picha

Ni nini maana ya mlo kamili?

Mlo kamili ni mkusanyiko kuu wa vyakula mbalimba kwa pamoja huimarisha na kuujenga  mwili wa binadamu na wanyama kwa sababu vinaleta virutubishi vyote vinavyohitajika.  Mkusanyiko wa vyakula vinavyotengeneza mlo kamili Kuna majina ya vyakula

Protini

Protini ni kundi dogo la chakula linalofanya kazi ya kuujenga mwili. Protini hufanya kazi ya kuponesha vidonda na majerah ambayo mtu ameyapata katika mwili wake.mfani nyama,samaki,maharage,mayai,senene nk

 

Mafuta

Mafuta ni kundi dogo la chakula linalofanya kazi ya kuipa miili yetu joto. Vyakula hivi ni muhimu kwa watu wanaokaa maeneo au sehemu yenye baridi .

Mfano wa vyakula vinavyoipa miili yetu joto ni: mafuta,karanga,na alizeti

 

Wanga

Wanga ni kundi dogo la chakula linalofanya kazi ya kuiipa miili yetu nguvu. Vyakula vya wanga ni muhimu kwa sababu huipa miili yetu nguvu ambayo tunaitumia katika kufanya kazi mbalimbali; mfano wa kazi hizo ni: kutengeneza vitu mbalimbali n.k. mfano ugali,kande,mihogo,viazi n.k

Vyakula hivi ni muhimu kwa watu wanaofanya kazi nzito kwani huhitaji nguvu nyingi kwa ajili ya kazi nzito.

 

Vitamini

Vitamini ni kundi dogo la vyakula linalofanya kazi ya kuilinda miili yetu dhidi ya magonjwa mbalimbali.vyakula vya vitamin ni Kama vile Nanasi,chungwa,karoti,papai,n.k

Kuna vitamin A, B, C, D, E, B/1, B/2 n.k.

Vyakula vyenye vitamini A huzuia ugonjwa wa upungufu wa damu mwilini (anemia) ambao ni ukosefu wa vitamini hivyo

vyakula vyenye vitamini B huzuia ugonjwa wa beriberi

 vyakula vyenye vitamini C huzuia ugonjwa wa kiseyeye,

vyakula vyenye vitamini D huzuia ugonjwa wa matege 

vyakula vyenye vitamini E huzuia ugojwa wa via vya Uzazi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views 5452

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 web hosting     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Rangi za matunda

Fida za matunda huanzia kwenye rangi zake, je unajuwa kama rangi ya matunda inaeleza jambo?

Soma Zaidi...
Faida za kula Karoti

Umeshawahi kula karoti mbichi, ama ya kupikwa, je unazijuwa faida zake? soma makala hii

Soma Zaidi...
Nini maana ya protini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya protini

Soma Zaidi...