Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.
Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen.
1. Dalili ya kwanza ni tumbo kujaa gesi.
Kwa kawaida tumbo kujaa gesi ni kitu cha Kawaida kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa mbalimbali kwa hiyo ikitokea tumbo likajaa gesi, likakaza au kuvimba ni vizuri kabisa kuwahi hospital kwa ajili ya. Uangalizi zaidi.
2. Kuongezeka uzito wa ghafla.
Kuna wakati mwingine mama anaweza kuongezeka uzito kwa ghafla si kwa sababu ya kwamba ni afya ila ni kwa ajili ya kuwepo kwa ongezeko la homoni ya estrogen.
3. Mabadiliko ya hisia ya mara kwa mara au kwa kitaalamu huitwa mood change
Kuna kawaida Kuna kipindi mtu anahisi kuwa na hasira au kuwa na furaha yaani Kuna mabadiliko mengi kwa mtu utokea kwa hiyo Mama akifikia wakati wa manopause na akaona Dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuwahi hospital kwa matibabu zaidi.
4. Kuwepo kwa wasiwasi na msongo wa mawazo kwa kitaalamu huitwa anxiet.
Kuna kipindi Mama huwa na wasi wasi hata kwa kitu au vitu vidogo kwa kufanya hivyo ni sababu ya homoni kubadilika.
5. Kukosa usingizi.
Kuna wakati mwingine usingizi unakosa kabisa kwa hiyo sio kusema kwamba ni uchawa au vipi ila ni dalili za ongezeko la homoni ya estrogen.
6. Kuwepo kwa vipele vyekundu usoni.
Kuna wakati mwingine mama anakuwa na vipele vyekundu usoni, hali hii haiwatokei watu wengi ila ni kwa akina Mama Wachache.
7. Kuota kwa vinyama kwenye via vya uzazi .
Kuna wakati mwingine kunakuwepo kwa vinyama kwenye via vya uzazi hali hii inatokea lakini si kwa wanawake wengi.
8. Kuvimba kwa maziwa.
Kuna kipindi ambapo Mama anaweza kumaliza miaka mingi amenyonyesha lakini kwa sababu ya kuwepo kwa ongezeko la homoni mwilini usababisha maziwa kuvimba hali ambayo usababisha wasiwasi mwingi kwa akina Mama walio wengi.
9. Utokaji mwingi wa damu wakati wa hedhi kwa kiasi ambacho si kawaida na siku nyingine.
10. Maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara.
Kuna wakati mwingine mama uhisi maumivu ya kichwa yasiyo ya kawaida kila mara hata akitumia dawa hali ni Ile Ile tu.
11. Kupoteza kumbukumbu na kuongezeka kwa uzito.
Kuna wakati mwingine mama anaongezeka Uzito ghafla na kuambatana na kupoteza kumbukumbu .
12. Pamoja na Dalili tulizoziona si kila dalili ni matatizo ya homoni kuongezeka ila ni vizuri kabisa kwenda hospital kwa ajili ya uangalizi zaidi na kupata ushauri wa daktari
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 web hosting 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Je nitahakikisha vipi Kama Nina ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuhakiki Kama u-mjamzito
Soma Zaidi...Dalili za kuziba kwa mirija ya uzazi
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea kwa sababu ya kuziba kwa mishipa ya uzazi, ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kuziba kwa mishipa ya uzazi.
Soma Zaidi...Huduma kwa wasioona hedhi
Posti hii inahusu zaidi msaada au namna ya kuwahudumia wale wasioona hedhi na wamefikiwa kwenye umri wa kuweza kuona hedhi.
Soma Zaidi...dalili za uchungu kwa mama mjamzito
Makala hii itakwenda kukufundisha baadhi ya dalili za uchungu kwa mama mjamzito.
Soma Zaidi...Mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama ananyonyesha
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama anaenyonyesha
Soma Zaidi...Ni ipi hasa siku ambayo nitafute ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kutafuta ujauzito
Soma Zaidi...