picha

Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.

Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen.

1.  Dalili ya kwanza ni tumbo kujaa gesi.

Kwa kawaida tumbo kujaa gesi ni kitu cha Kawaida kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa mbalimbali kwa hiyo ikitokea tumbo likajaa gesi, likakaza au kuvimba ni vizuri kabisa kuwahi hospital kwa ajili ya. Uangalizi zaidi.

 

2. Kuongezeka uzito wa ghafla.

Kuna wakati mwingine mama anaweza kuongezeka uzito kwa ghafla si kwa sababu ya kwamba ni afya ila ni kwa ajili ya kuwepo kwa ongezeko la homoni ya estrogen.

 

3. Mabadiliko ya hisia ya mara kwa mara au kwa kitaalamu huitwa mood change 

Kuna kawaida  Kuna kipindi mtu anahisi kuwa na hasira au kuwa na furaha yaani Kuna mabadiliko mengi kwa mtu utokea kwa hiyo Mama akifikia wakati wa manopause na akaona Dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuwahi hospital kwa matibabu zaidi.

 

4. Kuwepo kwa wasiwasi na msongo wa mawazo kwa kitaalamu huitwa anxiet.

Kuna kipindi Mama huwa na wasi wasi hata kwa kitu au vitu vidogo kwa kufanya hivyo ni sababu ya homoni kubadilika.

 

5. Kukosa usingizi.

Kuna wakati mwingine usingizi unakosa kabisa kwa hiyo sio kusema kwamba ni uchawa au vipi ila ni dalili za ongezeko la homoni ya estrogen.

 

6. Kuwepo kwa vipele vyekundu usoni.

Kuna wakati mwingine mama anakuwa na vipele vyekundu usoni, hali hii haiwatokei watu wengi ila ni kwa akina Mama Wachache.

 

7. Kuota kwa vinyama kwenye via vya uzazi .

Kuna wakati mwingine kunakuwepo kwa vinyama kwenye via vya uzazi hali hii inatokea lakini si kwa wanawake wengi.

 

8. Kuvimba kwa maziwa.

Kuna kipindi ambapo Mama anaweza kumaliza miaka mingi amenyonyesha lakini kwa sababu ya kuwepo kwa ongezeko la homoni mwilini usababisha maziwa kuvimba hali ambayo usababisha wasiwasi mwingi kwa akina Mama walio wengi.

 

9. Utokaji mwingi wa damu wakati wa hedhi kwa kiasi ambacho si kawaida na siku nyingine.

 

10. Maumivu ya  kichwa ya mara Kwa mara.

Kuna wakati mwingine mama uhisi maumivu ya kichwa yasiyo ya kawaida kila mara hata akitumia dawa hali ni Ile Ile tu.

 

11. Kupoteza kumbukumbu na kuongezeka kwa uzito.

Kuna wakati mwingine mama anaongezeka Uzito ghafla na kuambatana na kupoteza kumbukumbu .

 

12. Pamoja na Dalili tulizoziona si kila dalili ni matatizo ya homoni kuongezeka ila ni vizuri kabisa kwenda hospital kwa ajili ya uangalizi zaidi na kupata ushauri wa daktari

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2751

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app     πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰6 web hosting    

Post zinazofanana:

Mimba huonekana katka mkojo baada ya muda gan tangu itungwe

Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.

Soma Zaidi...
Jinsi mimba inavyotungwa na namna ambavyo jinsia ya mtoto inavyotokea

Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaumeΒ  .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu.

Soma Zaidi...
Mbinu za kupunguza Kichefuchefu

Point hii inahusu zaidi mbinu za kupunguza Kichefuchefu hasa kwa wagonjwa na watumiaji wa madawa mbalimbali yanayoweza kusababisha kichefuchefu.

Soma Zaidi...
Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa.

Soma Zaidi...
Dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.

Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia madawa ya shida ya upumuaji

Post hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya shida ya upumuaji, ni madhara madogo madogo ambayo utokea kwa watumiaji wa matatizo ya kupumua.

Soma Zaidi...