Wanaostahiki kupewa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa mujibu wa Qur’an (9:60) na (2:273), wanaostahiki kupewa Zakat ni waislamu tu katika makundi yafuatayo;

  1. Fukara.

-    Ni kundi la wale wasiojiweza kwa chochote cha kumudu maisha yao kabisa ya kila siku bila kusaidiwa.

 

  1. Maskini.

-    Ni wale wasio na uwezo wa kupata mahitaji yao ya msingi ya kimaisha ila wana uwezo wa kujikimu kwa kiasi fulani tu.

 

  1. Wanaozitumikia (Al-A’miliina A’laihaa).

-    Ni wale wote wanaozikusanya na kuzigawanya kwa wanaohusika bila kujali uwezo wao.

 

  1. Wanaotiwa nguvu nyoyo zao juu ya Uislamu.

-    Ni wale walioingia katika Uislamu karibuni na wanahitajika kuimarishwa imani zao juu ya Uislamu.

 

  1. Kuwakomboa Watumwa (Fir-riqaabu).

-    Ni kuwakomboa au kuwanunua watumwa au watu wote wanaoishi chini ya miliki ya watu (mabwana) na kuwaachia huru.


 

  1. Kuwasaidia wanaodaiwa kulipa madeni yao.

-    Ni kuwalipia waislamu madeni yao waliokopa ili kujikimu kimaisha lakini bila kukusudia wameshindwa kulipa deni zao.

 

  1. Kutumika Katika njia ya Allah (s.w).

-    Ni kutumika katika shughuli zote zinazopelekea kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.

 

  1. Kuwasaidia Wasafiri walioharibikiwa njiani (Ibnis-sabiil).

 -    Msafiri yeyote muislamu aliyeharibikiwa kwa kupoteza, kuibiwa au kuishiwa mali yake hata kama ni tajiri, ni wajibu kupewa zakat.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1814

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 web hosting    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini

Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha.

Soma Zaidi...
Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa

Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii.

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala?

Je kusimamisha swala kuna maana gani kwenye uislamu?

Soma Zaidi...
Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika post hii utajifunza maana ya twahara kiligha na kishria. Pia utajifunza umuhimu wake

Soma Zaidi...
Nafasi ya serikali katika ugawaji

Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi.

Soma Zaidi...
Mambo yanayotenguwa udhu

Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu.

Soma Zaidi...