image

Nini maana ya kusimamisha swala

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.

Maana ya Kusimamisha Swala

Kusimamisha swala ni tofauti na kuswali. Kuswali ni kufanya vitendo vya swala kama vile kusimama, kurukuu, kuitidali, kusujudu, n.k. Kusimamisha swala ni kuitekeleza swala kwa kuchunga na kutekeleza kwa ukamilifu yafuatayo:

 


(i)Sharti zote za swala.
(ii)Nguzo zote za swala.
(iii)Kuwa na khushui (unyenyekevu) wakati wote wa kutekeleza sharti na nguzo za swala.

 


Mtu akiswali bila ya kuzingatia na kutekeleza kwa ukamilifu mambo haya matatu, ataonekana kuwa kaswali, lakini atakuwa hajasimamisha swala na atastahiki kuadhibiwa vikali na Mola wake kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:

 


“Basi adhabu kali itawathibitikia wanaoswali, ambao wanapuuza swala zao (kwa kutozisimamisha), ambao hufanya ria ”. (107:4-6)


Kupuuza swala ni pamoja na kutotekeleza ipasavyo sharti za swala, nguzo za swala, na kutokuwa na unyenyekevu wakati wa kutekeleza sharti na nguzo za swala.


Hivyo, swala inayokubalika mbele ya Allah (s.w) ni ile iliyosimamishwa kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

 

“Hakika wamefuzu w aumini ambao katika swala zao ni wanyenyekevu ”. (23:1-2)
“Na ambao swala zao w anazihifadhi” . (23:9)
Kuhifadhi swala ni kutekeleza kwa ukamilifu sharti na nguzo zote za swala.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 966


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Lengo la kusimamisha swala kwa mwanadamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la kusimamisha swala. Soma Zaidi...

Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Zoezi la nne mada ya fiqh.
Maswali mbalimbali kuhusu fiqh. Soma Zaidi...

Namna ya kujitwaharisha mkojo wa Mtoto mdogo Najisi Hafifu
Soma Zaidi...

namna ya kuswali swala ya msafiri, nguzo zake na hukumu zake
Soma Zaidi...

Tofauti kati ya zakat na sadaqat
Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Matendo ya hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara Soma Zaidi...

Mambo yasiyoharibu Swaumu na Kufunguza mwenye kufunga
Soma Zaidi...

DARSA ZA SWALA NA NMNA YA KUSWALI SWALA ZA SUNA NA FARAHDI, SHARTI NA NGUZO NA SUNA ZA SWALA
Soma Zaidi...

Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?
Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga? Soma Zaidi...

nyakati za swala
3. Soma Zaidi...