Uchumi Katika Uislamu
Maana ya Uchumi
- Ni uzalishaji, usambazaji na utumiaji wa mali, rasilimali na huduma mbalimbali katika jamii ili kujenga mahusiano kati ya binaadamu na Allah (s.w).
Sifa za Uchumi wa Kiislamu
1. Dhana ya mafanikio
Huzingatia hatima yake ambayo ni kupata radhi za Allah (s.w) pekee.
2. Dhana ya umilikaji mali
Mmiliki hakika wa pekee wa mali na rasilimali zote ni Allah (s.w).
3. Dhana ya bidhaa
Ni kitu kilicho safi, kizuri, twahara, halali, n.k.
4. Dhana ya matumizi
Haifai kufuja au kutumia mali au rasilimali kwa njia za haramu.
5. Mizani ya wakati katika kutumia
Ni kujiuliza, nini matokeo ya mali au rasilimali hiyo baada ya muda fulani?
Njia na Misingi ya Uchumi Halali Katika Uislamu
i. Pasiwe na udanganyifu wowote katika uuzaji na ununuzi wa bidhaa au mali.
Rejea Qurโan (17:35), (26:181-183), (83:1-4)
ii. Pasiwe na viapo katika kuuza au kununua bidha, kwani ni miongoni mwa kuuza kwa ujanja-ujanja.
Abu Qatada ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:
โKuwa mwangalifu na viapo vingi katika uuzaji, kwa sababu japo
kunarahisisha uuzaji, kuna punguza barakaโ (Muslim).
iii. Pawe na uhuru kamili kwa mnunuzi kuikataa au kuikubali bidhaa baada ya kuiangalia.
iv. Bidhaa yenyewe iwe halali na iwe imechumwa kwa misingi ya halali pia.
v. Kuwepo na maelewano kati ya muuzaji na mnunuzi bila masharti. Dosari yeyote ya bidhaa ijulikane kabla ya manunuzi kufanyika.
vi. Muuzaji awe na uhuru wa kuuza bidhaa yake kwa bei yenye maslahi kwake na isiwe ya kumnyonya mnunuzi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir
Soma Zaidi...Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya.
Soma Zaidi...Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.
Soma Zaidi...Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...