Mtoto wa tajiri na maskini (sehemu ya pili)
Post hii inahusu zaidi watoto wa wawili ambapo mmoja ni mtoto wa tajiri na mwingine ni mtoto wa maskini.
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini.
1.basi hao watoto wakiendelea kukua na kusoma shule na kila mtu na ratiba yake mmoja ratiba yake ya maisha ya kitajiri na mwingine maisha yake ya umaskini, katika maisha ya mitihani shuleni mtoto wa tajiri alikuwa anakuwa wa kwanza kwa sababu waalimu walikuwa wanahongwa ela na mtoto wa maskini alikuwa anakuwa wa pili au wa tatu kwa kutumia akili zake,
2. Basi ikafika wakati wa mtihani wa mwisho yaani kumaliza darasa la Saba, wazazi wa mtoto wa tajiri wakapiga akili namna ya kumsaidia mtoto wao kwa sababu alikuwa kilaza, kwa hiyo walienda kwa familia ya mtoto maskini na kusonga Hela kubwa na kishirikiana na waalimu kusudi mtoto wa tajiri akae karibu na mtoto wa maskini Ili wawe wanaonyeshana majibu, basi wale wazazi wakapewa Hela na yule mtoto wa maskini alihaidiwa kupewa laptop na simu kubwa baada ya kumaliza shule na yule mtoto alifurahi sana kusikia hivyo.
3. Na siku ya mtihani ikafika kwa sababu wale wazazi walikuwa na ela waliongea pia na msimamizi wa mtihani naye alikubali wakae wote kusudi wamwonyeshe majibu, basi mtihani ukaanza yule mtoto wa tajiri akakaa na mtoto wa maskini na akamwonyesha kila kitu na mtihani ukimalizika salama na pia matokeo yakatoka na kwa kuwa yule mtoto wa maskini alikuwa na akila sana alichaguliwa kwenye shule za vipaji maalumu na pia yule mtoto wa tajiri naye alichaguliwa kwenye shule za vipaji maalumu kwa sababu mtihani alifanyiwa na mtoto wa tajiri.
4. Basi matokeo yalipotoka yule baba tajiri alifurahi sana na akamwongezea yule mtoto wa maskini zawadi kubwa na akahaidi kumlipia karo ya mwaka wa form one, na siku zilifika za kwenda shule yule mtoto wa tajiri alikuwa na kila kitu kilichohitajika shuleni ila mtoto wa maskini alikuwa na karo aliyofadhiriwa nauli na madaftari, karamu na sabini pamoja na uniform, hali iliyomfanya kuridhika na alichonacho, kwa sababu safari ilikuwa ndefu mtoto wa maskini alifungiwa mhogho wa kula njiani na maji ila yule wa tajiri alifungiwa vitu vingi mno vya kula njiani.
Itaendelea
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 ai web app 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.
Soma Zaidi...Hasara za wivu na kutokuwa wazi ( sehemu ya 2)
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu na kutokuwa wazi sehemu ya pili, sehemu hii inahusu mama Lisa anaenda kwa mama lina ili kuuliza kinachoendelea kwa mtoto wake , kwa hiyo tuona atapata jibu gani.
Soma Zaidi...Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)
Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa.
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili baada ya kuhamia shule mpya.
Soma Zaidi...Usichofahamu kuhusu mazoezi
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo hufahamu kuhusu mazoezi,ni mambo ambayo utokea au no matokeo mazuri kwa watu wanaofanya sana mazoezi.
Soma Zaidi...WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 1
Post hii inahusu zaidi hadithi mpya na nzuri inayoitwa wakati wa Kufumbuka, ni hadithi inayohusu maisha ya kawaida ambapo watu ushindwa kudhamini watu wa karibu nao na kuona watu wa mbali ndio wenye maana ila shida zikifika ndipo wanaona umuhimu wao.
Soma Zaidi...