Menu



Vyakula kwa wagonjwa wa sukari na utaratibu wao wa lishe

Post hii inakwenda kukufundisha utaratibu wa lishe kwa wagonjwa wenye kisukari pamoja na vyakula salamakwao.

Matibabu ya ugonjwa wa kisukari yanagharimu fedha nyingi. Kwa hiyo ni muhimu kuzuia na kudhibiti athari za kisukari mapema. Ili kudhibiti ugonjwa wa kisukari mgonjwa anapaswa kupatiwa matibabu sahihi, kufuatilia na kupima hali yake ya afya mara kwa mara pamoja na kuzingatia mtindo bora wa maisha na taratibu zinazofaa za ulaji wa chakula.

 

Zifuatazo ni kanuni za ulaji unaofaa zinazopaswa kuzingatiwa na mgonjwa wa kisukari:

1.Kula mlo kamili (angalau mara 3 kwa siku) kwa kuzingatia muda mahususi aliojipangia kwani hashauriwi kukaa na njaa kwa muda mrefu.

 

2.Dhibiti kiasi cha nishati – lishe (wanga) katika chakula ili kisizidi mahitaji ya mwili. Kiasi kitegemee mahitaji ya mtu binafsi.

 

3.Ongeza ulaji wa vyakula vyenye makapi – mlo kwa wingi. Kiasi kikubwa cha nishati-lishe kitokane na vyakula vya asili ya nafaka isiyokobolewa, mizizi na ndizi za kupika. Sukari inayotoka katika vyakula hivi hufyonzwa kwa taratibu na hivyo kupunguza kasi ya ongezeko la sukari katika damu.

 

4.Punguza kiasi cha vyakula vinavyozalisha nishati lishe kwa wingi hususani vyakula vyenye mafuta kwa wingi.

 

5.Panga utaratibu wa kula chakula na matumizi ya dawa. Iwapo unatumia insulin au dawa za kushusha kiwango cha sukari katika damu unapaswa kujipangia muda wa kula chakula na kumeza dawa ili kuzuia kupungua kwa sukari katika damu. Epuka kukaa kwa muda mrefu bila kula chakula.

 

6.Kula mbogamboga kwa wingi katika kila mlo.

7.Kula tunda katika kila mlo.

8.Epuka kunywa pombe.

9.Epuka ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi kama soda, keki, biskuti, pipi na asali.

 

Kanuni nyingine za kuzingatia ni:

1.Punguza uzito iwapo una uzito uliozidi - au dhibiti uzito wa mwili ili usifikie uzito uliozidi. Ni muhimu kuwa na uwiano sahihi wa uzito wa mwili kulingana na urefu wako.

 

2.Zingatia usafi na usalama wa chakula

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1075


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Faida za juice ya tende.
Posti hii inahusu zaidi faida ya juice ya tende,ni juice inayotumiwa na watu wengi sana na wengine wanajua kabisa faida zake na kuna wengine hawajui wanaitumia kama mazoea tu, ila kuna ambao hawajui kabisa basi zifuatazo ni faida za juice ya tende kwa wal Soma Zaidi...

Vyakula salama na vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo
Kamala hii inakwenda kufundisha vyakuna na vinjwaji salama anavyopaswa kutumia mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Pia utajifunza vyakula na vinywaji hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Soma Zaidi...

Aina za vyakula ambayo huongeza damu kwa wajawazito na watoto
Hizi ni aina za vyakula ambavyo husaidia katika kuongeza damu kwa wajawazito na watoto. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Mbegu za mronge
Soma Zaidi...

Faida za vyakula vya asili
Posti hii inahusu zaidi faida za matumizi ya vyakula vya asili, kama tunavyojua kwamba mababu na mabibi zetu walitumia vyakula vya asili wakaishi miaka mingi kweli. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula korosho
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula korosho Soma Zaidi...

Faida za kitunguu swaumu wakati wa ujauzito
Posti hii inahusu zaidi faida za kitunguu swaumu wakati wa ujauzito, kuna kipindi ambacho wanawake wakati wa ujauzito uchaguza vyakula mbalimbali kuna ambao wanaweza kutumia vitunguu saumu na kupata faida kubwa Soma Zaidi...

Vinywaji salama kwa mwenye kisukari
Vijuwe vinywaji salama kwa mgonjwa wa kisukari Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula panzi, senene na kumbikumbi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula senene, panzi na kumbikumbi Soma Zaidi...

Faida za muarobaini
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za muarobaini Soma Zaidi...