Menu



Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

1.Njia mojawapo ni ile ya kuwapatia wajawazito dawa za kutumia kwa mwezi mzima, dawa hizo ni ferrous sulphate ambayo ina milligram mia mbili na  follic asidi ambayo ina milligram 0.4mg hizi dawa kazi yake ni kuongeza damu kwa wajawazito kwa hiyo ni lazima kwa kila mjamzito kutumia dawa hizi na kuepuka mila na desturi za baadhi ya makabila ambayo yanapingana na matumizi ya dawa hizi.

 

2.Kupima wingi wa damu kwa kila mwanamke ambaye anaanza mahudhurio ya kwanza kwenye kliniki. Kila mjamzito anapogundulika kuwa ana mimba kitu cha kwanza ni kupima wingi wa damu, akikutwa ana upungufu wa damu anapaswa kupewa dawa au kama kiasi ni kidogo mno anaweza kuongezewa damu kwa hiyo ni vizuri mama wajawazito kupima mara kwa mara wingi wa damu.

 

3.Kuelimisha watu kujenga vyoo na kutumia vyoo mara kwa mara ili kuweza kuepuka wadudu wanaosababisha minyoo na pia kutumia dawa za minyoo kama vile Mebendazole na Albendazole kwa wanawake kwa hiyo wajawazito wanapaswa kutumia dawa hizi ili kuweza kuepuka hali ya kupunguza damu mwilini.

 

4. Kujaribu kuzuia magonjwa ambayo yanasababisha  upungufu wa damu kama vile Malaria  na magonjwa mengine kwa hiyo Mama wajawazito wanapaswa kutumia dawa za SP ipasavyo kwa sababu na Malaria nayo usababisha upungufu wa damu.

 

5.Pia akina mama wajawazito wanapaswa kutumia vyakula ambavyo vinaongeza damu kama vile mboga za majani, matunda, vyakula vyenye madini ya chuma kwa kufanya hivyo damu ya mama inaweza kuongezeka kwa kawaida ili Mama ajifungua anapaswa kuwa na damu walau 12ml kwenye mwili.

 

6.Kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelimisha watu kuhusu matumizi ya dawa za kuongeza damu kwa wajawazito na pia wajawazito wanapaswa kutumia mboga za majani na vyakula vyenye madini ya chuma kwa hiyo kwa upande wa makabila ambayo uwakataza wanawake wasitumie baadhi ya vyakula kama vile mboga za majani wanapaswa kuacha tabia hiyo kwa sababu damu ni muhimu kwa wajawazito .

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 1484

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Ni zipi njia za kutatua tatizo la nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukuletea njia za kutatua tatizo la nguvu za kiume

Soma Zaidi...
DARASA LA AFYA NA AFYA YA UZAZI

Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho.

Soma Zaidi...
Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa

Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.

Soma Zaidi...
Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri

Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kutoka.

Post hii inahusu zaidi dalili za mimba kutoka, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mimba zote ambazo utaka kutoka kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Mwanamke anatema mate mara kwa mara je inaweza kuwa ni ujauzito?

Ni kweli kuwa kutema mate mara kwa mara inaweza kuwa ni dlili za ujauzito. Lakini itambulije kuwa pekee sio kithibitishi cha ujauzito.

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa hedhi.

Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke

Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo

Soma Zaidi...
Njia za kupunguza tatizo la kutanuka kwa tezi dume.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo tunaweza kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili la kutanuka kwa tezi dume, kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili kwenye jamii kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...