Mtoto wa tajiri na maskini (sehemu ya pili)
Post hii inahusu zaidi watoto wa wawili ambapo mmoja ni mtoto wa tajiri na mwingine ni mtoto wa maskini.
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini.
1.basi hao watoto wakiendelea kukua na kusoma shule na kila mtu na ratiba yake mmoja ratiba yake ya maisha ya kitajiri na mwingine maisha yake ya umaskini, katika maisha ya mitihani shuleni mtoto wa tajiri alikuwa anakuwa wa kwanza kwa sababu waalimu walikuwa wanahongwa ela na mtoto wa maskini alikuwa anakuwa wa pili au wa tatu kwa kutumia akili zake,
2. Basi ikafika wakati wa mtihani wa mwisho yaani kumaliza darasa la Saba, wazazi wa mtoto wa tajiri wakapiga akili namna ya kumsaidia mtoto wao kwa sababu alikuwa kilaza, kwa hiyo walienda kwa familia ya mtoto maskini na kusonga Hela kubwa na kishirikiana na waalimu kusudi mtoto wa tajiri akae karibu na mtoto wa maskini Ili wawe wanaonyeshana majibu, basi wale wazazi wakapewa Hela na yule mtoto wa maskini alihaidiwa kupewa laptop na simu kubwa baada ya kumaliza shule na yule mtoto alifurahi sana kusikia hivyo.
3. Na siku ya mtihani ikafika kwa sababu wale wazazi walikuwa na ela waliongea pia na msimamizi wa mtihani naye alikubali wakae wote kusudi wamwonyeshe majibu, basi mtihani ukaanza yule mtoto wa tajiri akakaa na mtoto wa maskini na akamwonyesha kila kitu na mtihani ukimalizika salama na pia matokeo yakatoka na kwa kuwa yule mtoto wa maskini alikuwa na akila sana alichaguliwa kwenye shule za vipaji maalumu na pia yule mtoto wa tajiri naye alichaguliwa kwenye shule za vipaji maalumu kwa sababu mtihani alifanyiwa na mtoto wa tajiri.
4. Basi matokeo yalipotoka yule baba tajiri alifurahi sana na akamwongezea yule mtoto wa maskini zawadi kubwa na akahaidi kumlipia karo ya mwaka wa form one, na siku zilifika za kwenda shule yule mtoto wa tajiri alikuwa na kila kitu kilichohitajika shuleni ila mtoto wa maskini alikuwa na karo aliyofadhiriwa nauli na madaftari, karamu na sabini pamoja na uniform, hali iliyomfanya kuridhika na alichonacho, kwa sababu safari ilikuwa ndefu mtoto wa maskini alifungiwa mhogho wa kula njiani na maji ila yule wa tajiri alifungiwa vitu vingi mno vya kula njiani.
Itaendelea
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Simulizi za Hadithi Audio π2 web hosting π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 Bongolite - Game zone - Play free game π5 Madrasa kiganjani π6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili,ambapo Mama yake na Jackie pamoja na jack wakiwa hospital na jack anaendelea kumwita Julius kila mara.
Soma Zaidi...SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu
Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, hapa tunaona Jackie anajibu barua ya Julius kwa kusema yafuatayo.
Soma Zaidi...Hadithi katika kijiji cha burugo
Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii .
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.
Soma Zaidi...Hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya Binti mfalme ni hadithi ya kusisimua, kuhusu hadithi hii ni kwamba mfalme alihitaji mtoto wa kiume ila wanawake wote hawakumpata ila alitokea mke mdogo mmoja wa mfalme akajifungua watoto wawili mapacha mmoja wa kiume na
Soma Zaidi...