image

WAKATI WA KUFUMBUKA

Post hii ni mwendelezo wa hadithi inayohusu Kufumbuka ambapo , John anaonekana kama sio mtoto wa Mzee maganga kwa sababu na miungu imekili kwa sababu chakula chote kimeliwa na kuisha.

WAKATI WA KUFUMBUKA. 

Wakati ulipofika kutangazwa kwamba John sio mtoto wa Mzee maganga watu wote walishangilia sana na kupiga makofi kwa sababu walijisikia vibaya kuona John anamsaidia Mama yake maria ,kwa sababu John alimpenda sana mama yake ,alipewa nafasi ya kuongea kwamba anasemaje na wengi wakidhani kwamba anataka kujitetea Ili kuendelea kuishi kwenye ukoo.kwa hiyo aliisimama akiwa ana uchungu mkubwa ,wengi wakidhani labda ana uchungu wa kutopokelewa kwenye ukoo ila kwake ulikuwa ni uchungu wa kuona roho mbaya za watu ambao wanawatenga wenzao hasa upande wa mama zao waliona hawana haki.

 

 Basa baada ya kuona John amesimama mda mrefu bila kuongea Mzee mmoja mwenye busara akamtoa John pembeni akamwambia kwamba unapaswa kuongea na ukoo kufuata Mila na desturi Ili uweze kuhudumiwa kama mtoto wa nyumba hii na ukoo huu kwa sababu miungu imekukataa na pia baba zako wamekukataa, John akatikisa kichwa sawa,kwa hiyo Mzee mmoja  akasimama mbele ya umati akasema kwamba kwa niaba ya John anapenda kuongea Ili kuweza kurudi kwenye ukoo kama mwana ukoo kwa sababu tangia utoto wake ameshiriki mema yote ya hapa na kila kitu kwa hiyo anaomba ukoo wa kununua na jamii iendelee kumpokea, wakamuuliza John yeye hakusema chochote kwa sababu alikuwa na hasira, basi mkutano ukahailishwa na kila mtu akarudi kwao.

 

Basi na John akamshika mama yake mkono wakaelekea nyumbani, yule kijana aliyeona jinsi wazee walivyokula zile nyama ,siku Moja kwa kujiiba alipaswa kwenda kwa John usiku mmoja,kwa sababu hawakuruhusiwa kwenda mchana ,kwa sababu hawakupaswa kuongea na mama yao pamoja na mjomba wao kadri ya familia hii upande wa mama hawakuudhamini, basi yule kijana akamwambia  John kila kitu kikafahamika, kwa hiyo wakapanga jinsi ya kuwaibisha jamii ya wazee Ili waweze kujenga msimamo wa kujali familia kwa usawa hasa upande wa mama.

 

Kwa kawaida kama mtoto akionekana hafai kwenye familia Ili kuweza kurudi kwenye familia hiyo ni lazima kutoa matoleo maalumu kama vile ngombe kumi, pombe vidumu kumi, kuku kumi, mbuzi kumi, na vyakula,na mambo hayo yalichinjwa na watu walikuja kusheherekea na kula na mtoto aliingizwa ndani kadri ya utaratibu. Kwa kawaida mtoto aliongea neno na kuomba kuingia kwenye ukoo,na pia Kuna Mzee aliyesimama kama msimamizi wa kijana, kwa hiyo vitu vilikuwa vingi kwa Vijana walilokuwa na uwezo wa Chini hali iliyosababisha kushindwa kupata ruhusa ya kurudi kwenye ukoo tena au kwa wakati mwingine walipewa ruhusa baada ya miaka mingi, ila kwa John kwa sababu ya kuwa na kipato kikubwa hiyo ilikuwa ni kazi ndogo kwake.

 

Kwa hiyo siku ikafika,Sheria ya kwanza ilikuwa ni kwamba John anapaswa kumtoa mama yake na mjomba wake kwenye nyumba yake na kuwapeleka kwenye nyumba ya watumishi wa kawaida na akishapata ruhusa ya kuingia kwenye ukoo hapaswi kutoa msaada wowote kwa mama na mjomba,hali hii ilimfanya mama kuogopa sana na kuendelea kupoteza matumaini, kwa hiyo John aliongea na mama na mjomba kuhusu lengo lake ambalo ni kuifumbua macho jamii  kwamba watu wote ni sawa na kwamba katika maisha ya makuzi ya mtoto Kuna pande mbili ambazo ni mama na baba na pia wote wanapaswa kupendwa.

 

Hali hii ilimfanya mama na John kuwa na matumaini ila waliogopa sana kwamba uenda na John akauawa kwa sababu ya kuipindua jamii kwamba ni vigumu baba na Mama kuwa sawa na upande wa mama kuwa sawa na upande wa baba, ila John akasema yeye yupo tayari kwa lolote Ila hawezi kuuawa , kwa kaida Mzee maganga alikuwa na majeshi mbalimbali ya kumlinda  kwa yeyote yule aliyeenda kinyume na Mzee maganga aliuwa, kwa hiyo John aliogopa sana kuhusu Ilio kwa hiyo akaunda jeshi lake akaliaandaa akampa mzee maganga kama zawadi akihaidi kwamba ni jeshi ambali litamlinda siku ya kuomba kuingia kwenye ukoo na Mzee maganga alifurahi sana akiwaambia wanajeshi wake kwamba siku ya sherehe hiyo wanapaswa kwenda kulinda mifugo sehemu ya mbali Ili wasije kuibiwa.

