Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo?
Hukumu ya Muislamu Aliyeacha Kufunga kwa Makusudi
Japo kadha ya Ramadhani inaruhusiwa kwa yule aliyeruhusiwa kutofunga kutokana na udhuru wa kisheria, kadha haitajuzu kwa mtu aliyeacha makusudi, kwani hata akifunga mwaka mzima hawezi kuilipia siku hiyo moja aliyoacha kufunga pasi na udhuru kwa ushahidi wa Hadith ifu atayo:
Abu Hurairah (r.a) amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Mwenye kula siku moja ya Ramadhani bila ya ruhusa iliyotolewa na Mwenyezi Mungu, basi Swaum hiyo hailipiki hata akifunga mwaka mzima. (Abu, Daud, Ibn Majah n a Tirm idh).
Fundisho kubwa tunalolipata hapa ni kuwa kuacha makusudi kutekeleza amri ya Allah katika wakati wake uliowekwa ni jambo baya sana hata kama utatekeleza amri hiyo wakati mwingine. Ikumbukwe kuwa anachokiangalia Allah (s.w) si utekelezaji wa vitendo tu, bali huangalia na kumlipa mja kutokana na utii na unyenyekevu katika kufanya kitendo alicho kiamrisha.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Hii ni orodha ya watu ambao wanaweza kurithi malibya marehrmu.
Soma Zaidi...- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke?
Soma Zaidi...Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.
Soma Zaidi...