikutwa ana upungufu wa damu anapaswa kupewa dawa au kama kiasi ni kidogo mno anaweza kuongezewa damu kwa hiyo ni vizuri mama wajawazito kupima mara kwa mara wingi wa damu.

 

3.Kuelimisha watu kujenga vyoo na kutumia vyoo mara kwa mara ili kuweza kuepuka wadudu wanaosababisha minyoo na pia kutumia dawa za minyoo kama vile Mebendazole na Albendazole kwa wanawake kwa hiyo wajawazito wanapaswa kutumia dawa hizi ili kuweza kuepuka hali ya kupunguza damu mwilini.

 

4. Kujaribu kuzuia magonjwa ambayo yanasababisha  upungufu wa damu kama vile Malaria  na magonjwa mengine kwa hiyo Mama wajawazito wanapaswa kutumia dawa za SP ipasavyo kwa sababu na Malaria nayo usababisha upungufu wa damu.

 

5.Pia akina mama wajawazito wanapaswa kutumia vyakula ambavyo vinaongeza damu kama vile mboga za majani, matunda, vyakula vyenye madini ya chuma kwa kufanya hivyo damu ya mama inaweza kuongezeka kwa kawaida ili Mama ajifungua anapaswa kuwa na damu walau 12ml kwenye mwili.

 

6.Kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelimisha watu kuhusu matumizi ya dawa za kuongeza damu kwa wajawazito na pia wajawazito wanapaswa kutumia mboga za majani na vyakula vyenye madini ya chuma kwa hiyo kwa upande wa makabila ambayo uwakataza wanawake wasitumie baadhi ya vyakula kama vile mboga za majani wanapaswa kuacha tabia hiyo kwa sababu damu ni muhimu kwa wajawazito .

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/02/08/Tuesday - 09:38:06 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 921

Post zifazofanana:-

Kuzaliwa kwa Mtume S.A.W
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w, sehemu ya 5. Hapa utajifunza kuhusu kuzaliwa kwa Mtume. Soma Zaidi...

Huduma ya Kwanza kwa aliyeng'atwa na nyuki
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyuko Soma Zaidi...

Hadithi ya aliyekatwa vidole gumba
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Je kwa mfano mimi nmeupata ukimwi leo na sihitaji kwenda kupima yaaan uanza kujionyesha baada ya muda gani
Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa ukimwi huonekana baada ya muda gani toka kuathirika? Soma Zaidi...

Madhara ya kutotoa huduma kwa Mama anayevuja damu baada ya kujifungua
Posti hii inahusu zaidi Madara ya kutomsaidia mama anayetokwa na damu nyingi baada ya kujifungua. Soma Zaidi...

Utaratibu wa lishe kwa wagonjwa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wagonjwa Soma Zaidi...

Hatua za Kuzuia Maambukizi ya Uvimbe kwenye ovari na mirija ya uzazi
Posti hii inazungumzia kuhusiana na hatua za kujikinga na Maambukizi ya Uvimbe kwenye ovari na kwenye mirija ya uzazi Soma Zaidi...

Jinsi uislamu ulivyokomesha biashara ya utumwa wakati na baada ya mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...

Vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri,kwa sababu siku kwa siku kuna magonjwa mengi yanayotokea kwenye sehemu za siri ila kuna vyanzo mbalimbali ambavyo usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu mbalimbali za siri Soma Zaidi...

Zijue hasara za magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi hasara za magonjwa ya ngono, ni magonjwa yanayoambukizwa kwa kujamiiana bila kutumia kinga. Soma Zaidi...

Je inaweza ukaingia period wakati unaujauzito?
Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi? Soma Zaidi...

Mafunzo ya Computer kwa Kiswahili
Utajifunza na kuelewa hata kama hauna computer kwa muda huo Soma Zaidi...