 

Kwa hiyo John akawaambia jeshi lake kwamba akiwa anaongea kuhusu kuifumbua jamii kwa kudhamini sehemu ya upande wa mama na kuona kwamba baba na mama wote ni sawa, Mzee maganga akiwaamulu kwamba ua huyo hastahili kuishi mnapaswa kusogea kwangu na kunibeba kwamba Nina haki na kuamulisha kwamba watu wote wakubali na atakayekataa mnamkata kichwa, Basi John akapaswa kuunda na jeshi la ziadi Ili kuzuia habari zisienee mpaka kwenye jeshi la Mzee maganga ambalo liko mbali Ili kuzuia vita kati ya jeshi la Mzee maganga na jeshi jipya la John. Basi na habari ikapita kwa ndugu wa John Ili John akitoa tamko waje wamembeba mama yao wakisema nani kama mama na washangilie ikiwa baba yao atachukia wote wanapaswa kuhamia kwa John kwa maandamano makubwa na kuwashurutisha wazee wote na ndugu kuandamana wakiimba wimbo ufuatao.

 

baba na mama wote ni wazazi,kuwaheshimu na kuwatunza ni kitu cha muhimu kwa sababu wote walishirikiana katika kumtunza na kumlea mtoto na tabia ya kudharau upande wa mama ni dhambi kubwa kwa sababu watu wote ni sawa na wote wanahotaji msaada na kuishi maisha mazuri na ya kumpenda aliyewaumba,

 

Wimbo huu uliimbwa kwa watumishi na washabiki wa John na pia jeshi lote la John wakifahamu wimbo huu, basi siku yenyewe ikafika na nyama zikachinjwa kila kitu kikapikwa na pia miungu nayo waliipatia chakula chake Ili Ile na baada ya kula ndipo wengine wafuate, kwa sababu wale wazee ndio waliokula chakula kile ,waliachwa waendelee na kazi zao za kula chakula Chao, na wakala baada ya kula na sherehe ikaanza, basi ikafika wakati wa  mtoto kuanza kuomba utambulisho wa kuwa mwana ukoo, akaenda yule Mzee aliyehaguliwa kwa kazi hiyo akasema enyi familia na ukoo wa Mzee maganga kwa heshima na taathima kufuatia agizo la ukoo wetu maalufu tukiwa na Sheria kwamba atakayevunja Sheria ya kuthamini mama yake na kutunza upande wa mama yake ni lazima aangaliwe vizuri inawezekana huyo mtoto sio wa familia hii.kwa sababu tatizo hili limemkuta kijana wetu John na ameumia sana na kwa moyo wote amehiari kuwa hatahusika tena na kuwa karibu na mama yake Wala kumjali mjomba wake kwa hiyo kwa kutumia Mali zake atawajali upande wa baba tu.

 

Basi watu wote wakashangilia na pia Mzee maganga aliamka kwenye kiti chake na kumkumbatia John na John akamkumbatia baba yake ila machozi yalimtoka na yalikuwa machozi ya hasira kwa sababu ya unyanyasaji wa upande wa Mama kwa hiyo John alipewa nafasi ya kuongea.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 523


Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili,ambapo Mama yake na Jackie pamoja na jack wakiwa hospital na jack anaendelea kumwita Julius kila mara. Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI (sehemu ya sita)
Post inahusu zaidi hadithi ya NIMLAUMU NANI ambayo ni sehemu ya sita, katika kipengele hiki tunaenda kumwona msichana Amina anapambana na hatimaye anafunga ndoa ya kiserikali na Frank Soma Zaidi...

WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 2
Post hii ni mwendelezo wa hadithi ambayo Kwa jina inaitwa wakati wa Kufumbuka, ni mwendelezo wa pale maria anawekwa mbele ya wazee Ili akili kwamba John sio mtoto wa Mzee maganga ila maria akikumbuka wazi kwamba John ni mtoto wa Mzee maganga anakataa kuki Soma Zaidi...

USALITI (sehemu ya pili)
Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya Usaliti kati ya Rhoda na Moses ambapo Moses anampenda sana Rhoda na wakati wa kuoa umefika ila akagikilia kwamba akimuoa Rhoda inawezekana wasipate watoto kwa sababu ya mimba ambazo Rhoda alikuwa anatoa mara kwa mara. Soma Zaidi...

NIMLAUM NANI? (Sehemu ya pili)
Post hii ni mwendelezo wa hadithi iliyopita ambapo Frank aliwakuta Amina ambaye ni mpenzi wake ameumbatiana na James ambaye ni rafiki yake ,kwa hiyo tuendelee kusikia yaliyotokea baada ya Amina na James kukutwa na Franki. Soma Zaidi...

Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)
Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa. Soma Zaidi...

SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu
Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo. Soma Zaidi...

Hadithi za alif lela u lela
Haya ni masimulizi ya Hadithi za alif lela u lela Soma Zaidi...

Hadithi katika kijiji cha burugo
Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii . Soma Zaidi...

Usichofahamu kuhusu mazoezi
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo hufahamu kuhusu mazoezi,ni mambo ambayo utokea au no matokeo mazuri kwa watu wanaofanya sana mazoezi. Soma Zaidi...

Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya tatu)
Post hii inahusu zaidi mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini wakipanda gari kuelekea shule kuanza maisha mapya. Soma Zaidi...