Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.
1. Dalili ya kwanza ni tumbo kujaa gesi.
Kwa kawaida tumbo kujaa gesi ni kitu cha Kawaida kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa mbalimbali kwa hiyo ikitokea tumbo likajaa gesi, likakaza au kuvimba ni vizuri kabisa kuwahi hospital kwa ajili ya. Uangalizi zaidi.
2. Kuongezeka uzito wa ghafla.
Kuna wakati mwingine mama anaweza kuongezeka uzito kwa ghafla si kwa sababu ya kwamba ni afya ila ni kwa ajili ya kuwepo kwa ongezeko la homoni ya estrogen.
3. Mabadiliko ya hisia ya mara kwa mara au kwa kitaalamu huitwa mood change
Kuna kawaida Kuna kipindi mtu anahisi kuwa na hasira au kuwa na furaha yaani Kuna mabadiliko mengi kwa mtu utokea kwa hiyo Mama akifikia wakati wa manopause na akaona Dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuwahi hospital kwa matibabu zaidi.
4. Kuwepo kwa wasiwasi na msongo wa mawazo kwa kitaalamu huitwa anxiet.
Kuna kipindi Mama huwa na wasi wasi hata kwa kitu au vitu vidogo kwa kufanya hivyo ni sababu ya homoni kubadilika.
5. Kukosa usingizi.
Kuna wakati mwingine usingizi unakosa kabisa kwa hiyo sio kusema kwamba ni uchawa au vipi ila ni dalili za ongezeko la homoni ya estrogen.
6. Kuwepo kwa vipele vyekundu usoni.
Kuna wakati mwingine mama anakuwa na vipele vyekundu usoni, hali hii haiwatokei watu wengi ila ni kwa akina Mama Wachache.
7. Kuota kwa vinyama kwenye via vya uzazi .
Kuna wakati mwingine kunakuwepo kwa vinyama kwenye via vya uzazi hali hii inatokea lakini si kwa wanawake wengi.
8. Kuvimba kwa maziwa.
Kuna kipindi ambapo Mama anaweza kumaliza miaka mingi amenyonyesha lakini kwa sababu ya kuwepo kwa ongezeko la homoni mwilini usababisha maziwa kuvimba hali ambayo usababisha wasiwasi mwingi kwa akina Mama walio wengi.
9. Utokaji mwingi wa damu wakati wa hedhi kwa kiasi ambacho si kawaida na siku nyingine.
10. Maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara.
Kuna wakati mwingine mama uhisi maumivu ya kichwa yasiyo ya kawaida kila mara hata akitumia dawa hali ni Ile Ile tu.
11. Kupoteza kumbukumbu na kuongezeka kwa uzito.
Kuna wakati mwingine mama anaongezeka Uzito ghafla na kuambatana na kupoteza kumbukumbu .
12. Pamoja na Dalili tulizoziona si kila dalili ni matatizo ya homoni kuongezeka ila ni vizuri kabisa kwenda hospital kwa ajili ya uangalizi zaidi na kupata ushauri wa daktari
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Je na wewe unasumbuliwa na fangasi wenye uume. Post hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi msaada au namna ya kuwahudumia wale wasioona hedhi na wamefikiwa kwenye umri wa kuweza kuona hedhi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa wanawake, ni sababu ambazo upelekea wanawake wengi kuwa wagumba ukizingatia kuwa wanazaliwa wakiwa na uwezo kabisa wa kupata watoto lakini kwa sababu mbalimbali za kimazingira wanakoswa watoto, zifuatazo ni saba
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi changamoto za kwenye ndoa kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara,hizi ni changamoto za wakati wa kufanya tendo na mme wake au mtu mwingine kwa ajili ya kupata mtoto.
Soma Zaidi...Swali langi ni hiliMama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni?
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa harufu mbaya kwenye uke ukizingatia usafi huwa unafanyika mara kwa mara ila harufu bado inaendelea kuwa mbaya kwa hiyo tutaona sababu hapo chini.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili pamoja na mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua kwa Wanaume
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatua ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kutibu uvimbe au kwa kitaalamu huitwa fibroids. Hizi hatua zikitumika uweza kusaidia kupunguza kiwango cha kupata au kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
Soma Zaidi...