picha

Namna ya kutekeleza swala ya maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Utaratibu wa kusimamisha swala ya maiti ni kama ifuatavyo;

  1. Maiti iwekwe mbele.
  2. Imamu asimame katikati ya mwili wa maiti ikiwa maiti ni ya kike, na usawa wa mabega kama maiti ni ya kiume.
  3. Maamuma watasimama kwenye mistari (safu) kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, n.k.
  4. Baada ya hapo swala itaanza na kuendelea kama ifuatavyo:
    1. Nia - ambayo ni kukusudia moyoni.
    2. Kuleta takbira ya kwanza; kwa kusema, “Allaah Akbar”
    3. Imamu na maamuma watasoma suratul-Faatiha – kimya kimya.
    4. Imamu ataleta Takbira ya Pili kisha maamuma – kimya kimya kwa maamuma na si lazima kuinua mikono wao. 
    5. Kumswalia Mtume (s.a.w) kama ilivyo katika Tahiyyatu, wote – kimya kimya.
    6. Imamu ataleta takbira ya Tatu kisha maamuma- kama walivyofanya awali.
    7. Wote kumuombea maiti dua kimya kimya, ikiwemo: 

“Allaahumma ghfir lihayyinaa wamaayyitinaa washaahidinaa waghaaibinaa waswaaghirinaa wakaabirinaa wadhakirnaa waunthaanaa. Allaahumma man ahyaytahuu minnaa faahyi ‘alal Islaam. Waman tawaffaytahuu minnaa tawaffahuu ‘alal Imaani. Allaahumma laa tahirimnaa ajirahuu walaa taftinaa ba’adahuu”

    Tafsiri:

“Ewe Allah tusamehe sisi, na maiti wetu, na mashahidi, na wasiokuwepo miongoni wetu, vijana wadogo miongoni mwetu na wakubwa miongoni mwetu, wanamume wetu, na wanawake wetu. Ewe Allah, yeyote yule miongoni mwetu utakayemewezesha kuishi, mjaalie aishi katika Kiislamu na yeyote miongoni mwetu utakayemfisha, mfishe katika Imani (ya Kiislamu). Ewe Allah, usitukatishe ujira kutoka kwake na wala usitufitinishe baada yake.” 

 

            -   Au kwa kifupi tuweza kumuombea maiti kama ifuatavyo;

                “Allaahumma ghfir lahuu warhamhuu wa-afihii wa-afu-anhu”

            Tafsiri:

                “Ewe Allah, Mghufirilie na Umrehemu”.

 

  1. Imamu ataleta Takbira ya nne na maamuma kufuatihia kama awali.
  2. Wote watawaombea waislamu dua – (pia si lazima kuleta dua hii).

Rejea Qur’an (59:10).

 

  1. Imamu kutoa salaam na maamuma kufuatishia bila kutoa sauti kama ilivyo kwenye swala ya kawaida kwa kusema; 

        “Assalaamu ‘alaykum Warahmatullaah (Wabarakaatuh)”

    Tafsiri:

        “Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake”.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/02/Sunday - 02:58:48 pm Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1642

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

Tofauti kati ya zakat na sadaqat

Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Fadhila za usiku waalylat al qadir

Zijuwe fadhila za usiku wenye cheo kuliko nyusiku ya miezi 1000.

Soma Zaidi...
Nini maana ya twahara katika uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya twahara katika uislamu. Pia utakwenda kujifunza hukumu za twahara, aina za twahara na mambo mengineyo

Soma Zaidi...
Haki za kiuchumi za mwanamke katika uislamu

Haki za UchumiKuwa imara kiuchumi ni sababu mojawapo kubwa ya kumpa mtu hadhi katika jamii.

Soma Zaidi...
Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?

Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu?

Soma Zaidi...