image

Zaka katika mapambo, mali ya biashara na mali iliyofukuliwa ardhini

Zaka katika mapambo, mali ya biashara na mali iliyofukuliwa ardhini

Zaka ya mapambo ya dhababu na fedha, mali ya bishara na mali iliyofukuliwa ardhini



(iv)Vito (mapambo )vya Dhahabu na Fedha



Mapambo ya dhahabu na fedha yameharamishwa kwa Waislamu Wanaume. Wanawake wenye mapambo ambayo kiasi cha dhahabu au fedha kilichopo kwenye mapambo hayo kinafikia Nissab,wanalazimika kutoa Zakat kila mwaka unapopindukia.



Zainab mke wa Abdullah(r.a) ameeleza: Mtume wa Allah alituhutubia na akasema: “Enyi jumuia (mkusanyiko wa) wa wanawake! Toeni Zakat hata kutoka kwenye mapambo yenu, kwa sababu katika wakazi wa motoni mtakuwa w engi zaidi katika siku ya Kiyama ” (Tirmidh).



Amr bin Shuaib(r.a) amesimulia kutoka kwa baba yake na baba yake alisema kuwa wanawake wawili walikuja kwa Mtume (s.a.w) na bangili mbili za dhahabu wamevaa mikononi mwao Mtume aliwauliza “mmelipa Zakat yake” ‘Hapana’, walijibu. Kisha Mtume (s.a.w) akawauliza: ‘Mngetaka kwamba Allah awavalishe bangili za moto?’ ‘Hapana ’ walijibu. Alisema (Mtume): “Basi lipeni Zakat yake ” (Tirmidh).



(v)Mali yakuchimbuliwa chini ya ardhi au mali ya kuokota



Mali iliyofukuliwa chini au madini hutolewa ushur au Zakat kiasi cha moja ya tano (1/5 au 20%) ya thamani ya mali hiyo kama tunavyofahamishwa katika Hadith.
Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “... Na kuna moja ya tano (1/5) inayolazimu kutolewa Zakat kutokana na mali iliyo chini ya ardhi”. (Bukhari na Muslim).



Hadith hii inatufahamisha kuwa mali yoyote iliyochimbuliwa chini ya ardhi ambayo haikuwa na mmiliki yoyote kabla ya hapo, itakuwa ni halali kwa aliyeigundua na kuichimbua lakini atalazimika kutoa ushuru au kiwango cha Zakat kiasi cha 1/ 5 au 20% ya mali hiyo. Hali kadhalika mali yoyote ya kuokota iliyokosa mwenyewe baada ya kutangazwa kwa muda mrefu wa kutosha unaokubalika katika sharia ya kiislamu inakuwa ni mali ya mwenye kuokota, na atalazimika kuitolea Zakat kiasi cha 1/5 au 20% ya mali hiyo. Mali ya kuchimbuliwa chini au mali ya kuokota haina Nisaab wala haina muda bali Zakat yake hutolewa pale pale inapopatikana.



(vi)Mali ya Biashara
Bidhaa za biashara pamoja na fedha taslimu zinatakiwa zihesabiwe na kutolewa Zakat baada ya mwaka kupindukia.
Samura bin Jundab (r.a) ameeleza: Mtume wa Allah alikuwa akituelekeza tukusanye Zakat kutoka kwenye vile tulivyovihesabu kama bidhaa (za biashara). (Abu Daud).



Bidhaa za biashara zitatolewa Zakat kwa kuthamanishwa na fedha taslim kwa kiasi cha 1/40 au 2.5% ya mali yote ya bidhaa zote za biashara. Kwa hiyo mali ya biashara nisaab yake itakuwa sawa na nisaab ya fedha au dhahabu. Tofauti na dhahabu, fedha na fedha taslim ambazo hutolea Zakat baada ya kukaa kwa kipindi cha mwaka mmoja, bidhaa za biashara si lazima zikae kwa kipindi cha mwaka mmoja ndio ijuzu Zakat juu yake bali kila mwisho wa mwaka, mfanyabiashara atahesabu bidhaa zake zote anazozifanyia biashara na kuzitolea Zakat kwa kiwango cha 2.5%. Hapana Zakat juu ya vifaa vinavyotumika kwa matumizi ya nyumbani au vitendea kazi. Kwa mfano, nyumba za kufanyia kazi kama vile maduka, ofisi, na hoteli, mashine za kufanyia kazi, samani za nyumbani, ofisini dukani, hotelini, n.k. magari ya kusafiria na kusafirishia bidhaa, vyote hivi havistahiki kutolewa Zakat.



Kwa msisitizo zaidi Zakat inajuzu tu kwa mali inayotengenezwa kwa ajili ya kuuzwa au mali inayonunuliwa kwa ajili ya kuuzwa; kwa mfano magari yaliyonunuliwa au nyumba zilizotengenezwa kwa ajili ya kuuzwa zitatolewa Zakat kila mwisho wa mwaka.Jambo muhimu linalotakiwa lizingatiwe kabla ya kutoa Zakat ni madeni. Ni sharti madeni na haki nyingine zote za watu zitolewe ndio mali ihesabiwe kwa ajili ya Zakat.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 397


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Tofauti kati ya hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

nguzo za uislamu: Kutoa zaka, lengo la kutoa zaka na faida zake
Kutoa Zakat. Soma Zaidi...

Ni kwa nini lengo la Funga na swaumu halifikiwi na wafungaji?
Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji Wengi? Soma Zaidi...

Fiqh.
Kipengele hichi tutajifunza chimbuko la fiqh na maana ya figh. Soma Zaidi...

Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf Soma Zaidi...

Namna ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.
Post hii inakwenda kukugundisha jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji
Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu. Soma Zaidi...

Kuandama kwa Mwezi na Kufunga ama kufungua ramadhani, sheria na hukumu za kuangalia mwezi
Soma Zaidi...

Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii
4. Soma Zaidi...

Riba na Madhara Yake Katika Jamii
- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara. Soma Zaidi...

Nyakati za swala za dharura swala ya mgonjwa na mafiri
Soma Zaidi...

Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu funga za sunnah na jinsi ya kuzigunga. Soma Zaidi...