Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.
Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen.
1. Dalili ya kwanza ni tumbo kujaa gesi.
Kwa kawaida tumbo kujaa gesi ni kitu cha Kawaida kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa mbalimbali kwa hiyo ikitokea tumbo likajaa gesi, likakaza au kuvimba ni vizuri kabisa kuwahi hospital kwa ajili ya. Uangalizi zaidi.
2. Kuongezeka uzito wa ghafla.
Kuna wakati mwingine mama anaweza kuongezeka uzito kwa ghafla si kwa sababu ya kwamba ni afya ila ni kwa ajili ya kuwepo kwa ongezeko la homoni ya estrogen.
3. Mabadiliko ya hisia ya mara kwa mara au kwa kitaalamu huitwa mood change
Kuna kawaida Kuna kipindi mtu anahisi kuwa na hasira au kuwa na furaha yaani Kuna mabadiliko mengi kwa mtu utokea kwa hiyo Mama akifikia wakati wa manopause na akaona Dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuwahi hospital kwa matibabu zaidi.
4. Kuwepo kwa wasiwasi na msongo wa mawazo kwa kitaalamu huitwa anxiet.
Kuna kipindi Mama huwa na wasi wasi hata kwa kitu au vitu vidogo kwa kufanya hivyo ni sababu ya homoni kubadilika.
5. Kukosa usingizi.
Kuna wakati mwingine usingizi unakosa kabisa kwa hiyo sio kusema kwamba ni uchawa au vipi ila ni dalili za ongezeko la homoni ya estrogen.
6. Kuwepo kwa vipele vyekundu usoni.
Kuna wakati mwingine mama anakuwa na vipele vyekundu usoni, hali hii haiwatokei watu wengi ila ni kwa akina Mama Wachache.
7. Kuota kwa vinyama kwenye via vya uzazi .
Kuna wakati mwingine kunakuwepo kwa vinyama kwenye via vya uzazi hali hii inatokea lakini si kwa wanawake wengi.
8. Kuvimba kwa maziwa.
Kuna kipindi ambapo Mama anaweza kumaliza miaka mingi amenyonyesha lakini kwa sababu ya kuwepo kwa ongezeko la homoni mwilini usababisha maziwa kuvimba hali ambayo usababisha wasiwasi mwingi kwa akina Mama walio wengi.
9. Utokaji mwingi wa damu wakati wa hedhi kwa kiasi ambacho si kawaida na siku nyingine.
10. Maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara.
Kuna wakati mwingine mama uhisi maumivu ya kichwa yasiyo ya kawaida kila mara hata akitumia dawa hali ni Ile Ile tu.
11. Kupoteza kumbukumbu na kuongezeka kwa uzito.
Kuna wakati mwingine mama anaongezeka Uzito ghafla na kuambatana na kupoteza kumbukumbu .
12. Pamoja na Dalili tulizoziona si kila dalili ni matatizo ya homoni kuongezeka ila ni vizuri kabisa kwenda hospital kwa ajili ya uangalizi zaidi na kupata ushauri wa daktari
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 web hosting π3 Dua za Mitume na Manabii π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 ai web app π6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Dalili na sababu za Kukosa hedhi
Post hii inaongelea kuhusiana na Kukosa hedhi ambapo kitaalamu hujulikana Kama Amenorrhea ni kutokuwepo kwa hedhi - hedhi moja au zaidi ya kukosa. Wanawake ambao wamekosa angalau hedhi tatu mfululizo wana amenorrhea, kama vile wasichana ambao hawajaanz
Soma Zaidi...kunauwezekano wa darri ya kchefuchefu ictokee kabsa kwa mjauzito
Kichefuchefu ni moja katika dalili za mimba za mapema, Lucinda je upo uwezekano kwa mwanamke kuwa na ujauzito bila hata ya kuwa na kichefuchefu?
Soma Zaidi...Mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka.
Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusiana na kubalehe kwa msichana na mvulana.
KubaleheΓΒ ni wakati mwili wa mtoto unapoanza kubadilika na kuwa wa mtu mzima (balehe) hivi karibuni. Kubalehe ambao huanza kabla ya umri wa miaka 8 kwa wasichana na kabla ya umri wa miaka 9 kwa wavulana.
Soma Zaidi...Nini husababisha maumivu ya uume
Kama uume wako unauma ama unahisi kuwa unaunguza ama kuchoma choma, post hii imekuandalia somo hili.
Soma Zaidi...Maelekezo muhimu kwa Mama au mlezi wa mtoto mgonjwa
Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto.
Soma Zaidi...