picha

Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

1.Njia mojawapo ni ile ya kuwapatia wajawazito dawa za kutumia kwa mwezi mzima, dawa hizo ni ferrous sulphate ambayo ina milligram mia mbili na  follic asidi ambayo ina milligram 0.4mg hizi dawa kazi yake ni kuongeza damu kwa wajawazito kwa hiyo ni lazima kwa kila mjamzito kutumia dawa hizi na kuepuka mila na desturi za baadhi ya makabila ambayo yanapingana na matumizi ya dawa hizi.

 

2.Kupima wingi wa damu kwa kila mwanamke ambaye anaanza mahudhurio ya kwanza kwenye kliniki. Kila mjamzito anapogundulika kuwa ana mimba kitu cha kwanza ni kupima wingi wa damu, akikutwa ana upungufu wa damu anapaswa kupewa dawa au kama kiasi ni kidogo mno anaweza kuongezewa damu kwa hiyo ni vizuri mama wajawazito kupima mara kwa mara wingi wa damu.

 

3.Kuelimisha watu kujenga vyoo na kutumia vyoo mara kwa mara ili kuweza kuepuka wadudu wanaosababisha minyoo na pia kutumia dawa za minyoo kama vile Mebendazole na Albendazole kwa wanawake kwa hiyo wajawazito wanapaswa kutumia dawa hizi ili kuweza kuepuka hali ya kupunguza damu mwilini.

 

4. Kujaribu kuzuia magonjwa ambayo yanasababisha  upungufu wa damu kama vile Malaria  na magonjwa mengine kwa hiyo Mama wajawazito wanapaswa kutumia dawa za SP ipasavyo kwa sababu na Malaria nayo usababisha upungufu wa damu.

 

5.Pia akina mama wajawazito wanapaswa kutumia vyakula ambavyo vinaongeza damu kama vile mboga za majani, matunda, vyakula vyenye madini ya chuma kwa kufanya hivyo damu ya mama inaweza kuongezeka kwa kawaida ili Mama ajifungua anapaswa kuwa na damu walau 12ml kwenye mwili.

 

6.Kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelimisha watu kuhusu matumizi ya dawa za kuongeza damu kwa wajawazito na pia wajawazito wanapaswa kutumia mboga za majani na vyakula vyenye madini ya chuma kwa hiyo kwa upande wa makabila ambayo uwakataza wanawake wasitumie baadhi ya vyakula kama vile mboga za majani wanapaswa kuacha tabia hiyo kwa sababu damu ni muhimu kwa wajawazito .

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2528

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Nini husababisha mtoto kukosa maji kabla ya kuzaliwa?

inaweza kutokea kuwa mtoto aliye tumboni akaishiwa maji hata kabla ya kuzaliwa. yes hali hii huweza kuwapata baadhiya watoto.

Soma Zaidi...
Sababu za kuwepo fangasi ukeni

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa Ugonjwa wa fangasi,ni sababu mbalimbali ambazo zinaweza kusababisha fangasi.

Soma Zaidi...
Sababu za wajawazito kupata Bawasili.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinafanya wajawazito kupata ugonjwa wa Bawasili, kwa sababu tatizo hili linawapa wakina mama wajawazito, kwa hiyo tutaona kwa nini wajawazito wanapatwa na tatizo hili sana.

Soma Zaidi...
Kujaa gesi tumboni

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon

Soma Zaidi...
Kiwango cha juu cha Androgen

Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.

Soma Zaidi...
Hatua za ukuwaji was mimba na dalili zake

Somo hili linakwenda kukuletea hatua za ukuaji mimba na dalili zake

Soma Zaidi...