Navigation Menu



Siku za hatari, siku za kubeba mimba

Hizi ni siku hatari kwa mwanamke ambazo ni ahisi kwake kubeba mimba, siku nitakueleza ni zipi na ni zipi sifa zake

Siku za hatari, siku za kubeba mimba

SIKU ZA KATARI NA SIKU ZA KUSHIKA MIMBA.
Kila mwanamke ana siku yake ambayo ni hatari zaidi kushika mimba. Siku hii inaweza kufanana na mwanamke mwingine ambaye anafanana naye mahesabu. Hata hivyo wanaweza kutofautiana kutokana na vyakula, maumbile na hali za maisha. Hapa nitakuletea orodha ya siku hatari za mwanamke.



Nini maana ya siku hatari?
Hizi ni siku ambazo mwanamke anakadiriwa kupata ujauzito. Ni mfululizo wa siku ambazo makadirio ya mwanamke kupata ujauzito ni mkubwa kuliko siku nyingine. Kabla ya kuzijuwa siku hizi kwanza hakikisha unajuwa vyema idadi ya siku mwanamke anazokwenda hedhi. Wanawake wanakwenda hedhi ndani ya mzunguruko unaoanzania siku 21 mpaka 35. hii inamaana kuna am,bao siku zao ni nyingi na wengine ni kidogo.



Sasa ni ipi siku hatari kwa mwanamke, siku ambayo mawanamke atapata ujauzito?. siku hii nitakuorodheshea, ila kwanza nataka tu nikujuze kwa ufupi sifa ya siku hiyo. Kwa nini, ni kwa sababu siku hizi zipo nyingi na zote ni hatari kwani zinaweza kuleta mimba. Ila katika hizo ipo ambayo ni hatari zaidi. Siku hiyo ina sifa hizi:-



1.Mwili wa mwanamke katika siku hii utakuwa na joto kulinganisha na siku zilizopita. Kwa urahisi unaweza kugunduwa kama unatumia kipima joto. Ila ukiwa makini unaweza kujigunduwa kama joto lako limepanda. Hakikisha ongezeko hiki ka joto hakiambatani na shida nyingine za kiafya kama maradhi.



2.Uteute unaopatikana kwenye shingo ya kizazi utakuwa umeongezeka na ni wenye kuteleza kama vile majimajiya yai lililopasuliwa. Kama utaingizakidole ndani zaidi ya uke unaweza kuupata kwenye kidole chako.



3.Siku hii hamu ya kushiriki tendo la ndoa nikubwa kuliko siku yingine. Hii haina haja ya kuielezea. Kama mwanamke homoni zake hazina shida basi lakima kutakuwa na siku ambayo atahitaji sana kushiriki ngono kuliko siku nyingine.



Nitaijuwaje siku hatari, ya kupata mimba?
Kikawaida yai hutolewa (ovulation) kwa makadiria ya siku 12 mpaka 16 kabla ya kupata hedhi nyingine. Yaani unaweza kuhesabu kabla ya kuingia hedhi siku 12 nyuma, kisha toa siku 4 mnyuma ndani ya siku nne zizi ndizo yai hutolewa. siku hizi ndizo moja wapo yai hutolewa. Kwa mfano:--



1.Mwanamke mwenye mzunguko wa siku 21, sasa tunatoa siku 12 nyuma kabla ya kuingia hedhi (21 - 12 = 9) kisha toa nne nyuma (9-4=5) basi mwanamke huyu anaweza kutoa yai kati ya siku ya 5 na 9 katika siku zake.



2.Mwanamke mwenye mzunguruko wa siku 32: tunaanza kutoa siku 12 nyuma kabla ya kupata hedhi yake (32-12=20) tonatoa siku nne tena nyuma (20-4=16) kwa hiyo mwanamke huyu anaweza kutoa yai kati ya siku ya 16 mpaka 20



Tumia mfano huu kwa kuitafuta siku yako ya kupata ujauzito. Kama utakuwa na maoni na maswali wasiliana nasi hapo chini.





                   



Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 2439


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Malezi ya mtoto mchanga na mama mjamzito
Post hii itakwenda kukuletea mambo kadhaa yanayohusiana na malezi bora ya mama mjamzito na mtoto mchanga Soma Zaidi...

Jinsi ya kushusha homoni za kiume.
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada. Soma Zaidi...

Kwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?
Je unaweza kunielezaKwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini? Soma Zaidi...

Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa?
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa. Soma Zaidi...

mim mjamzito lakini maumwa kiuno nakuacha nakuvuta ukeni wiki ya 39 na siku4
Soma Zaidi...

Siku za kupata mimba
Nitakujulisha siku ya kupata mimba na sifa zake, na namna ya kuweza kuitafuta Soma Zaidi...

Mishipa ya machozi kufunga kwa mtoto.
Posti inahusu nzaidi kufunga kwa mishipa ya machozi ya mtoto kwa kawaida mishipa ya mtoto inapaswa kufunguka baada ya mwaka mmoja lakini kwa wengine ubaki imefungwa hata baada ya mwaka mmoja na kusababisha madhara mbalimbali kwa mtoto. Soma Zaidi...

Maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada Soma Zaidi...

Huduma kwa wasioona hedhi
Posti hii inahusu zaidi msaada au namna ya kuwahudumia wale wasioona hedhi na wamefikiwa kwenye umri wa kuweza kuona hedhi. Soma Zaidi...

Kazi za homoni katika Mzunguko hedhi.
Post hii inahusu zaidi kazi za homoni katika Mzunguko wa hedhi, katika kipindi hiki kuna homoni mbalimbali ambazo ufanya kazi kama tutakavyoona. Soma Zaidi...