picha

Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

1.Njia mojawapo ni ile ya kuwapatia wajawazito dawa za kutumia kwa mwezi mzima, dawa hizo ni ferrous sulphate ambayo ina milligram mia mbili na  follic asidi ambayo ina milligram 0.4mg hizi dawa kazi yake ni kuongeza damu kwa wajawazito kwa hiyo ni lazima kwa kila mjamzito kutumia dawa hizi na kuepuka mila na desturi za baadhi ya makabila ambayo yanapingana na matumizi ya dawa hizi.

 

2.Kupima wingi wa damu kwa kila mwanamke ambaye anaanza mahudhurio ya kwanza kwenye kliniki. Kila mjamzito anapogundulika kuwa ana mimba kitu cha kwanza ni kupima wingi wa damu, akikutwa ana upungufu wa damu anapaswa kupewa dawa au kama kiasi ni kidogo mno anaweza kuongezewa damu kwa hiyo ni vizuri mama wajawazito kupima mara kwa mara wingi wa damu.

 

3.Kuelimisha watu kujenga vyoo na kutumia vyoo mara kwa mara ili kuweza kuepuka wadudu wanaosababisha minyoo na pia kutumia dawa za minyoo kama vile Mebendazole na Albendazole kwa wanawake kwa hiyo wajawazito wanapaswa kutumia dawa hizi ili kuweza kuepuka hali ya kupunguza damu mwilini.

 

4. Kujaribu kuzuia magonjwa ambayo yanasababisha  upungufu wa damu kama vile Malaria  na magonjwa mengine kwa hiyo Mama wajawazito wanapaswa kutumia dawa za SP ipasavyo kwa sababu na Malaria nayo usababisha upungufu wa damu.

 

5.Pia akina mama wajawazito wanapaswa kutumia vyakula ambavyo vinaongeza damu kama vile mboga za majani, matunda, vyakula vyenye madini ya chuma kwa kufanya hivyo damu ya mama inaweza kuongezeka kwa kawaida ili Mama ajifungua anapaswa kuwa na damu walau 12ml kwenye mwili.

 

6.Kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelimisha watu kuhusu matumizi ya dawa za kuongeza damu kwa wajawazito na pia wajawazito wanapaswa kutumia mboga za majani na vyakula vyenye madini ya chuma kwa hiyo kwa upande wa makabila ambayo uwakataza wanawake wasitumie baadhi ya vyakula kama vile mboga za majani wanapaswa kuacha tabia hiyo kwa sababu damu ni muhimu kwa wajawazito .

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2362

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 ai web app     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Je tumbo huanza kukua baada ya mda gan?

Ni Swali kila mjamzito anataka kujiuliza hasa akiwa katika mimba ya kwanza. Wengine wanataka kujuwa ni muda gani anujuwe mavazi makubwa. Kama na wewe unataka kujuwa muda ambao tumbo huwa kubwa, endelea kusoma.

Soma Zaidi...
Madhara ya vidonge vya P2

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutumia mara kwa mara vidonge vya P2,

Soma Zaidi...
Kiwango cha juu cha Androgen

Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu fangasi za ukeni

Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.

Soma Zaidi...
Kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito faida na hasara zake

Soma Zaidi...
Dalili za kuharibika kwa mimba

Katika post hii utajifunza ishara na dalili ninazoonyesha kuwa mimba ipo hatarini kutoka ama inaweza kuwa imeshatoka.

Soma Zaidi...